omarilyas
JF-Expert Member
- Jan 24, 2007
- 2,130
- 145
Katika siku za hivi karibuni "vigogo" wa CCM wanakutana mjini dodoma kama halmashauri kuu ya chama ambayo kwa kawaida hufuata kikao cha kamati kuu. Ni wazi kuwa baada ya uovu wa EPA na dafalau la BUTIAMA rais Kikwete analazimika kutumia nafasi hii kuthibitisha umuhimu wa yeye kuwa rais wa Tanzania. JK anapaswa kufanya na kutekeleza maamuzi mazito sio tu kunusuru urais wake kutoka kwa makucha ya maifisadi na wahafidhina wa kundini mwake lakini pia kulinda Tanzania yetu ambayo inategemea sana hadhi na uhalali wa urais wake katika taasisi za kiserikali na jamii kwa ujumla.
JK anapaswa kufunga macho na kuamuru utekelezaji wa hatua kali kwa mafisadi ama watenda maovu kwa lugha ya Ki-CCM na vilevile kuonyesha uzito wa nafasi yake kama Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kuwashurutisha mahafidhina ama wateka nyara wa mapinduzi ya Zanzibar kukubali kuunda muundo wa kiserekali utakoweza kushughulikia mizizi ya matatizo ya Zanzibar. Kama serikali ya mseto ama serikali ya mpito yote sawa.
JK akifanya makosa ya kusita kufanya maamuzi na kutekeleza hayo mazito ni wazi safari ya uchaguzi 2010 itakuwa ngumu lakini zaidi mafisadi wetu watachukua mwanya kuvuruga urais wake. Hili litapelekea kutoa nafasi kwa mafisadi ama wale wapya ama wale wazoefu waliosafishwa hivi karibuni kujigeuza kuwa wakombozi wetu. Hawa watapata nguvu za kuchezea asasi ya urais kwa manufaa yao na mbaya zaidi "watanzania wa kawaida" ambao ndio nguzo kuu ya urais wa JK wataaminishwa kuwa kweli jamaa ni msanii ama hovyo na wao (mafisadi wapya, mafisadi wazoefu na wale mashuhuri na wasio mashuhuri) ndio kweli wanaweza kuwasaidia watanzania. Fikiria pale yule tuliyekuwa tunamwita ZERO ambaye sasa ni msomi wa IVY LEAGUE na aliyesafishwa na gazeti la MUHINGO anapoanza kuwa chaguo mbadala la mswahili Jakaya........
Zaidi ya hayo ni wazi kuwa bila ya JK kuchukua hatua thabiti za kuonekana juu ya watenda maovu maarufu, angalao wale mabronso wa EPA, atakuwa amewaacha watanzania mikononi mwa matapeli wa kisiasa kina KIMARO, Mama Malecela, Mwakyembe na wengine kujichukulia umaarufu katika kikao cha bunge kinachoanza kesho...
Na wakishindwa hao kuendelea kuwapiga bao watanzania basi wajue watanzania wako tayari kuchukua hatua kivyaovyao, kwanza watajaribu adhabu za kijamii kama kuwazomea, kuwasusa, kuwatenga wao na vizizvyao.....na hilo likishindikana tusubiri kile ambacho hatukifikirii...
Ndugu zangu mliopewa dhamana ya kulinda asasi ya URAIS....chonde msiache nafasi hii ya mwisho kupita....ioneeni huruma Tanzania yenu hata kama mko mguu ndani mguu nje.....mwambieni ukweli mkuu wenu bila uoga wala unafiki, hilo ndio jukumu lenu kuu....
Tanzanianjema
JK anapaswa kufunga macho na kuamuru utekelezaji wa hatua kali kwa mafisadi ama watenda maovu kwa lugha ya Ki-CCM na vilevile kuonyesha uzito wa nafasi yake kama Rais wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kuwashurutisha mahafidhina ama wateka nyara wa mapinduzi ya Zanzibar kukubali kuunda muundo wa kiserekali utakoweza kushughulikia mizizi ya matatizo ya Zanzibar. Kama serikali ya mseto ama serikali ya mpito yote sawa.
JK akifanya makosa ya kusita kufanya maamuzi na kutekeleza hayo mazito ni wazi safari ya uchaguzi 2010 itakuwa ngumu lakini zaidi mafisadi wetu watachukua mwanya kuvuruga urais wake. Hili litapelekea kutoa nafasi kwa mafisadi ama wale wapya ama wale wazoefu waliosafishwa hivi karibuni kujigeuza kuwa wakombozi wetu. Hawa watapata nguvu za kuchezea asasi ya urais kwa manufaa yao na mbaya zaidi "watanzania wa kawaida" ambao ndio nguzo kuu ya urais wa JK wataaminishwa kuwa kweli jamaa ni msanii ama hovyo na wao (mafisadi wapya, mafisadi wazoefu na wale mashuhuri na wasio mashuhuri) ndio kweli wanaweza kuwasaidia watanzania. Fikiria pale yule tuliyekuwa tunamwita ZERO ambaye sasa ni msomi wa IVY LEAGUE na aliyesafishwa na gazeti la MUHINGO anapoanza kuwa chaguo mbadala la mswahili Jakaya........
Zaidi ya hayo ni wazi kuwa bila ya JK kuchukua hatua thabiti za kuonekana juu ya watenda maovu maarufu, angalao wale mabronso wa EPA, atakuwa amewaacha watanzania mikononi mwa matapeli wa kisiasa kina KIMARO, Mama Malecela, Mwakyembe na wengine kujichukulia umaarufu katika kikao cha bunge kinachoanza kesho...
Na wakishindwa hao kuendelea kuwapiga bao watanzania basi wajue watanzania wako tayari kuchukua hatua kivyaovyao, kwanza watajaribu adhabu za kijamii kama kuwazomea, kuwasusa, kuwatenga wao na vizizvyao.....na hilo likishindikana tusubiri kile ambacho hatukifikirii...
Ndugu zangu mliopewa dhamana ya kulinda asasi ya URAIS....chonde msiache nafasi hii ya mwisho kupita....ioneeni huruma Tanzania yenu hata kama mko mguu ndani mguu nje.....mwambieni ukweli mkuu wenu bila uoga wala unafiki, hilo ndio jukumu lenu kuu....
Tanzanianjema