Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Mheshimiwa Mwenyekiti wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika, maarufu kama AU, Bwana Jakaya Mrisho Kikwete, naomba utege sikio umsikilize Mchungaji.
Najua nimekuwa nikiongelea sana kuhusu mambo ya ndani ya nchi yetu na kukutaka usimame kidete kusafisha uozo ulioleta Ufisadi, Uzemba na Uhujumu. Naam nashukuru kwa taratibu umeeanza kazi.
Lakini safari hii Bwana Muungwana, Mchungaji anaongelea nafasi yako kama Mwenyekiti wa Umoja wa Nchi za Kiafrika.
Naomba utumie utashi wako kutatua matatizo ya Afrika bila kumuonea haya mtu!
Ulimtumia Membe kutoa tamko kuhusu Sudan, wakati jirani wa Kenya walipopata msukosuko wakati wa uchaguzi, sauti yako haikusikika. Ukasaidia Serikali ya Comoro iondokane na ugaidi.
Lakini kuna mambo ambayo yanahitaji sauti yako ya ukali na uongozi mahiri ukitumia uzoefu wako katika masuala ya mambo ya nje na kimataifa.
Nakuomba wakati unamalizia muda wako kama Mwenyekiti wa AU, utuletee ufumbuzi Zimbabwe ambako ukatili wa ndugu yetu wa awali wa mapambano, Robert Gabriel Mugabe unatishia si uhai wa Raia wasio na makosa pekee, bali ni hatari kwa usalama wetu kusini mwa Afrika.
Aidha inabidi uwakalishe chini kina Museveni na Kagame na waambie waache kumsaidia Jenerali Nkunda ambaye analeta vurugu Kongo.
Na mwisho, sauti yako inahitajika ma kwa kupeleka Jeshi lakulinda Amani au kuunda kamati ya usuluhishi ili kuleta Amani na kuwepo kwa Serikali katika Jamhuri ya Somalia.
Raila Odinga katoa kauli ambayo inaonyesha ujasiri kwa kutaka Mugabe awajibishwe, swali langu kwako je uko tayari kusimamia haki za binadamu na demokrasia Afrika kwa kumshurtisha Mugabe aachane na ubabe wake
Je uko tayai kuwakalisha chini zile koo pale Mogadishu ambazo sasa zinatambaa Bahari ya Hindi kuteka meli ili Somalia iwe na Serikali?
Je kule Afrika Magharibi anzia Nigeria, Sierra Leone na kwingine utulivu tunaounona ni wa kweli au ni mazugazuga?
Nakuomba basi uchukue hatua kubwa katika uenyekiti wako kuhakikisha unahamasisha uwajibikaji wa viongozi, kuimarika kwa Demokrasia na Kulinda haki za Binadamu ikiwa ni ziada ya cvita ya kutetea maslahi ya kiuchumi ya Afrika.
Ni hayo tuu Ndugu Mwenyekiti.
Najua nimekuwa nikiongelea sana kuhusu mambo ya ndani ya nchi yetu na kukutaka usimame kidete kusafisha uozo ulioleta Ufisadi, Uzemba na Uhujumu. Naam nashukuru kwa taratibu umeeanza kazi.
Lakini safari hii Bwana Muungwana, Mchungaji anaongelea nafasi yako kama Mwenyekiti wa Umoja wa Nchi za Kiafrika.
Naomba utumie utashi wako kutatua matatizo ya Afrika bila kumuonea haya mtu!
Ulimtumia Membe kutoa tamko kuhusu Sudan, wakati jirani wa Kenya walipopata msukosuko wakati wa uchaguzi, sauti yako haikusikika. Ukasaidia Serikali ya Comoro iondokane na ugaidi.
Lakini kuna mambo ambayo yanahitaji sauti yako ya ukali na uongozi mahiri ukitumia uzoefu wako katika masuala ya mambo ya nje na kimataifa.
Nakuomba wakati unamalizia muda wako kama Mwenyekiti wa AU, utuletee ufumbuzi Zimbabwe ambako ukatili wa ndugu yetu wa awali wa mapambano, Robert Gabriel Mugabe unatishia si uhai wa Raia wasio na makosa pekee, bali ni hatari kwa usalama wetu kusini mwa Afrika.
Aidha inabidi uwakalishe chini kina Museveni na Kagame na waambie waache kumsaidia Jenerali Nkunda ambaye analeta vurugu Kongo.
Na mwisho, sauti yako inahitajika ma kwa kupeleka Jeshi lakulinda Amani au kuunda kamati ya usuluhishi ili kuleta Amani na kuwepo kwa Serikali katika Jamhuri ya Somalia.
Raila Odinga katoa kauli ambayo inaonyesha ujasiri kwa kutaka Mugabe awajibishwe, swali langu kwako je uko tayari kusimamia haki za binadamu na demokrasia Afrika kwa kumshurtisha Mugabe aachane na ubabe wake
Je uko tayai kuwakalisha chini zile koo pale Mogadishu ambazo sasa zinatambaa Bahari ya Hindi kuteka meli ili Somalia iwe na Serikali?
Je kule Afrika Magharibi anzia Nigeria, Sierra Leone na kwingine utulivu tunaounona ni wa kweli au ni mazugazuga?
Nakuomba basi uchukue hatua kubwa katika uenyekiti wako kuhakikisha unahamasisha uwajibikaji wa viongozi, kuimarika kwa Demokrasia na Kulinda haki za Binadamu ikiwa ni ziada ya cvita ya kutetea maslahi ya kiuchumi ya Afrika.
Ni hayo tuu Ndugu Mwenyekiti.