safuher
JF-Expert Member
- Feb 11, 2019
- 11,161
- 15,839
Sehemu za kujifunza uvumilivu wewe ndo unajifunza ususuavu.Huyu anayemtongoza mke wangu kila siku alikuwa jamaa yangu wa karibu, nilisoma naye O-Level kisha nikaja fanya naye kazi. Alikuwa karibu hivyo haikuwa ngumu mimi kumpa namba ya mke wangu.
Hasa sababu mke wangu ana wivu sana so sometimes nikitaka kutoka namwambia jamaa ampigie wife amwombe kuwa tunatoka wote.
Jamaa alianza kumsifia sifia wife kama utani baadaye nikakata kabisa ukaribu naye nilipoona anazidi sana kutaka ukaribu. Mwishowe akaanza mwambia wife kuwa mimi nina diversions nyingi sana, si mwaminifu.
Akaendelea na kuanza tuma texts za mapenzi n.k wife akawa ananionesha. Sasa ameomba kabisa game na anaomba iwe kesho au kesho kutwa yeye atakuwa free aende na wife popote atakapo.
Nimemwambia wife akubali, wamepanga kila kitu na jamaa katuma 50,000 ya uber ili wife asitumie gari yake.
Sasa nawaza adhabu ya kwenda mpa jamaa. Maana ile 50,000 yake na nyingine nitakodisha watu watatu. Tutaenda sehemu hiyo, nataka nimfanye kitu ambacho yaani akija sikia kuwa mwanamke ameolewa awe anakimbia huku analia kabisa.
Sitaki polisi wala nini, naombeni msaada wenu. Adhabu ya kufaa kabisa. Sitaki muua, nataka aishi akijutia jambo hilo milele. Nyie si mnaona sisi tuliooa hatuna maana? Basi haina shida...wallah atasimulia maana ntamwachia ulimi ili aweze simulia wenzie.
Nisaidieni ushauri wa Adhabu, sitaki maneno ya sijui polisi, sijui ushauri nasaha. Nataka Ushauri wa adhabu ya kufaa hasa ili iwe fundisho na kwa wengine.
Kumuoa mwanamke haina maana kuwa hatotongozwa na wengine,kuoa mwanamke maana yake haruhusiwi kuolewa na wengine kwa sasa ni mkeo.
Achana nae,maisha haya bwana we chukulia simple tu