Ni kama waliojaribu kuuwa legacy ya Nyerere huwa wanatapa upinzani mkali hadi leo wakati Nyerere alishafariki zaidi ya miaka 20 iliyopita.
Watu huwa wanarejea hotuba tu.
Naona watu ambao sikutegemea kamwe kwamba tungekuwa upande mmoja nao, sasa inajitokeza hivyo, au nasoma vibaya?

Basi ngoja nikueleze kwa uchache: Magufuli alifanya kosa (yapo mengi, lakini naandika kuhusu kosa hili 'specifically')
Kosa lake hili ndio udhaifu wake mkubwa wa uongozi.

Hakuweza kuwatambua wasaidizi wake waaminifu, ambao angewalea na kuwaachia maono yake wayaendeleze. Yeye alijiona yeye tu basi, na nguvu zake kwamba atafanikisha anayotaka yafanyike.

Badala ya kuwafundisha wasaidizi wake waaminifu wapate uzoefu na kulinda hayo maono, yeye kawekeza kwenye kuwanunua watu kama akina Ndugae, kwa njia mbalimbali, mradi wasimzuie kufanya alichotaka kufanya. Hilo ndilo kosa lake kubwa, na linamtambulisha kipekee kabisa, na mbali kabisa na Mwalimu Nyerere.

Magufuli hakuwa na muda, wala uwezo wa kuwaeleza wananchi wakaelewa. Kuondoka kwake, kaondoka na kila kitu. Wananchi hawakubaki na kitu!

Mkuu 'kijogoodi' ukitaka kunisoma na kunielewa, utanielewa vizuri tu.
 
Spika wa Bunge ameshauri mradi wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo uendelee kwa sababu Magufuli alishauriwa vibaya, hii ni baada ya kamati ya Bunge ya bajeti kushauri kuwa serikali iangalie kuhusu kuendelea na mradi huo...
Ukiona mtu mwenye macho anajifanya kipofu jua ameishaoshwa huyu. mbona hamkuyasema wakati wa Magufuli kama siyo unafiki na ufisadi jamani?
 
Mh SpikaNdugai yupo sahihi kabisa kuhusu ujenzi wa bandari ya Bagamoyo.Kwa kweli ameona mbali.Kwa sasa tupo kwenye ushindani mkubwa na jirani zetu hasa Kenya.Wenzetu wamejenga Bandari nyingine kubwa Lamu itakayoisaidia ya Mombasa.Wanaingiza mabilioni.Meli nyingi za mizigo za landlocked countries zinapitia pale.

Sie tunahangaika na SGR tena ya abiria na sio mizigo. Isitoshe Kenya wamejenga uwanjabwa ndege kilomita chache kutoka Mpakani Namanga.Hili Hayati Mzee Sitta alilikemea sana lakini hakusikilizwa.leo watalii wanatua pale,wanaambiwa mlima kilimanjaro wao,sisi tulibaki tukifukuzana na kuwalazimisha wawekezaji kulipa makodi ya kubambikwa,n.k wakakimbia na mapesa yao.Maduka ya kubadilishia pesa yakafungwa Hasa Dar na Arusha.

Mtalii anashangaa,eti mpaka aende benki.Harudi tena. Na mengine mengi.Ukazuka ugonjwa wa corona ndio kabisa wakenya wakapata sababu.yaliyofuata wote tunayajua.Dont visit Tanzania. Its Dangerous because they are claiming corona free.Mabilionea watalii ndio kabisa wakapotea.

Hili tangazo liliwahi kutolewa na baadhi ya vyombo vya habari vya Kenya kuua sekta yetu ya utalii.walifanikiwa kwa kiasi kikubwa.Tunaacha kujenga bandari ya Bagamoyo tunajenga uwanja wa ndege kijijini.Ripoti za CAG Assad zikashutumiwa na kuondolewa kwa uonevu.Huyu wa sasa abarikiwe sana.

Wenzetu wameingia ubia na mashirika makubwa ya ndege, sie tunajifanya tuna hela kumbe zinaliwa,hadi kufikia kukamatwa.Aibu kubwa. Nashauri tusimamishe ununuzi mpya wa ndege na kuziuza zingine ili pesa zitakazopatikana ziende kuboresha huduma za jamii kama vile Mahospitali, kuboresha mishahara, kuboresha mashule, vyuo n.k. TUBADILIKE AWAMU YA SITA.HONGERA MH.SPIKA UMEONA MBALI.
 
Magufuli kiukweli bila unafiki kaumiza watu wengi mno na hakua na vision nzuri ya uchumi
 
Mmeshlipwa hela mje mtetetee ujinga??

Bandari ya Bagamoyo idea ni nzuri
Lakini kukopa dollars bilioni 20 Kwa mchina Kwa ajili ya bandari ni upumbavu..

Masharti ya mchina ni pamoja na kuiendesha hiyo bandari Hadi pesa yake irudi

Magufuli alikuwa sahihi kusema mkataba ulikuwa wa kipumbavu kabisa...

Tujenge bandari bila kukopa nchi yeyote
 
Naunga mkono hoja ijengwe Ili kuchangamsha uchumi hasa hiyo train ya umeme na barabara ziwe busy kusafirisha mizigo.
 
Ngoja mkosee muingie 18 ya mchina
Mtamkumbuka jpm

Ova
Kuna watu wapumbafu sana! Hela ya mchina wa sasa ni ya kuogopa kama ukoma! Angalieni wenyewe Lusaka ilivyobadirishwa kuwa himaya ya china!
Kenya nao wako mbioni kujikuta wameuza sehemu ya nchi yao, angalieni zote mpaka mwisho mfyuuu👇



 
Ndicho nachosema, wamejaa kila mahali kuanzia chini mpaka juu...Hawa watu wakujipendekeza na kutengeneza CV za kwenda kupata viyoyozi badala ya kusaidia nchi na raia ili welfare ya kila moja ipande...
Uko sahihi Mkuu, wanasema kikulacho ki nguoni mwako.

Adui wa Mtanzania ni Mtanzania wenzetu
 
Mheshimiwa Speaker Ndugai anatutia kichevuchevu. He was for Bagamoyo Port before he wasn’t for and now he is for again! Watanzania, huu ni uongozi wa aina gani?

Hivi ni kweli Speaker wetu hajui kilichotokea kwa mataifa yaliyoingia kichwa kichwa kwa Wachina au ni kwa sababu ametumia office yetu ya umma kwa manufaa binafsi? Atuambie kama ziara yake ya China iliambatana na kuvuta mpunga au kupewa ahadi ambazo zinamnufaisha yeye binafsi.

Huu ni ujinga sasa!
 
Spika wa Bunge ameshauri mradi wa ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo uendelee kwa sababu Magufuli alishauriwa vibaya, hii ni baada ya kamati ya Bunge ya bajeti kushauri kuwa serikali iangalie kuhusu kuendelea na mradi huo.

Ndugai amesema kuwa mradi huo utakuwa na faida kubwa kwa Watanzania na tukichelewa hatutauta tena.

Magufuli alisema mradi huo ulikuwa ni hasara kwani ulikuwa na masharti magumu ikiwemo ya kuzuia bandari yoyote kuendelezwa, wala TRA kukusanya kodi na kupewa lease kwa miaka 99.




Pia soma:

1)
Spika Job Ndugai: Kutokana na masharti ya Mradi wa Bandari Bagamoyo, ni sahihi Serikali kuusitisha

2) Rais Magufuli ataja sababu kusitisha ujenzi bandari ya Bagamoyo kwa Mkopo wa Dola Bilioni 10

Mheshimiwa Speaker Ndugai anatutia kichevuchevu. He was for Bagamoyo Port before he wasn’t for and now he is for again! Watanzania, huu ni uongozi wa aina gani?

Hivi ni kweli Speaker wetu hajui kilichotokea kwa mataifa yaliyoingia kichwa kichwa kwa Wachina au ni kwa sababu ametumia office yetu ya umma kwa manufaa binafsi? Atuambie kama ziara yake ya China iliambatana na kuvuta mpunga au kupewa ahadi ambazo zinamnufaisha yeye binafsi.

Huu ni ujinga sasa!
Ngoja nikuongezee hasira mpaka tukawanyoe wenyewe hao wapumbafu wasiojua china ya sasa siyo ile iliyotujengea reli ys TAZARA👇


 
Mheshimiwa Speaker Ndugai anatutia kichevuchevu. He was for Bagamoyo Port before he wasn’t for and now he is for again! Watanzania, huu ni uongozi wa aina gani?

Hivi ni kweli Speaker wetu hajui kilichotokea kwa mataifa yaliyoingia kichwa kichwa kwa Wachina au ni kwa sababu ametumia office yetu ya umma kwa manufaa binafsi? Atuambie kama ziara yake ya China iliambatana na kuvuta mpunga au kupewa ahadi ambazo zinamnufaisha yeye binafsi.

Huu ni ujinga sasa!
Mheshimiwa Speaker Ndugai anatutia kichevuchevu. He was for Bagamoyo Port before he wasn’t for and now he is for again! Watanzania, huu ni uongozi wa aina gani?

Hivi ni kweli Speaker wetu hajui kilichotokea kwa mataifa yaliyoingia kichwa kichwa kwa Wachina au ni kwa sababu ametumia office yetu ya umma kwa manufaa binafsi? Atuambie kama ziara yake ya China iliambatana na kuvuta mpunga au kupewa ahadi ambazo zinamnufaisha yeye binafsi.

Huu ni ujinga sasa!
Ngoja nikuongezee hasira mpaka tukawanyoe wenyewe hao wapumbafu wasiojua china ya sasa siyo ile iliyotujengea reli ys TAZARA👇


 
Back
Top Bottom