Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 29,348
- 40,220
Kumekuwa na tabia ambayo si nzuri kwenye mahusiano, unakuta kijana wa kiume ameoa, ana mke na watoto; Mbaya zaidi ndugu wa mwanaume wanakuwa wanaegemea upande wa mwanaume tu, watafanya naye mawasiliano vizuri ila kwa upande wa mke wa ndugu yao, hawafanyi mawasiliano iwe kwa kupiga simu au kwa kutuma ujumbe wa meseji.
Undugu wa aina hii tunaita undugu wa ki-unafiki, kama mwanaume atakuwa na kipato na hatakuwa makini anaweza kuishia kupigwa mizinga isiyoeleweka na ndugu zake....huku mkewe na watoto wakiwa wako katika hali isiyoeleweka.
Hii inamaana wewe baharia ukifa, mkeo na watoto wako wanakuwa hawana undugu tena na ndugu zako; au wanaishia kwenye manyanyaso ya mashangazi n.k
Kuwa makini na ndugu wanaofanya mawasiliano na wewe tu, bila wao kuwa na ukaribu au mawasiliano na mkeo na watoto wako; hao ni wanyonyaji.
Undugu wa aina hii tunaita undugu wa ki-unafiki, kama mwanaume atakuwa na kipato na hatakuwa makini anaweza kuishia kupigwa mizinga isiyoeleweka na ndugu zake....huku mkewe na watoto wakiwa wako katika hali isiyoeleweka.
Hii inamaana wewe baharia ukifa, mkeo na watoto wako wanakuwa hawana undugu tena na ndugu zako; au wanaishia kwenye manyanyaso ya mashangazi n.k
Kuwa makini na ndugu wanaofanya mawasiliano na wewe tu, bila wao kuwa na ukaribu au mawasiliano na mkeo na watoto wako; hao ni wanyonyaji.