Nikukumbushe
JF-Expert Member
- Jun 4, 2013
- 2,602
- 408
Kusema kuwa mtu/kitu kife hiyo sio dhamira njema.Ndg wassira alisema mwaka 2013 CHADEMA lazima ife alikuwa na dhamira gani? Katika hali ya kawaida huwezi kuua chama kama hujaua watu,kwani chama hakiundwi na miti bali ni watu. Kutokana na kauli yake hii, ni dhahiri kuwa kauli ya WASSIRA iko katika utekelezaji, kwa kutumia ufahamu mdogo tu ambao haumhitaji mtu kuwa na PhD huwezi kuua chama kama haujaua viongozi, wanachama na washabiki wa chama, chama kinaundwa na watu sio miti wala nyasi.
Ndg Wassira, kauli zako hizi zinatutia mashaka na kuweka hisia na tuhuma zetu juu yako, kwani inawezekana unaratibu mambo haya kupitia jeshi la polisi, kwanza cheo chako kinasanifu yaliyotokea. Waziri mzima unatoa kauli kama hii, huku ukijua ni mwakilishi wa serikali, umeipaka matope serikali yako na chama chenu.
Najua hakuna jingine linalowapa hofu bali ni hofu ya kuachia dola. Na hofu hii inatokana na maovu mliyoyafanya kwenye utawala wenu yakiwemo ufisadi, rushwa, mikataba hewa, ujangili, utoroshaji wa pesa za walipa kodi, mauaji ya raia wasio na hatia.
Kwa taarifa tu, CCM haiwezi kutawala milele daima, mwisho wenu upo tu. Na jiandaeni kuficha sura zenu baada ya kutoka madarakani kwa kuzomewa kama mbwa.
NCHI HII SIYO YA CCM NA SERIKALI YAKE ,BALI NI YA WATANZANIA WOTE.
Ndg Wassira, kauli zako hizi zinatutia mashaka na kuweka hisia na tuhuma zetu juu yako, kwani inawezekana unaratibu mambo haya kupitia jeshi la polisi, kwanza cheo chako kinasanifu yaliyotokea. Waziri mzima unatoa kauli kama hii, huku ukijua ni mwakilishi wa serikali, umeipaka matope serikali yako na chama chenu.
Najua hakuna jingine linalowapa hofu bali ni hofu ya kuachia dola. Na hofu hii inatokana na maovu mliyoyafanya kwenye utawala wenu yakiwemo ufisadi, rushwa, mikataba hewa, ujangili, utoroshaji wa pesa za walipa kodi, mauaji ya raia wasio na hatia.
Kwa taarifa tu, CCM haiwezi kutawala milele daima, mwisho wenu upo tu. Na jiandaeni kuficha sura zenu baada ya kutoka madarakani kwa kuzomewa kama mbwa.
NCHI HII SIYO YA CCM NA SERIKALI YAKE ,BALI NI YA WATANZANIA WOTE.