NEC Dodoma: Nafasi ya mwisho kwa JK kutetea urais wake na kulinda Tanzania yetu

omarilyas

JF-Expert Member
Jan 24, 2007
2,130
145
Katika siku za hivi karibuni "vigogo" wa CCM wanakutana mjini dodoma kama halmashauri kuu ya chama ambayo kwa kawaida hufuata kikao cha kamati kuu. Ni wazi kuwa baada ya uovu wa EPA na dafalau la BUTIAMA rais Kikwete analazimika kutumia nafasi hii kuthibitisha umuhimu wa yeye kuwa rais wa Tanzania. JK anapaswa kufanya na kutekeleza maamuzi mazito sio tu kunusuru urais wake kutoka kwa makucha ya maifisadi na wahafidhina wa kundini mwake lakini pia kulinda Tanzania yetu ambayo inategemea sana hadhi na uhalali wa urais wake katika taasisi za kiserikali na jamii kwa ujumla.

JK anapaswa kufunga macho na kuamuru utekelezaji wa hatua kali kwa mafisadi ama watenda maovu kwa lugha ya Ki-CCM na vilevile kuonyesha uzito wa nafasi yake kama Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kuwashurutisha mahafidhina ama wateka nyara wa mapinduzi ya Zanzibar kukubali kuunda muundo wa kiserekali utakoweza kushughulikia mizizi ya matatizo ya Zanzibar. Kama serikali ya mseto ama serikali ya mpito yote sawa.

JK akifanya makosa ya kusita kufanya maamuzi na kutekeleza hayo mazito ni wazi safari ya uchaguzi 2010 itakuwa ngumu lakini zaidi mafisadi wetu watachukua mwanya kuvuruga urais wake. Hili litapelekea kutoa nafasi kwa mafisadi ama wale wapya ama wale wazoefu waliosafishwa hivi karibuni kujigeuza kuwa wakombozi wetu. Hawa watapata nguvu za kuchezea asasi ya urais kwa manufaa yao na mbaya zaidi "watanzania wa kawaida" ambao ndio nguzo kuu ya urais wa JK wataaminishwa kuwa kweli jamaa ni msanii ama hovyo na wao (mafisadi wapya, mafisadi wazoefu na wale mashuhuri na wasio mashuhuri) ndio kweli wanaweza kuwasaidia watanzania. Fikiria pale yule tuliyekuwa tunamwita ZERO ambaye sasa ni msomi wa IVY LEAGUE na aliyesafishwa na gazeti la MUHINGO anapoanza kuwa chaguo mbadala la mswahili Jakaya........

Zaidi ya hayo ni wazi kuwa bila ya JK kuchukua hatua thabiti za kuonekana juu ya watenda maovu maarufu, angalao wale mabronso wa EPA, atakuwa amewaacha watanzania mikononi mwa matapeli wa kisiasa kina KIMARO, Mama Malecela, Mwakyembe na wengine kujichukulia umaarufu katika kikao cha bunge kinachoanza kesho...

Na wakishindwa hao kuendelea kuwapiga bao watanzania basi wajue watanzania wako tayari kuchukua hatua kivyaovyao, kwanza watajaribu adhabu za kijamii kama kuwazomea, kuwasusa, kuwatenga wao na vizizvyao.....na hilo likishindikana tusubiri kile ambacho hatukifikirii...

Ndugu zangu mliopewa dhamana ya kulinda asasi ya URAIS....chonde msiache nafasi hii ya mwisho kupita....ioneeni huruma Tanzania yenu hata kama mko mguu ndani mguu nje.....mwambieni ukweli mkuu wenu bila uoga wala unafiki, hilo ndio jukumu lenu kuu....

Tanzanianjema
 
Zaidi ya hayo ni wazi kuwa bila ya JK kuchukua hatua thabiti za kuonekana juu ya watenda maovu maarufu, angalao wale mabronso wa EPA, atakuwa amewaacha watanzania mikononi mwa matapeli wa kisiasa kina KIMARO, Mama Malecela, Mwakyembe na wengine kujichukulia umaarufu katika kikao cha bunge kinachoanza kesho...


Na wewe nawe, umeanza vizuri lakini hapo ndio umeharibu kabisa. Sasa hao kwa nini unawaita matapeli wa kisiasa au wivu unakusumbua? Haya mapambano yanahitaji kona mbalimbali, hatuwezi kuyashinda kwa kutegemea watu wachache unaowataka wewe-sio ni akina nani hao ambao kwako sio matapeli. Acha kukatisha watu tamaa. Na hilo limkutana unalishabikia la nini wakati wanakwenda kujipanga namna ya kudhibiti habari za wizi wao zisisambae. Yaani hadi leo unaendelea kuwa na matumaini na Kikwete, ama kwa kweli watanzania wengine ni kichwa ngumu hasa na sikio la kufa halisikii dawa!
 
Hawa watu katiba ionawalinda na wao pia wanalindana,usitegemee jipya zaidi ya kuambiana kama huwezi kaa pembeni.
 
Huyu bwana atakuwa kahongwa na Rostam Aziz awaite wapiganaji wetu matapeli, siyo bure ana ajenda ya siri.
 
Na wewe nawe, umeanza vizuri lakini hapo ndio umeharibu kabisa. Sasa hao kwa nini unawaita matapeli wa kisiasa au wivu unakusumbua? Haya mapambano yanahitaji kona mbalimbali, hatuwezi kuyashinda kwa kutegemea watu wachache unaowataka wewe-sio ni akina nani hao ambao kwako sio matapeli. Acha kukatisha watu tamaa. Na hilo limkutana unalishabikia la nini wakati wanakwenda kujipanga namna ya kudhibiti habari za wizi wao zisisambae. Yaani hadi leo unaendelea kuwa na matumaini na Kikwete, ama kwa kweli watanzania wengine ni kichwa ngumu hasa na sikio la kufa halisikii dawa!

WATANZANIA NDIO WALIWAO!!!!! amen
 
Huyu bwana atakuwa kahongwa na Rostam Aziz awaite wapiganaji wetu matapeli, siyo bure ana ajenda ya siri.


Simple mind at work.....no wonder CHENGE akawa mwenyekiti wa maadili CCM na akathubutu kulalama kuwa Tanzania inaelekea pabaya na sio kuwa yeye na wenziwe wameipeleka pabaya
 
Mtu yeyote anayempa JK "nafasi ya mwisho" anahitaji kupewa nafasi ya mwisho.
 
Bwana Tz njema ata kama uu mwanachama mwadilifu wa CCM haingii akilini hao watu kuwaita matepeli ata kama ndugu zako wa karibu wamekumbwa na yale walioyaongea.
Suala apa ni maslai ya Taifa and not otherwise I mean tuepuke unazi usio na msingi.
Ila sishangai watanzania wengi ni wagumu wa kubadilika that being the case wataendelea kulizwa uku cost of living ikipaa na standard ya maisha ikishuka.
Jamani tubadilike izi sio zama za bora liende,tz itajengwa na watz wenyewe
 
Zaidi ya hayo ni wazi kuwa bila ya JK kuchukua hatua thabiti za kuonekana juu ya watenda maovu maarufu, angalao wale mabronso wa EPA, atakuwa amewaacha watanzania mikononi mwa matapeli wa kisiasa kina KIMARO, Mama Malecela, Mwakyembe na wengine kujichukulia umaarufu katika kikao cha bunge kinachoanza kesho.
Tanzanianjema

Wabunge kutetea wananchi wake tayari wanaitwa Matapeli wa kisiasa, mmmmh...!! Sasa kama Mama Malecela, Kimaro na Mwakyembe wakiwa matapeli wa kisiasa na WEWE UTAKUWA NANI?? Mie nafikiri wewe ndiye tapeli unataka kutapeli watu hapa JF waamini unachokisema. Ulianza vizuri lakini topic yako ikaaribiwa na utapeli huo ulioingiza hapo. Anyway tunaheshimu kile unachoamini.
 
JK nafasi yake ya mwisho ilikuwa Butiama ambako pia aligalagazwa vya kutosha. Nafikiri sasa hivi hiyo nafasi imeisha kwisha, kinachosubiriwa ni labda kundi la wabunge wachukue initiative zao.
 
Wabunge kutetea wananchi wake tayari wanaitwa Matapeli wa kisiasa, mmmmh...!! Sasa kama Mama Malecela, Kimaro na Mwakyembe wakiwa matapeli wa kisiasa na WEWE UTAKUWA NANI?? Mie nafikiri wewe ndiye tapeli unataka kutapeli watu hapa JF waamini unachokisema. Ulianza vizuri lakini topic yako ikaaribiwa na utapeli huo ulioingiza hapo. Anyway tunaheshimu kile unachoamini.

Tatizo sio kutetea wananchi bali ni character na kilichowapelekea kufanya hivyo. Hivi kwani hao watatu tu ndio "wanaotetea" wananchi? Mbona sijawataja wengineo?

Nilishawahi kusema hapa kuwa katika Tanzania ya matatizo kama hii kuna hatari ya watanzania kupata MASIHA FEKI. Na kwangu mimi hili ni hatari kuliko hao wa vijisenti tulionao. Nakuhakikishia hao niliowataja nawajua vilivyo kijamii na kisiasa na wote nisingependa kuona watanzania wanajidanganya kuwa ni watetezi wao.

Hata hivyo sishangai wewe kuwa na muono huo kwani hilo ni kawaida kisiasa kama ilivyo kawaida kwa matapeli wa kisiasa kuibuka katika nyakati hatari kama hizi.....

Tanzanianjema
 
Tumekuwa tukiwakera,
niliamua kukaa kimya,
ila hakuna maana,
Mie nataka wakubali yaishe,

Jakaya ataondoka leo jioni kwenda Dodoma kwa kazi mbili

1.Kwa ajili ya kikao
2.Kushinikiza Wabunge waipitishe Bajeti itakayosomwa leo jioni maana ni mbmovu na haina msaada wowote

JE, kwa kuangalia yanayoendelea leo nchini, kuna sababu yoyote ya kuendelea kupambana na ufisadi au tukubali yaishe? ..Mzee Mwanakijiji
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom