"Ndugunization" ni tatizo kubwa Tanzania. It must be tackled from the roots, vinginevyo italiangamiza taifa

Mathanzua

JF-Expert Member
Jan 4, 2017
15,814
20,657
"Ndugunization" ni neno la zamani ambalo lilitoholewa kutoka kwenye lugha ya Kiswahili.Kwa Kiingereza ni 'Nepotism'.Neno hili lina maana ya kumpendelea mtu ambaye ni ndugu katika vitu kama ajira nk.Hata hivyo mimi nitalitumia neno hili nikiwa na maana ya 'kumpendelea mtu yeyote aliyekaribu nawe ili aweze kupata chochote kitakachomsaidia katika maisha yake.'

Mwalimu Nyerere alikemea sana tabia hii,hasa kwa kuwa alijua 'ndugunization' ina athari mbaya katika ustawi wa taifa.'Ndugunization' au nepotism inaweka watu wasiostahili sehemu mbalimbali wasizostahili na hivyo kuzorotesha utendaji kwa ujumla katika taifa katika nyanja zote za uzalishaji,utoaji huduma na hata katika siasa.Ni cancer mbaya katika taifa na jamii, ambayo inatakiwa kuchukiwa na kila mwana jamii.

Kwa bahati mbaya tumeona tabia hii ikiendelea kuimarika katika taifa letu, ndani ya serikali,mashirika mbali mbali na hata kwenye nyanja za siasa, jambo ambalo ni hatari kwa ustawi wa taifa kama nilivyosema.Tulishuhudia jinsi watoto wa viongozi mbali mbali walivyokuwa wamejazana Bank Kuu,tunaona jinsi watoto wa viongozi wa Wizara na mashirika mbali mbali walivyojazana katika taasisi hizo.Wakati mwingine najiuliza,hivi vijana wetu wasio na ndugu in responsible positions au connections, wao wakaponee wapi?Alienation hii ni mbaya na italigharimu taifa sana.Ni bomu ambalo linasubiri kupasuka.Nadhani ifike mahali Watanzania wote kwa ujumla wetu tuchukie vice hii,ili kila Mtanzania apate stahiki yake.'Ndugunization' italiangamiza taifa,we all have to say no to this very old-fashioned menace.Kama vile taifa lilivyovalia njuga swala la ufisadi,vyeti feki na ukwepaji kodi,ni vema pia taifa likaelekeza nguvu zake katika swala hili.
 
Hebu taja mlolongo wa watu au viongozi waliopata nyazifa kwa sababu ya "..ndugunization.."

vinginevyo Acha hofu za kufikirika
 
="Saguda47, post: 24671521, member: 364706"]Hebu taja mlolongo wa watu au viongozi waliopata nyazifa kwa sababu ya "..ndugunization.."

vinginevyo Acha hofu za kufikirika
Aseme amemlenga nani hasa.
 
Hii kitu inaharibu sana,hata ambao tunaona wapo vizur na wenyewe wamepatikana kupitia hii njia. Utalalamika mwishowe itabidi ukubaliane na hali tu.
 
sekta ya sheria nadhani imo miongoni mwa zile zinazoongoza kwa ukabila na kujuana;
Mkuu ni kila sekta aisee,iwe jeshini,kwenye dini,elimu n.k Kama upo huko na hauna wa kujuana naye juu tambua umefeli sana. Huku nilipo kuna jamaa n askar JWTZ ana V tatu lakini maisha anayoishi anawazidi kwa mbali maofisa. Huku nilipo elimu,kuna watu nimeanza nao kazi,kila gap linalotokea kama kusimamia na kusahihisha wamo tu kila mwaka,mimi nabaki kushangaa tu.
 
Hebu taja mlolongo wa watu au viongozi waliopata nyazifa kwa sababu ya "..ndugunization.."

vinginevyo Acha hofu za kufikirika
It's nonsense kufanya hivyo na wala hiyo sio nia ya bandiko hili.Unayekataa kwamba tatizo hili halipo ni lazima utakuwa mnufaika.Tatizo hili lipo, mwenye nia ya kweli ya ustawi wa taifa letu anajua.Swali ni how we can tackle the problem,denial haitatusaidia sana,it will only deepen the crisis.
 
Hata wabunge viti maalumu chadema huteuliwa na mbowe kwa unduginization
 
Mkuu ni kila sekta aisee,iwe jeshini,kwenye dini,elimu n.k Kama upo huko na hauna wa kujuana naye juu tambua umefeli sana. Huku nilipo kuna jamaa n askar JWTZ ana V tatu lakini maisha anayoishi anawazidi kwa mbali maofisa. Huku nilipo elimu,kuna watu nimeanza nao kazi,kila gap linalotokea kama kusimamia na kusahihisha wamo tu kila mwaka,mimi nabaki kushangaa tu.
Pole sana kijana, jipe moyo,yana mwisho.
 
It's nonsense kufanya hivyo na wala hiyo sio nia ya bandiko hili.Unayekataa kwamba tatizo hili halipo ni lazima utakuwa mnufaika.Tatizo hili lipo, mwenye nia ya kweli ya ustawi wa taifa letu anajua.Swali ni how we can do it,denial haitatusaidia sana.
yawezekana lipo sana tu, lakini kama mlalamikaji huna facts then no one will work on it!! nafaham kada za kiulinzi zimejaza ndugu....
 
"Ndugunization" ni neno la zamani ambalo lilitoholewa kutoka kwenye lugha ya Kiswahili.Neno hili lina maana ya kumpendelea mtu ambaye ni ndugu katika vitu kama ajira nk.Hata hivyo mimi nitalitumia neno hili nikiwa na maana ya 'kumpendelea mtu yeyote aliyekaribu nawe ili aweze kupata chochote kitakachomsaidia katika maisha yake.'

Mwalimu Nyerere alikemea sana tabia hii,hasa kwa kuwa alijua 'ndugunization' ina athari mbaya katika ustawi wa taifa.'Ndugunization' inaweka watu wasiostahili sehemu mbalimbali na hivyo kuzorotesha utendaji kwa ujumla katika taifa katika nyanza zote za uzalishaji,utoaji huduma na hata katika siasa.Ni cancer mbaya katika taifa, ambayo inatakiwa kuchukiwa na kila mtu.

Kwa bahati mbaya tumeona tabia hii ikiendelea kuimarika katika taifa letu, ndani ya serikali,mashirika mbali mbali na hata kwenye nyanja za siasa, jambo ambalo ni hatari kwa ustawi wa taifa kama nilivyosema.Tulishuhudia jinsi watoto wa viongozi mbali mbali walivyokuwa wamejazana Bank Mkuu,tunaona jinsi watoto wa viongozi wa Wizara na mashirika mbali mbali walivyojazana katika taasisi hizo.Wakati mwingine najiuliza,hivi Watanzania wasio na ndugu in responsible positions, wao wakaponee wapi?Alienation hii ni mbaya na italigharimu taifa sana.Nadhani ifike mahali Watanzania wote kwa ujumla wetu tuchukie vice hii,ili kila Mtanzania apate stahiki yake.'Ndugunization' italiangamiza taifa,we all have to say no to this very old-fashioned menace.Kama vile taifa lilivyovalia njuga swala la ufisadi,vyeti feki na ukwepaji kodi,ni vema pia taifa likaelekeza nguvu zake katika swala hili.
Ya sasa inaitwa bashitenization iko palepale alipokuwa Mwalimu. Mtathubutu?
 
Back
Top Bottom