Mtoto wa Shule
JF-Expert Member
- Nov 16, 2014
- 11,641
- 8,576
Dogo, kwa kutamka kuwa Polepole ndiye "aliyesimamia" mchakato wa kumfukuza Membe ujue umemkweza sana ndani ya CCM na hivyo anapaswa "kuogopwa". Ebu fikiria, CCM ina Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti Bara na Zanzibar, Secretariat chini ya Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu Bara na Zanzibar. Bado kuna Kamati ya Wenyeviti na Makamu Wenyeviti Wastaafu Taifa, Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa, lakini bado unasema " eti" Katibu Mwenezi wa Chama Taifa ndio "alisimamia" mchakato wa kumfukua Membe chamani? Aisee, huyo MTU usimbeze!!!Sote tunakumbuka ya kwamba Polepole akiwa katibu mwenezi wa CCM Taifa, alisimamia mchakato wa kumfukuza uanachama Membe kwa kosa la "kutamka" kwamba atachukuwa fomu ya kugombea Urais ili apambane na aliyekuwa Rais na mwenyekiti wa CCM Taifa ndugu Magufuli.
Kwa kutumia "kanuni za chama" Polepole alibariki ubakwaji huu wa katiba ya nchi na ile ya chama na kuidhinisha Membe afukuzwe chamani.
Hivi sasa Polepole "anatamka" maneno ya makufuru ya kupingana na sera na uongozi wa mwenyekiti wa ccm taifa, mama Samia.
Nini kinaizuia CCM hii kutumia kanuni zile zile zilizotumika kumfukuza Membe uanachama, zisitumike kumfukuza Polepole??