sindesunde
JF-Expert Member
- Dec 21, 2018
- 358
- 346
Kama kichwa habari dunia imenizonga kwakua inawezakana nilipata furaha ya wazazi kwakua naambiwa baba yangu alifariki nikiwa na miaka 4 napata akili namuona mama angu na kwenda kabulini kwa baba na mama ila hisia maelezo naambiwa nimefanana na mzee!kwa kifupi baada ya kufariki mzee maisha yalibadirika sana kwa maelezo ya bi mkubwa maisha yalikua poa ila baada ya mzee kufariki ndugu walizingua ila poa mtoto wa kiume nikapambana na mama yangu akiwa mama ntilie bi mkubwa akapambana sana mpaka ananianziasha darasa la kwanza pale shuleni umri ushasonga sana miaka 10 naanziswa darasa la kwanza!ila nilikua poa na waalimu walinikubali kwakukua mama yangu aliwaambia ukweli juu ya hali zetu kwa hiyo sikua napata vipingamizi sana ata baadhi ya ofa kama daftari vitabu nilikua napendelewa nikapiga nikafika darasa la pili hapo hakuna cha ndugu upande wa baba angu !Naanza darasa la pili kwa shida nafika darasa 3 mziki ukawa mzito zaidi bi mkubwa akaanza kuumwa kansa ambayo ndio ilioperekea kufariki.lkn bi mkubwa akukuta tamaa mpaka namliza darasa la 7 muda hua alirudi kwao kwa wajomba zangu baada ya hali kua mbaya sana kwake maana muhimbili walisema awamuwezi il niliisi kwa kua atukua na pesa na wajomba zangu ni watu wanaitaji sana pesa kuliko utu.Mtambue muda wote hapo kati nishakaa kwa ndugu na maisha ya utumwa nayajua zaidi Itaindelea