Wakudadavuwa
JF-Expert Member
- Feb 17, 2016
- 17,506
- 15,997
Wasalaam,
Kwanza nianze kwa watakia kila laheri na mandalizi ya sherehe za mwisho wa mwaka na pia kuwatakia heri ya mwaka mpya wa 2019 watanzania wote.
kwa kumkumbuka rafiki, shemeji na mdogo wangu aliyetangulia mbele za haki miezi michache iliyopita katika mwaka huu wa 2018 Dr.Misanya Bingi . Nimeanza kwa kumkumbuka sababu tulizoea kuitana shemeshi sababu mkewe ni mchagga. Nakumbuka miaka ya mwishoni mwa 90 na mwanzoni 2000 tulikuwa tunakutana mitaa jijini Dar es salaam katika bar maarufu ya Maryland ambapo palikuwa ni karibu na ofisi za ITV/RADIO one ambapo alikuwa ni mtangazaji.
Hapa Maryland ndipo hasa kulizaa mada ambayo marehemu Misanya aliamua kuipeleka redioni baada ya hoja niliyoizua katika bar hiyo tukiwa na wengine ambao wengi ni marehemu akina Moses Justine, Julius Nyaisangah bila kumsahau kaka yangu Charles Hilary. Mada ilihusu siri ya kabila la wachaga na mtoto wa kwanza, kama ilivyo kawaida vijana wengi wa kichagga walipendelea kuoa na kuacha wake zao kwenye vijiji vyao na kisha kwenda mijini na mambo yalipo kaa sawa ndipo familia zao ziliwafuata mijini.
Hoja kuu ilikuwa katika familia nyingi za kichagga mtoto wa kwanza ni wa ‘babu’, yaani wakati kijana yupo mjini ilibidi mzee ‘amsaidie’ mwanaye. Mada hii ilirindima na ilileta mjadala mkubwa mijini na vijijini hususani maeneo ya Dar na Kilimanjaro haswa ukizingatia Radio One ilikuwa inasikilizwa kwa wingi sana maeneo hayo na Minsanya Bingi alikuwa ni kivutio kikubwa kwa wasikilizaji. Pamoja na malalamiko kutoka kwa baadhi ya wachagga kudhalilishwa ilisaidia vijana wengi kutoacha wake zao vijijini na ndipo kwa sasa vijana wengi wa kichagga wanaoanza maisha wamekuwa wakiambatana na wake zao.
Ajizi nyumba ya njaa, tatizo hili sasa limerudi upya katika mtindo tofauti, kwa sasa mtoto wa kwanza ni wa kijana mwenyewe. Hatahivyo, mbio za maisha na tama ya pesa na mtindo wa maisha umewafanya wanaume wengi wa kichagga kusahau wake zao hivyo watoto wengi wa katikati kuzaliwa huwa si wao. Na utafiti usio rasmi umeonyesha watoto hao mimba zao hutungwa kipindi cha mwisho wa mwaka ambapo wanawake hutangulizwa vijijini kujipanga kwa ajili ya matambiko na sikukuu za mwisho wa mwaka.
Kumekuwa na tabia ya wanaume kusafiri kuja Moshi tarehe 24 usiku huku wake zao na watoto wakitangulia wiki kadhaa sasa hapa kumekuwa ni upenyo wa wanawake ‘’waliotelekezwa’’mijini kufurahia uanamke wao na kujikuta wakipata mimba. Pia kwa wafanyabiashara wa Kariakoo wanawake wengi wameonekana wakivinjari kwa siri na wafanyabiashara wadogo wadogo (wamachinga) kutokana na ‘ubize’ na ulevi wa waume zao.
Wito wangu ni kuwa tunapokuja Moshi wanaume wakichagga wakati tunazungumzia maisha na kufanya matambiko tulizungumie hili suala la tutalea na kugharamia visivyo vyetu. Tutakosa vyote mwishowe yaani mali na familia.
Kwanza nianze kwa watakia kila laheri na mandalizi ya sherehe za mwisho wa mwaka na pia kuwatakia heri ya mwaka mpya wa 2019 watanzania wote.
kwa kumkumbuka rafiki, shemeji na mdogo wangu aliyetangulia mbele za haki miezi michache iliyopita katika mwaka huu wa 2018 Dr.Misanya Bingi . Nimeanza kwa kumkumbuka sababu tulizoea kuitana shemeshi sababu mkewe ni mchagga. Nakumbuka miaka ya mwishoni mwa 90 na mwanzoni 2000 tulikuwa tunakutana mitaa jijini Dar es salaam katika bar maarufu ya Maryland ambapo palikuwa ni karibu na ofisi za ITV/RADIO one ambapo alikuwa ni mtangazaji.
Hapa Maryland ndipo hasa kulizaa mada ambayo marehemu Misanya aliamua kuipeleka redioni baada ya hoja niliyoizua katika bar hiyo tukiwa na wengine ambao wengi ni marehemu akina Moses Justine, Julius Nyaisangah bila kumsahau kaka yangu Charles Hilary. Mada ilihusu siri ya kabila la wachaga na mtoto wa kwanza, kama ilivyo kawaida vijana wengi wa kichagga walipendelea kuoa na kuacha wake zao kwenye vijiji vyao na kisha kwenda mijini na mambo yalipo kaa sawa ndipo familia zao ziliwafuata mijini.
Hoja kuu ilikuwa katika familia nyingi za kichagga mtoto wa kwanza ni wa ‘babu’, yaani wakati kijana yupo mjini ilibidi mzee ‘amsaidie’ mwanaye. Mada hii ilirindima na ilileta mjadala mkubwa mijini na vijijini hususani maeneo ya Dar na Kilimanjaro haswa ukizingatia Radio One ilikuwa inasikilizwa kwa wingi sana maeneo hayo na Minsanya Bingi alikuwa ni kivutio kikubwa kwa wasikilizaji. Pamoja na malalamiko kutoka kwa baadhi ya wachagga kudhalilishwa ilisaidia vijana wengi kutoacha wake zao vijijini na ndipo kwa sasa vijana wengi wa kichagga wanaoanza maisha wamekuwa wakiambatana na wake zao.
Ajizi nyumba ya njaa, tatizo hili sasa limerudi upya katika mtindo tofauti, kwa sasa mtoto wa kwanza ni wa kijana mwenyewe. Hatahivyo, mbio za maisha na tama ya pesa na mtindo wa maisha umewafanya wanaume wengi wa kichagga kusahau wake zao hivyo watoto wengi wa katikati kuzaliwa huwa si wao. Na utafiti usio rasmi umeonyesha watoto hao mimba zao hutungwa kipindi cha mwisho wa mwaka ambapo wanawake hutangulizwa vijijini kujipanga kwa ajili ya matambiko na sikukuu za mwisho wa mwaka.
Kumekuwa na tabia ya wanaume kusafiri kuja Moshi tarehe 24 usiku huku wake zao na watoto wakitangulia wiki kadhaa sasa hapa kumekuwa ni upenyo wa wanawake ‘’waliotelekezwa’’mijini kufurahia uanamke wao na kujikuta wakipata mimba. Pia kwa wafanyabiashara wa Kariakoo wanawake wengi wameonekana wakivinjari kwa siri na wafanyabiashara wadogo wadogo (wamachinga) kutokana na ‘ubize’ na ulevi wa waume zao.
Wito wangu ni kuwa tunapokuja Moshi wanaume wakichagga wakati tunazungumzia maisha na kufanya matambiko tulizungumie hili suala la tutalea na kugharamia visivyo vyetu. Tutakosa vyote mwishowe yaani mali na familia.