Ndugu wanaCCM, Wembe alioutumia Polepole kumnyolea Membe kwanini usitumike sasa kumnyoa Polepole?

Sote tunakumbuka ya kwamba Polepole akiwa katibu mwenezi wa CCM Taifa, alisimamia mchakato wa kumfukuza uanachama Membe kwa kosa la "kutamka" kwamba atachukuwa fomu ya kugombea Urais ili apambane na aliyekuwa Rais na mwenyekiti wa CCM Taifa ndugu Magufuli.

Kwa kutumia "kanuni za chama" Polepole alibariki ubakwaji huu wa katiba ya nchi na ile ya chama na kuidhinisha Membe afukuzwe chamani.

Hivi sasa Polepole "anatamka" maneno ya makufuru ya kupingana na sera na uongozi wa mwenyekiti wa ccm taifa, mama Samia.

Nini kinaizuia CCM hii kutumia kanuni zile zile zilizotumika kumfukuza Membe uanachama, zisitumike kumfukuza Polepole??
Dogo, kwa kutamka kuwa Polepole ndiye "aliyesimamia" mchakato wa kumfukuza Membe ujue umemkweza sana ndani ya CCM na hivyo anapaswa "kuogopwa". Ebu fikiria, CCM ina Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti Bara na Zanzibar, Secretariat chini ya Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu Bara na Zanzibar. Bado kuna Kamati ya Wenyeviti na Makamu Wenyeviti Wastaafu Taifa, Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa, lakini bado unasema " eti" Katibu Mwenezi wa Chama Taifa ndio "alisimamia" mchakato wa kumfukua Membe chamani? Aisee, huyo MTU usimbeze!!!
 
  • Thanks
Reactions: G4N
Dogo, kwa kutamka kuwa Polepole ndiye "aliyesimamia" mchakato wa kumfukuza Membe ujue umemkweza sana ndani ya CCM na hivyo anapaswa "kuogopwa". Ebu fikiria, CCM ina Mwenyekiti, Makamu Mwenyekiti Bara na Zanzibar, Secretariat chini ya Katibu Mkuu na Naibu Katibu Mkuu Bara na Zanzibar. Bado kuna Kamati ya Wenyeviti na Makamu Wenyeviti Wastaafu Taifa, Kamati Kuu na Halmashauri Kuu ya Taifa, lakini bado unasema " eti" Katibu Mwenezi wa Chama Taifa ndio "alisimamia" mchakato wa kumfukua Membe chamani? Aisee, huyo MTU usimbeze!!!
Duuh! Kwa ufafanuzi huu kumbe mwenezi ni kajitu fulani kasiko na kazi chamani. Sasa kwann huwa makatibu waenezi CCM hichomoza na kuonekana kama watu muhimu sana ndani ya ccm??

Rejea Nape, Polepole na sasa Shaka H.
Shaka
 
Duuh! Kwa ufafanuzi huu kumbe mwenezi ni kajitu fulani kasiko na kazi chamani. Sasa kwann huwa makatibu waenezi CCM hichomoza na kuonekana kama watu muhimu sana ndani ya ccm??

Rejea Nape, Polepole na sasa Shaka H.
Shaka
You've understanding myopia. Sidhani kama naweza kukuelewesha ukaelewa.
 
Kunawatu wanataka polepole atolewe ccm, Wala hakuna tatzo ila wajue kuwa wasije wakafanya makosa ambayo yanaweza kuja kuwaghalim baadae, maana nikiangalia sioni kabisa kosa lake, kabisa, ila membe alikuwa na makosa ya wazi wazi, ambayo hata asie kuwa na sim janja anajua kuwa membe alikuwa na shida...
 
Chawa wa Magufuli atapata tabu Sana kafurushwa jikoni,zama za kubeba fuko la hela kununua wapinzani na kununua wasanii wakajaze mikutano limepita.
Nje ya siasa hana ujanja wowote wa kuishi.
Arudi kwao akaokoote mabuyu aishi.Aamini nje ya siasa anaweza ishi,chama kimerudi nyumbani.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom