Ndugai kumwita Masele akiwa katikati ya vikao vya PAP ni kuonyesha dharau kubwa kwa PAP na AU, na analalamika akiambiwa Bunge lake ni dhaifu?

Synthesizer

JF-Expert Member
Feb 15, 2010
11,143
18,774
Hivi Ndugai alikuwa na uharaka gani wa kumuita Masele nyumbani akijua alikuwa katikati ya kikao cha PAP, kama kweli hakuwa akitumika na Raisi wa PAP aliyetuhumiwa kwa makosa ya ngono?

Kwa kiongozi mwenye hekima na busara, vitu ambavyo naona ni adimu kwa Ndugai, hata kama Masele alikuwa na kosa, basi angesubiri kwanza amalize shughuli ya PAP, kwa kuwa Masele angerudi tu nyumbani. Hakukuwa na ulazima wa kufanya jambo hili kwa kutumia nguvu kubwa aliyotumia na kuiingiza Tanzania katika mmweko wenye kutia aibu kwamba tunafanya mambo ovyo ovyo. Mwenye kufanya mabo ovyo ovyo hapa ni wazi ni Ndugai, sio Masele.

Ndugai anakiri kwamba kumwita Masele hakuhusiani na PAP, sasa kwa nini unataka kuvuruga vikao vya PAP kwa jambo ambalo lilihitaji subira kidogo tu? Je ni Ndugai kujiona kuwa ana mamlaka makubwa kuliko PAP, au kuona kuwa Bunge na Tanzania ni muhimu kuliko PAP?

Huyu Ndugai ana matatizo sana ya kisaikolojia. Analalamika Bunge la Tanzania kudharilishwa kwa kuitwa dhaifu lakini yeye anafanya tendo la juu kabisa kuonyesha dharau kwa Bunge la Afrika. Na huyo huyo Ndugai alipiga mtu, mwanachama mwenzie wa CCM, fimbo ya kichwa kwa jambo dogo tu la kutoelewana. Ni huyo huyo Ndugai alitoa matamko kwamba CAG atakuja hata kwa pingu. Na yote haya yanadhihirisha jambo moja ambalo inabidi uwe na akili ya mwenda wazimu kutoliona - Ndugai ana dharau, hana busara wala hekima, na hafai katika uongozi wa nafasi nyeti kama Uspika.

AU inapaswa kuilalamikia rasmi Tanzania kwa tabia ya kuonyesha dharau kwa kikao halali cha PAP.
 
nani ana habari na matokeo ya kikao cha nidhamu dhidi ya Masele, na pia ukaguzi wa ofisi ya CAG? Huyu Ndugai hajaumbuka tu?

Alishaumbuka alipomuita CAG kwa vitusho na dharau; aneumbuka zaidi alivyofanya hivyo kwa Masele pia. Kwa sababu hajui kijifunza na kuona aibu iko siku atajiaibisha zaidi!
 
Sijawahi kuona spika anayeita wabunge na viongozi kwa vitisho vya pingu na polisi, huyu ndiyo spika wa kwanza kumuona
NImesema humu ndani, kwamba Ndugai anatakiwa kufikishwa kwenye kamati hiyo ya nidhamu kwa makosa yafuatayo;
  1. Kuonyesha dharau kwa Bunge la Afrika (PAP), kikao halali cha African Union (AU)
  2. Kutumia lugha ya kashfa, yenye kuhukumu na kudhalilisha kwa viongozi wa kitaifa (CAG - kufikishwa kwa pingu; Masele - kufanya mambo ya ovyo ovyo)
  3. Kudharau (undermine) ofisi ya raisi wa Tanzania (kuvunja mkataba wa Bandari Bagamoyo ni sawa na kuweka mkokoteni usukume punda, afadhali tungeacha SGR)
  4. Nk
 
Alishaumbuka alipomuita CAG kwa vitusho na dharau; aneumbuka zaidi alivyofanya hivyo kwa Masele pia. Kwa sababu hajui kijifunza na kuona aibu iko siku atajiaibisha zaidi!
Labda wenye tatizo ni sisi Watanzania (au Katiba?) kwamba tunavumilia kuwa na watu ambao wanatenda watakavyo katika ofisi za umma lakini hakuna tunalofanya. Katiba inakiukwa kimakusudi tunakubali. Tunapigwa na polisi bila kosa, hata tukiwa vilema, tunakubali. Kuna siku tupapewa taahira kuwa raisi wetu tutakubali tu.

NI lini tunaweza kwa mfano, Dar es Salaam nzima kwenda kukaa mbele ya Ikulu na kusema hatutoki hadi Ndugai kaondolewa!

Angalia Sudan. Wanakaa kuzingira makao makuu ya jeshi na wanasema hawaondoki hadi kieleweke!
 
Yale yale, ukistaajabu ya CAG ,utayaona ya Masele. Tunashusha hadhi ya bunge kwa petty issues.
 
Yale yale, ukistaajabu ya CAG ,utayaona ya Masele. Tunashusha hadhi ya bunge kwa petty issues.
Mkuu hivi hiyo avatar yako ni picha ya nini, nachukua muda mwingi kuichunguza kuliko kusoma posts:p Mtu yuko shimoni ataokolewa na ndege? Maana yake nini?

1105430
 
Back
Top Bottom