Ndugai hakutakiwa kuomba msamaha; Sasa kajitia kitanzi mwenyewe

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,339
51,864
Kwema wakuu!

Katika duru za kisiasa, kinachoendelea ni sakata la Mhe. Spika na Mkuu wa nchi, Mhe. Rais Samia.
Nimesikiliza pande zote mbili nikaona nami nitoe maoni yangu.

Kama mimi ndio ningekuwa Spika nisingeomba Msamaha, ningeweza kufafanua kauli zangu kwa namna ya kutetea kile nilichokuwa nakiamini.

Kitendo alichokifanya Ndugai ni kujisaliti yeye mwenyewe, kushindwa kutetea kile alichokiamini. Na hapa ndipo alipozidiwa na Ndugu Humphrey Polepole.

Sikuona sababu ya Spika kuomba msamaha wakati aliyoyasema yalikuwa ni dhahiri, kuhusu kukopa kaongea vizuri kabisa kuwa tusiwe taifa la kukopa kopa ingawaje hajakataza kukopa. Ndugai kwa upande wake kajaribu kutoa maoni yake kuwa yeye aliona bora kuminyana sisi kwa sisi kwa kutozana kodi kuliko kukopa kopa, huo ni mtazamo wake na ambao nafahamu wapo wengi watakaoungana na yeye kimtazamo na wapo watakaompinga vilevile.

Kitendo cha mtu kuomba msamaha kwa jambo alilolitenda kwa makusudi na ndicho anachokiamini ni kutia kitanzi mwenyewe na kutoa kibali cha upande wa pili kumshambulia atakavyo.

Kuomba msamaha sio ishara ya kukubaliwa isipokuwa kutangaza umeshindwa.

Kuomba msamaha kuna mata zaidi kama Mkubwa akimuomba mdogo msamaha lakini sio mdogo akimuomba mkubwa msamaha.

Mdogo akimuomba mkubwa msamaha huwa na mambo mawili, mosi; Unafiki kutokana na hofu kwa kuwa hana ubavu wa kupambana na mkubwa wake, mbili toba ya kweli ambayo hii wengi ni 10% lakini 90% ni unafiki

Lazima tujifunze kuwa Mtu mzima unapokosea kwa makusudi hata uombe msamaha haitabadilisha lolote upande wa pili, yaani tayari ushaondoa Uaminifu na kamwe huwezi kuurejesha.

Ndugai hakupaswa kuomba msamaha, angetulia na kuendelea na mambo mengine hii ingewapa kazi upande wa pili, lakini kujisalimisha ni kurahisisha kupigwa.

Ndugai pia kapoteza bara na pwani, wale waliokuwa wanamuunga mkono kwa mtazamo wake sasa wanamuona mnafiki, na wale aliowaponda wanakopa kopa pia wanamuona mnafiki hata angeomba msamaha kwa machozi ya damu.

Bora Polepole kabakiza uaminifu kwa wafuasi wake, wanamuona shujaa, na wanaweza kumsikiliza. Lakini sasa hivi nani atamsikiliza tena Ndugai, maana hata yeye mwenyewe hawezi kujisikiliza,

Hii inatupa fundisho sisi wengine wachanga namna ya kufanya maamuzi.
Kama utashindwa basi kwa nini uingie kwenye vita ambayo ulijua tangu mwanzo utashindwa na kudhalilika?

Wito; Kama Ndugai aliongea hayo akiwa na agenda ya siri kama ilivyotanabaishwa na Mhe. Rais basi awajibike au kuwajibishwa, lakini kama ni maoni yake binafsi na hakuna nguvu kutoka nje basi msamaha wake upokelewe.

Hata hivyo nafasi ya Urais sio ya mtu mmoja, hivyo yeyote anayetaka kuwania asionekane ni adui wa nchi.

Tuache demokrasia ichukue mkondo wake. Kutaka Urais 2025 sio dhambi wala sio kosa la jinai. Labda wanaotaka wawe wanahujumu utendaji kazi wa Serikali iliyopo madarakani lakini kama ni kuikosoa kwenye mapungufu yake ili ionekane haina sifa ya kuendelea 2025 hilo sio kosa kimsingi.

Tujenge nchi
 
Ndugai kwa upande wake kajaribu kutoa maoni yake kuwa yeye aliona bora kuminyana sisi kwa sisi kwa kutozana kodi kuliko kukopa kopa,
kama angelikuwa na nia njema
Si angelipendekeza wabunge basi wapunguziwe mishahara minono na kukata maposho ili kuisaidia Seriali kupata pesa za ziada!
naona huko kubanana kwenyewe kunatuhusu zaidi sisi walala hoi tuu ambao wengi wetu mapato yetu ni duni sana vijisenti vichavhe tunavyotumiana kwenye mitandao ni ili kupunguziana makali ya maisha. SasaTozo ni janga kwa wanyonge.

Ndungai anatukejeli sisi Wanyonge na kutaka tubanwe zaidi.
Suala la kukopa linasababishwa na ongezeko la mahitaji ya Huduma za nchi kwa raia na wakati Mapato ni duni ,hayaendani na ukuaji wa mahitaji yetu kama Taifa. Hapo ndio kuoneha kuwa Serikali Ya ccm imeendelea Kushindwa kuleta uwiano wa Mapato na Matumizi.
Ndungai ni wale wale ,Walo shindwa Kuongoza Taifa Kufika kwenye Neema bila ya Madeni.
Mbona TZ ilishauzwa zamani? Mumesahau Enzi za Mkapa?
 
kama angelikuwa na nia njema
Si angelipendekeza wabunge basi wapunguziwe mishahara minono na kukata maposho ili kuisaidia Seriali kupata pesa za ziada!
naona huko kubanana kwenyewe kunatuhusu zaidi sisi walala hoi tuu ambao wengi wetu mapato yetu ni duni sana vijisenti vichavhe tunavyotumiana kwenye mitandao ni ili kupunguziana makali ya maisha. SasaTozo ni janga kwa wanyonge.

Ndungai anatukejeli sisi Wanyonge na kutaka tubanwe zaidi.
Suala la kukopa linasababishwa na ongezeko la mahitaji ya Huduma za nchi kwa raia na wakati Mapato ni duni ,hayaendani na ukuaji wa mahitaji yetu kama Taifa. Hapo ndio kuoneha kuwa Serikali Ya ccm imeendelea Kushindwa kuleta uwiano wa Mapato na Matumizi.
Ndungai ni wale wale ,Walo shindwa Kuongoza Taifa Kufika kwenye Neema bila ya Madeni.
Mbona TZ ilishauzwa zamani? Mumesahau Enzi za Mkapa?


Nakuelewa Mkuu.

Ila nazungumzia scenario ya Ndugai kuomba Msamaha ambao kimsingi ukitazama hautamsaidia Kwa lolote ni Bora angebaki Kama POLEPOLE asubiri matokeo.

Ndugui inaonekana alikuwa jasiri kuanzisha Jambo ambalo anaogopa matokeo yake. Hili ni kosa
 
Mkuu we hukuwepo kwenye kile kikao kwa ufupi ndugai aliponda mkopo wa 1.3 bila chenga tena mkopo ilikuwa zuga tu hisia zake unaona kabisa anamdisi maza spana alizopewa ni haki yake kabisa.
 
Mkuu we hukuwepo kwenye kile kikao kwa ufupi ndugai aliponda mkopo wa 1.3 bila chenga tena mkopo ilikuwa zuga tu hisia zake unaona kabisa anamdisi maza spana alizopewa ni haki yake kabisa.


Mimi sinatatizo na malumbano Yao ya Madaraka.
Tatizo langu ni udhaifu aliouonyeshe spika hata Pambano halijanoga.

Yaani Kama tungekuwa tumelipia angepaswa kurudisha pesa za kiiingilio tulizotoa.

Hoja yangu asingepaswa kuomba Msamaha Kama ilivyo Kwa kina Polepole na Gwajima.
 
Mimi sinatatizo na malumbano Yao ya Madaraka.
Tatizo langu ni udhaifu aliouonyeshe spika hata Pambano halijanoga.

Yaani Kama tungekuwa tumelipia angepaswa kurudisha pesa za kiiingilio tulizotoa.

Hoja yangu asingepaswa kuomba Msamaha Kama ilivyo Kwa kina Polepole na Gwajima.
Mkuu huyo bwege hakuomba msamaha kwa hiari yake,kilichotokea kwa huyo siri anayo mwenyewe waliamua kumvua nguo,alikuwa anajaribu kingiza kidole kwenye mdomo wa chura kujua kama ana meno.
 
Kuna ishu za msingi mnasahaulishwa.
Shtukeni.
Samia na ndugai wakirumbana Wana hasara gani?
Nani ANAMKUMBUKA MBOWE MAHABUSU?
Sio Kweli.

Unajua Ndugai na Samia ni watu wazima?

Sio rahisi kucheza michezo ya kudhalilishana au kujidhalilisha.
Hii ishu ipo Sirius
 
namna hii
1641386740806.png
 
Bado kuna gap linaloweza kutumika na yeyote mbele ya safari, huyo mwenye kete sasa hivi nae akili ndogo kuicheza hii michezo hajui, labda aombe Mungu kila atakaemtingisha aishie kumuomba msamaha, siasa ni kama upepo unabadilika uelekeo kila dakika.

Huyu kiongozi tuliyenaye hana hekima, huwezi mtu mstaarabu kuombwa msamaha (japo hakuna kosa alilotendwa) aishie kumuitia mwenzake kikundi cha mipasho toka mikoani wakamsute ikulu, hizi ni tabia za kisichana ambazo hazifai kuendelea kukaa pale ikulu.
 
Kuna ishu za msingi mnasahaulishwa.
Shtukeni.
Samia na ndugai wakirumbana Wana hasara gani?
Nani ANAMKUMBUKA MBOWE MAHABUSU?

Sio kweli, mbowe kwa sasa ndio hivyo tena hapo tegemeo kubwa ni Rais, wala hakuna haja ya michezo ya namna unayofikiria wewe.

Ungenambia ishu ya polepole ningekubali lakini kwa Spika Vs Rais haiwezi kuwa mchezo
 
Bado kuna gap linaloweza kutumika na yeyote mbele ya safari, huyo mwenye kete sasa hivi nae akili ndogo kuicheza hii michezo hajui, labda aombe Mungu kila atakaemtingisha aishie kumuomba msamaha, siasa ni kama upepo unabadilika uelekeo kila dakika.


Ni kweli,

Mama angepaswa ajibu hoja hizi wiki mbili au tatu kama sio mwezi baadae, au asiliongelee kabisa
 
Kwema wakuu!

Katika duru za kisiasa, kinachoendelea ni sakata la Mhe. Spika na Mkuu wa nchi, Mhe. Rais Samia.
Nimesikiliza pande zote mbili nikaona nami nitoe maoni yangu.

Kama mimi ndio ningekuwa Spika nisingeomba Msamaha, ningeweza kufafanua kauli zangu kwa namna ya kutetea kile nilichokuwa nakiamini.

Kitendo alichokifanya Ndugai ni kujisaliti yeye mwenyewe, kushindwa kutetea kile alichokiamini. Na hapa ndipo alipozidiwa na Ndugu Humphrey Polepole.
Sikuona sababu ya Spika kuomba msamaha wakati aliyoyasema yalikuwa ni dhahiri, kuhusu kukopa kaongea vizuri kabisa kuwa tusiwe taifa la kukopa kopa ingawaje hajakataza kukopa. Ndugai kwa upande wake kajaribu kutoa maoni yake kuwa yeye aliona bora kuminyana sisi kwa sisi kwa kutozana kodi kuliko kukopa kopa, huo ni mtazamo wake na ambao nafahamu wapo wengi watakaoungana na yeye kimtazamo na wapo watakaompinga vilevile.

Kitendo cha mtu kuomba msamaha kwa jambo alilolitenda kwa makusudi na ndicho anachokiamini ni kutia kitanzi mwenyewe na kutoa kibali cha upande wa pili kumshambulia atakavyo.
Kuomba msamaha sio ishara ya kukubaliwa isipokuwa kutangaza umeshindwa.
Kuomba msamaha kuna mata zaidi kama Mkubwa akimuomba mdogo msamaha lakini sio mdogo akimuomba mkubwa msamaha.
Mdogo akimuomba mkubwa msamaha huwa na mambo mawili, mosi; Unafiki kutokana na hofu kwa kuwa hana ubavu wa kupambana na mkubwa wake, mbili toba ya kweli ambayo hii wengi ni 10% lakini 90% ni unafiki

Lazima tujifunze kuwa Mtu mzima unapokosea kwa makusudi hata uombe msamaha haitabadilisha lolote upande wa pili, yaani tayari ushaondoa Uaminifu na kamwe huwezi kuurejesha.

Ndugai hakupaswa kuomba msamaha, angetulia na kuendelea na mambo mengine hii ingewapa kazi upande wa pili, lakini kujisalimisha ni kurahisisha kupigwa.

Ndugai pia kapoteza bara na pwani, wale waliokuwa wanamuunga mkono kwa mtazamo wake sasa wanamuona mnafiki, na wale aliowaponda wanakopa kopa pia wanamuona mnafiki hata angeomba msamaha kwa machozi ya damu.

Bora Polepole kabakiza uaminifu kwa wafuasi wake, wanamuona shujaa, na wanaweza kumsikiliza. Lakini sasa hivi nani atamsikiliza tena Ndugai, maana hata yeye mwenyewe hawezi kujisikiliza,

Hii inatupa fundisho sisi wengine wachanga namna ya kufanya maamuzi.
Kama utashindwa basi kwa nini uingie kwenye vita ambayo ulijua tangu mwanzo utashindwa na kudhalilika?

Wito; Kama Ndugai aliongea hayo akiwa na agenda ya siri kama ilivyotanabaishwa na Mhe. Rais basi awajibike au kuwajibishwa, lakini kama ni maoni yake binafsi na hakuna nguvu kutoka nje basi msamaha wake upokelewe.
Hata hivyo nafasi ya Urais sio ya mtu mmoja, hivyo yeyote anayetaka kuwania asionekane ni adui wa nchi. Tuache demokrasia ichukue mkondo wake. Kutaka Urais 2025 sio dhambi wala sio kosa la jinai. Labda wanaotaka wawe wanahujumu utendaji kazi wa serikali iliyopo madarakani lakini kama ni kuikosoa kwenye mapungufu yake ili ionekane haina sifa ya kuendelea 2025 hilo sio kosa kimsingi.

Tujenge nchi
 
Ushauri wako kwake (Ndugai) ni mzuri sana. Principally, hivyo ndivyo ilivyo, kwamba, mtu lazima asimame na kukutetea daima kile anachokiamini bila kujali matokeo yake...

Yesu Kristo Bwana na Mwokozi wa ulimwengu alisimamia kweli aliyoamini hata kama iligharimu UHAI wake...

LAKINI MIMI NAONGEZEA HAYA KWA AJILI YA WATU WA AINA YA CCM WENYE MAMLAKA NA MADARAKA YA KISERIKALI:

Kwamba, kwa mujibu wa mfumo wa utawala wetu "Rais" ni kila kitu. Obviously, Ndugai alipigwa upofu na ujinga wa kifikra hata akajikuta haoni nguvu ya mhimili wa "EXECUTIVE/U-RAIS" dhidi yake kiasi cha kuropoka na mdomo wake unamponza sasa...

Kina Ndugai hawa wana nafasi ya kutumia fursa hii waliyonayo kwa sasa kuleta usawazisho wa mfumo wetu wa utawala kwa kuhakikisha tuna katiba inayolinda na kuweka UHURU WA KWELI wa mihimili ya utawala (Bunge, Mahakama na Serikali/Executive)

Tungekuwa na uhuru wala kusingekuwa na mjadala wa maoni tu ya mtu tena ktk nafasi ya U - SPIKA aliyoyatoa kuhusu utendaji wa serikali...

Kwa kuwa hata Bunge/Spika hayuko huru, yupo pale kwa hisani ya Executive (Rais), alikuwa MJINGA SANA kupanua mdomo wake kukosoa mkono unaokupa kula...!!

Hii kazi alitakiwa awaachie kina Tundu Lissu, Freeman Mbowe na wengine kina sisi huku...

LABDA sasa akili zao hawa kina Ndugai zitaanza kuona na kuelewa kwanini watu wanataka KATIBA MPYA YA WANANCHI....
 
Kuna ishu za msingi mnasahaulishwa.
Shtukeni.
Samia na ndugai wakirumbana Wana hasara gani?
Nani ANAMKUMBUKA MBOWE MAHABUSU?
Sasa kesi si mpaka isikilizwe tena? Utakaa unacheza muziki hata kama kinachosikika lunigani ni taarifa ya habari?!!!
 
swali mnamkumbuka au ndo mnacheza kila ngoma wanayopiga CCM?
Kuna haja gani upinzani kuingilia ugomvi wa Samia na ndugai?
mtadai lini haki zenu?
Sasa kesi si mpaka isikilizwe tena? Utakaa unacheza muziki hata kama kinachosikika lunigani ni taarifa ya habari?!!!
 
Back
Top Bottom