Mikael Aweda
JF-Expert Member
- Dec 17, 2010
- 2,973
- 3,901
Sikuamini macha yangu, nikasoma magazeti mpaka matatu ili nijiaminishe, sasa nimeamini kuwa JK ni msanii wa kutupwa.
Baada ya Lowasa kujitetea kuhusu Richmond na kufanikiwa kumhusisha JK na Richmond, pia alimtuhumu Nape kwa kumchafua yeye ( Lowasa) bila ushahidi, alifuatia waziri mkuu mstaafu Sumaye ambaye pamoja na maelezo mengine ya kumtetea Lowasa alihoji, tuwafanyeje Nape na Chiligati ikiwa kamati ya maadili itamsafisha Lowasa? aliuliza Sumaye.
Hii ni kutokana na kwamba hawa akina Nape wameshazunguka nchi nzima kumchafua Lowasa kama bw Lowasa alivyotuambia. Kitu ambacho sikutegemea,
JK alikadakia kauli ya Sumaye na kusema, watachukuliwa hatua za kinidhamu.
Sakata hili ni baada ya NEC kukubaliana na pendekezo la CC ya NEC lilisomwa na Pius Msekwa la kuomba suala kujivua gamba lirudishwe ktk kamati ya maadili, hoja ambayo ilipita.
My take,
Mbele ya macho yangu, ndani ya ukumbi wa Diamond Jubilee mwaka 2011, JK akiwa mgeni Rasmi ktk tamasha Nyimbo za Injili alituambia, Nape anayoyazungumza kuhusu gamba siyo maneno yake mwenyewe bali ya ccm - ndiyo kazi tuliyomtuma.
Jana alisema kama ikidhihirika ktk kamati ya maadili kuwa Nape alimtuhumu Lowasa Bila kufuata utaratibu wa chama basi atachukuliwa hatua za kinidhamu.
Ikumbukwe kwamba;
Hoja mojawapo ya Lowasa na Sumaye ni kwamba, kwa nini suala la Lowasa halikupelekwa ktk kamati ya maadili kama ilivyotaratibu za Chama na badala yake Nape akalikimbiza ktk vyombo vya habari?
Pili, Ikimbukwe kuwa ktk maelezo ya Lowasa alisema, Mkiti unakumbuka ukiwa nje ya nchi, nilikupigia kukushauri kuwa tuvunje mkataba wa Richmond, wewe ukasema ngoja tusikie ushauri wa kamati ya makatibu wakuu ambao ndo waliosababisha mkataba usivunjwe?
Tatu, mkiti unafahamu kuwa hakuna jambo nililofanya ambalo sijakushirikisha, kila kitu unajua.
Nne, Lowasa akiwa ameshika hansard ya Bunge aliuliza ripoti ya Richmond haijasema nimehusika, ilisema ninapaswa kuwajibishwa kutokana na makosa ya watendaji walioko chini yangu.
My take 2
Nini hatma ya Nape Ndani ya CCM?
Je, tukisema kuwa ccm imefika mwisho huu utakuwa ni ushabiki wa kisiasa?
Je, Lowasa kufanikiwa kumhusisha JK na Richmond moja kwa moja, JK atapata wapi ujasiri wa kuendeleza zoezi la kuwavua wengine gamba au kupambana na ufisadi.
Je, kama zoezi la uvuaji wa gamba likihitimishwa kwa staili hii, nini kitawafanya watz wasiichague Chadema 2015?
je, hoja ya Chadema ya Ufisadi ambayo waliiparamia sasa si itawabakiza magamba kweli.
Baada ya Lowasa kujitetea kuhusu Richmond na kufanikiwa kumhusisha JK na Richmond, pia alimtuhumu Nape kwa kumchafua yeye ( Lowasa) bila ushahidi, alifuatia waziri mkuu mstaafu Sumaye ambaye pamoja na maelezo mengine ya kumtetea Lowasa alihoji, tuwafanyeje Nape na Chiligati ikiwa kamati ya maadili itamsafisha Lowasa? aliuliza Sumaye.
Hii ni kutokana na kwamba hawa akina Nape wameshazunguka nchi nzima kumchafua Lowasa kama bw Lowasa alivyotuambia. Kitu ambacho sikutegemea,
JK alikadakia kauli ya Sumaye na kusema, watachukuliwa hatua za kinidhamu.
Sakata hili ni baada ya NEC kukubaliana na pendekezo la CC ya NEC lilisomwa na Pius Msekwa la kuomba suala kujivua gamba lirudishwe ktk kamati ya maadili, hoja ambayo ilipita.
My take,
Mbele ya macho yangu, ndani ya ukumbi wa Diamond Jubilee mwaka 2011, JK akiwa mgeni Rasmi ktk tamasha Nyimbo za Injili alituambia, Nape anayoyazungumza kuhusu gamba siyo maneno yake mwenyewe bali ya ccm - ndiyo kazi tuliyomtuma.
Jana alisema kama ikidhihirika ktk kamati ya maadili kuwa Nape alimtuhumu Lowasa Bila kufuata utaratibu wa chama basi atachukuliwa hatua za kinidhamu.
Ikumbukwe kwamba;
Hoja mojawapo ya Lowasa na Sumaye ni kwamba, kwa nini suala la Lowasa halikupelekwa ktk kamati ya maadili kama ilivyotaratibu za Chama na badala yake Nape akalikimbiza ktk vyombo vya habari?
Pili, Ikimbukwe kuwa ktk maelezo ya Lowasa alisema, Mkiti unakumbuka ukiwa nje ya nchi, nilikupigia kukushauri kuwa tuvunje mkataba wa Richmond, wewe ukasema ngoja tusikie ushauri wa kamati ya makatibu wakuu ambao ndo waliosababisha mkataba usivunjwe?
Tatu, mkiti unafahamu kuwa hakuna jambo nililofanya ambalo sijakushirikisha, kila kitu unajua.
Nne, Lowasa akiwa ameshika hansard ya Bunge aliuliza ripoti ya Richmond haijasema nimehusika, ilisema ninapaswa kuwajibishwa kutokana na makosa ya watendaji walioko chini yangu.
My take 2
Nini hatma ya Nape Ndani ya CCM?
Je, tukisema kuwa ccm imefika mwisho huu utakuwa ni ushabiki wa kisiasa?
Je, Lowasa kufanikiwa kumhusisha JK na Richmond moja kwa moja, JK atapata wapi ujasiri wa kuendeleza zoezi la kuwavua wengine gamba au kupambana na ufisadi.
Je, kama zoezi la uvuaji wa gamba likihitimishwa kwa staili hii, nini kitawafanya watz wasiichague Chadema 2015?
je, hoja ya Chadema ya Ufisadi ambayo waliiparamia sasa si itawabakiza magamba kweli.