Mnyakatari
JF-Expert Member
- Oct 25, 2010
- 2,027
- 1,791
Akitolea ufafanuzi hoja ya Mwigulu Nchemba bungeni leo asubuhi naibu spika amesema kuwa tangu bunge hili la kumi lianze halijawahi kupokea ushahidi wowote kutoka kwa wabunge wanaotakiwa kufanya hivyo na kiti! Ilikuwa ni baada ya Mwigulu kuomba mwongozo kuhusu maneno ya Mnyika kuwa alihusika kwenye wizi wa EPA.
Concern yangu kubwa hapa ni alichokisema Ndugai kuwa wabunge hasa wa upinzani wajiangalie na matamshi yao ndani ya bunge na wawe wapole wanapotakiwa kufuta kauli zao kuliko kujifanya wana ushahidi ukizingatia kuwa hakuna ushahidi uliowahi kuwasilishwa kwenye bunge hili.
Sote tunakumbuka matukio kama hayo bungeni na idadi ya wabunge waliowahi kuambiwa walete ushahidi kuthibitisha wayasemayo.Zitto Kabwe,Godbless Lema ni mfano wa wabunge ambao wamewahi kutakiwa ushahidi kwenya bunge hili na wao wenyewe kusema baadaye kuwa wameshawasilisha.
Pia kwenye sakata la Godbless Lema,Spika Makinda ameshawahi kulithibitishia bunge kuwa ameupokea.Hiyo ilikuwa ni baada ya kuombwa mwongozo na Zitto(kama sikosei) kuwa ushahidi wa Lema usomwe bungeni kama umeshawasilishwa mezani kwake naye akajibu kuwa amepokea huo ushahidi na wanaendelea kuufanyia kazi.
Hata kwa upande wa Zitto,Makinda aliwahi kuthibitisha kupokea ushahidi wake na baadaye Zitto mwenyewe kuthibitisha.
Ndugai pia aliendelea kudai kuwa wabunge waache kudanganya kwenye mitandao kuwa wamewasilisha ushahidi huku wakijua kuwa hawajafanya hivyo.
Hata hili la Mnyika Ndugai amesema kilichowasilishwa ni utangulizi tu na wala sio ushahidi wa alichokizungumza kinyume na inavyosemwa kwenye mitandao na magazeti!
Hili linaleta picha gani?kwamba wabunge wetu wanadanganya? Spika Makinda alidanganya? Wabunge wetu kwa kushirikiana na Makinda wametudanganya na Ndugai ameamua kuwatolea uvivu?Kwamba Kinachowasilishwa huwa hakikidhi kuitwa Ushahidi wa tuhuma husika?
Tujadili.
Concern yangu kubwa hapa ni alichokisema Ndugai kuwa wabunge hasa wa upinzani wajiangalie na matamshi yao ndani ya bunge na wawe wapole wanapotakiwa kufuta kauli zao kuliko kujifanya wana ushahidi ukizingatia kuwa hakuna ushahidi uliowahi kuwasilishwa kwenye bunge hili.
Sote tunakumbuka matukio kama hayo bungeni na idadi ya wabunge waliowahi kuambiwa walete ushahidi kuthibitisha wayasemayo.Zitto Kabwe,Godbless Lema ni mfano wa wabunge ambao wamewahi kutakiwa ushahidi kwenya bunge hili na wao wenyewe kusema baadaye kuwa wameshawasilisha.
Pia kwenye sakata la Godbless Lema,Spika Makinda ameshawahi kulithibitishia bunge kuwa ameupokea.Hiyo ilikuwa ni baada ya kuombwa mwongozo na Zitto(kama sikosei) kuwa ushahidi wa Lema usomwe bungeni kama umeshawasilishwa mezani kwake naye akajibu kuwa amepokea huo ushahidi na wanaendelea kuufanyia kazi.
Hata kwa upande wa Zitto,Makinda aliwahi kuthibitisha kupokea ushahidi wake na baadaye Zitto mwenyewe kuthibitisha.
Ndugai pia aliendelea kudai kuwa wabunge waache kudanganya kwenye mitandao kuwa wamewasilisha ushahidi huku wakijua kuwa hawajafanya hivyo.
Hata hili la Mnyika Ndugai amesema kilichowasilishwa ni utangulizi tu na wala sio ushahidi wa alichokizungumza kinyume na inavyosemwa kwenye mitandao na magazeti!
Hili linaleta picha gani?kwamba wabunge wetu wanadanganya? Spika Makinda alidanganya? Wabunge wetu kwa kushirikiana na Makinda wametudanganya na Ndugai ameamua kuwatolea uvivu?Kwamba Kinachowasilishwa huwa hakikidhi kuitwa Ushahidi wa tuhuma husika?
Tujadili.