Ndugai: Hakuna Ushahidi uliowahi kuwasilishwa kwenye bunge hili!

Mnyakatari

JF-Expert Member
Oct 25, 2010
2,027
1,791
Akitolea ufafanuzi hoja ya Mwigulu Nchemba bungeni leo asubuhi naibu spika amesema kuwa tangu bunge hili la kumi lianze halijawahi kupokea ushahidi wowote kutoka kwa wabunge wanaotakiwa kufanya hivyo na kiti! Ilikuwa ni baada ya Mwigulu kuomba mwongozo kuhusu maneno ya Mnyika kuwa alihusika kwenye wizi wa EPA.

Concern yangu kubwa hapa ni alichokisema Ndugai kuwa wabunge hasa wa upinzani wajiangalie na matamshi yao ndani ya bunge na wawe wapole wanapotakiwa kufuta kauli zao kuliko kujifanya wana ushahidi ukizingatia kuwa hakuna ushahidi uliowahi kuwasilishwa kwenye bunge hili.

Sote tunakumbuka matukio kama hayo bungeni na idadi ya wabunge waliowahi kuambiwa walete ushahidi kuthibitisha wayasemayo.Zitto Kabwe,Godbless Lema ni mfano wa wabunge ambao wamewahi kutakiwa ushahidi kwenya bunge hili na wao wenyewe kusema baadaye kuwa wameshawasilisha.

Pia kwenye sakata la Godbless Lema,Spika Makinda ameshawahi kulithibitishia bunge kuwa ameupokea.Hiyo ilikuwa ni baada ya kuombwa mwongozo na Zitto(kama sikosei) kuwa ushahidi wa Lema usomwe bungeni kama umeshawasilishwa mezani kwake naye akajibu kuwa amepokea huo ushahidi na wanaendelea kuufanyia kazi.

Hata kwa upande wa Zitto,Makinda aliwahi kuthibitisha kupokea ushahidi wake na baadaye Zitto mwenyewe kuthibitisha.
Ndugai pia aliendelea kudai kuwa wabunge waache kudanganya kwenye mitandao kuwa wamewasilisha ushahidi huku wakijua kuwa hawajafanya hivyo.

Hata hili la Mnyika Ndugai amesema kilichowasilishwa ni utangulizi tu na wala sio ushahidi wa alichokizungumza kinyume na inavyosemwa kwenye mitandao na magazeti!

Hili linaleta picha gani?kwamba wabunge wetu wanadanganya? Spika Makinda alidanganya? Wabunge wetu kwa kushirikiana na Makinda wametudanganya na Ndugai ameamua kuwatolea uvivu?Kwamba Kinachowasilishwa huwa hakikidhi kuitwa Ushahidi wa tuhuma husika?

Tujadili.
 
Inaonekana Ndugai kafuzu kozi ya kuitetea Serikali,fuatilia miongozo na ushauri wake always anasihi kutoipinga serikali as is ni naibu waziri fulani
 
Inaonekana Ndugai kafuzu kozi ya kuitetea Serikali,fuatilia miongozo na ushauri wake always anasihi kutoipinga serikali as is ni naibu waziri fulani

Inashangaza sana mkuu,Unafikiri ni kwa nini aliongea vile kuhusu ushahidi unaowasilishwa na wabunge?
 
Ndugai amevunja kanuni zifuatazo leo;

Naomba kunukuu kanunizifuatazo ;
1. Kanuniya 5 (1) ambayo inasema kuwa "katikakutekeleza majukumu yake yaliyotajwa katika ibara ya ya 84 ya Katiba , Spikaataongozwa na kanuni hizi ………."

2. Kanuniya 63 (2) " Mbunge yeyote anapokuwa akisema Bungeni hatachukuliwa kuwa anasema uongo iwapo anafanya rejea ya habari kuhusu jambo Fulani lililotangazwa aulililoandikwa na vyombo vya habari"

3. Kanuniya Adhabu : hii ni kanuni ya 73 (3) "Endapo mbunge yeyote atatakiwa kuthibitisha ukweli wa jambo au suala alilolisema Bungeni na hadi kufikia mwisho wa muda aliopewa amekataa au ameshindwa kutoa uthibitisho huo, Spika anaweza kumsimamisha Mbunge huyo kuhudhuria vikao vya Bunge visivyozidi vitano"

4. Kanuniya kupelekwa kamati ya haki, maadili na madaraka ya bunge ni 74(1) "Spika anaweza kutaja jina la Mbunge kwamba amedharau mamlaka ya Spika na kisha kupeleka jina hilo kwenye kamati ya Haki, Maadili na Madaraka ya Bunge….."
 
Ndugai amevunja kanuni zifuatazo leo;

Naomba kunukuu kanunizifuatazo ;
1. Kanuniya 5 (1) ambayo inasema kuwa "katikakutekeleza majukumu yake yaliyotajwa katika ibara ya ya 84 ya Katiba , Spikaataongozwa na kanuni hizi ………."
2. Kanuniya 63 (2) " Mbunge yeyote anapokuwa akisema Bungeni hatachukuliwa kuwa anasemauongo iwapo anafanya rejea ya habari kuhusu jambo Fulani lililotangazwa aulililoandikwa na vyombo vya habari"
3. Kanuniya Adhabu : hii ni kanuni ya 73 (3) "Endapo mbunge yeyote atatakiwakuthibitisha ukweli wa jambo au suala alilolisema Bungeni na hadi kufikiamwisho wa muda aliopewa amekataa au ameshindwa kutoa uthibitisho huo,Spikaanaweza kumsimamisha Mbunge huyo kuhudhuria vikao vya Bunge visivyozidi vitano"
4. Kanuniya kupelekwa kamati ya haki, maadili na madaraka ya bunge ni 74(1) "Spikaanaweza kutaja jina la Mbunge kwamba amedharau mamlaka ya Spika na kasha kupelekajina hilo kwenye kamati ya Haki,Maadili na Madaraka ya Bunge….."

Hapa tunaona kuwa suala la Mnyika limepelekwa kamati ya haki,maadili na madaraka ya bunge kimakosa!Hakuna mahali ambapo mamlaka ya spika imedharauliwa na Mnyika kama inavyotaka kanini ya 74(1)
 
Tatizo Ndugai ana jazba sana alikuwa na haja gani kuanza kuongea yale yote na je mbona wanapopewa ushahidi wenye mashiko wanaishiakukaa kimya? Spika na wasaidizi wake wamegeuka kuwa sehemu ya serikali. Kuna haja kupitisha kifungu kwenye katibu mpya spika na wasaidizi wake kutokuwa wabunge wawe watu huru
 
Huyu naibu spika lengo lake ni kuwatisha wabunge wa upinzani,hasa wa CDM, lakini anachosahau ni kuwa hawa jammaa hawatishiwi nyau, na wataendelea kuleta tuhuma zenye ushahidi mzito, ambapo kama kawaida ya kiti cha spika, kwa kuwa lengo lao ni kukingia kifua chama chao cha mabwepande, ushahidi wowote wenye nguvu, kama ule wa Lema vs Liwalo na liwe na Zitto vs Mkulo, ushahidi wa aina hiyo utaozea kwenye cabinet za Bunge, tusitarajie kuwa itatokea siku watathubutu kuutoa hadharani!!
 
Kwa siku za karibuni tokea Mnyika abainishe JK dhaifu naona Ndugai kachange na kuonyesha chuki zake wazi kabisa,,pamoja na mengine yote,,maneno aliyomtolea Mdee leo yanadhihirisha hili
 
akitolea ufafanuzi hoja ya mwigulu nchemba bungeni leo asubuhi naibu spika amesema kuwa tangu bunge hili la kumi lianze halijawahi kupokea ushahidi wowote kutoka kwa wabunge wanaotakiwa kufanya hivyo na kiti! Ilikuwa ni baada ya mwigulu kuomba mwongozo kuhusu maneno ya mnyika kuwa alihusika kwenye wizi wa epa.

Concern yangu kubwa hapa ni alichokisema ndugai kuwa wabunge hasa wa upinzani wajiangalie na matamshi yao ndani ya bunge na wawe wapole wanapotakiwa kufuta kauli zao kuliko kujifanya wana ushahidi ukizingatia kuwa hakuna ushahidi uliowahi kuwasilishwa kwenye bunge hili.

Sote tunakumbuka matukio kama hayo bungeni na idadi ya wabunge waliowahi kuambiwa walete ushahidi kuthibitisha wayasemayo.zitto kabwe,godbless lema ni mfano wa wabunge ambao wamewahi kutakiwa ushahidi kwenya bunge hili na wao wenyewe kusema baadaye kuwa wameshawasilisha.

Pia kwenye sakata la godbless lema,spika makinda ameshawahi kulithibitishia bunge kuwa ameupokea.hiyo ilikuwa ni baada ya kuombwa mwongozo na zitto(kama sikosei) kuwa ushahidi wa lema usomwe bungeni kama umeshawasilishwa mezani kwake naye akajibu kuwa amepokea huo ushahidi na wanaendelea kuufanyia kazi.

Hata kwa upande wa zitto,makinda aliwahi kuthibitisha kupokea ushahidi wake na baadaye zitto mwenyewe kuthibitisha.
Ndugai pia aliendelea kudai kuwa wabunge waache kudanganya kwenye mitandao kuwa wamewasilisha ushahidi huku wakijua kuwa hawajafanya hivyo.

Hata hili la mnyika ndugai amesema kilichowasilishwa ni utangulizi tu na wala sio ushahidi wa alichokizungumza kinyume na inavyosemwa kwenye mitandao na magazeti!

Hili linaleta picha gani?kwamba wabunge wetu wanadanganya? Spika makinda alidanganya? Wabunge wetu kwa kushirikiana na makinda wametudanganya na ndugai ameamua kuwatolea uvivu?kwamba kinachowasilishwa huwa hakikidhi kuitwa ushahidi wa tuhuma husika?

Tujadili.
kuna uwezekano mkubwa ndugai akwa anadanganya kutokana na tabia yake ya kuilinda serikali badala ya kusimamia kanuni za bunge. Yeye na mabumba oooooooovyo kweli!
 
Ndugai naona ni naibu spika mfu kiakili mara anapoongoza Bunge lina mshinda na kinachotokea anapata hasira kutokana na uelewa wake kuwa mdogo kwenye nyaja ya siasa
 
Tatizo si ndugai..tatizo chama kilichompendekeza..chama makini hakiwezi kuruhusu mtu mtupu kama ndugai kuongoza organ kama bunge
 
Akitolea ufafanuzi hoja ya Mwigulu Nchemba bungeni leo asubuhi naibu spika amesema kuwa tangu bunge hili la kumi lianze halijawahi kupokea ushahidi wowote kutoka kwa wabunge wanaotakiwa kufanya hivyo na kiti! Ilikuwa ni baada ya Mwigulu kuomba mwongozo kuhusu maneno ya Mnyika kuwa alihusika kwenye wizi wa EPA.

Concern yangu kubwa hapa ni alichokisema Ndugai kuwa wabunge hasa wa upinzani wajiangalie na matamshi yao ndani ya bunge na wawe wapole wanapotakiwa kufuta kauli zao kuliko kujifanya wana ushahidi ukizingatia kuwa hakuna ushahidi uliowahi kuwasilishwa kwenye bunge hili.

Sote tunakumbuka matukio kama hayo bungeni na idadi ya wabunge waliowahi kuambiwa walete ushahidi kuthibitisha wayasemayo.Zitto Kabwe,Godbless Lema ni mfano wa wabunge ambao wamewahi kutakiwa ushahidi kwenya bunge hili na wao wenyewe kusema baadaye kuwa wameshawasilisha.

Pia kwenye sakata la Godbless Lema,Spika Makinda ameshawahi kulithibitishia bunge kuwa ameupokea.Hiyo ilikuwa ni baada ya kuombwa mwongozo na Zitto(kama sikosei) kuwa ushahidi wa Lema usomwe bungeni kama umeshawasilishwa mezani kwake naye akajibu kuwa amepokea huo ushahidi na wanaendelea kuufanyia kazi.

Hata kwa upande wa Zitto,Makinda aliwahi kuthibitisha kupokea ushahidi wake na baadaye Zitto mwenyewe kuthibitisha.
Ndugai pia aliendelea kudai kuwa wabunge waache kudanganya kwenye mitandao kuwa wamewasilisha ushahidi huku wakijua kuwa hawajafanya hivyo.

Hata hili la Mnyika Ndugai amesema kilichowasilishwa ni utangulizi tu na wala sio ushahidi wa alichokizungumza kinyume na inavyosemwa kwenye mitandao na magazeti!

Hili linaleta picha gani?kwamba wabunge wetu wanadanganya? Spika Makinda alidanganya? Wabunge wetu kwa kushirikiana na Makinda wametudanganya na Ndugai ameamua kuwatolea uvivu?Kwamba Kinachowasilishwa huwa hakikidhi kuitwa Ushahidi wa tuhuma husika?

Tujadili.
BUNGE LETU NI CHURCH OF LIERS!!! kuhusu EPA na Ufisadi wote bado makinda eti haamini mpaka kuwepo na ushahidi! she come from church of liers! wizi wa wanasiasa hauna nyayo! huwezi hata siku moja ukagundua kadokoa vipi au kapewa rushwa kiasi gani! Makinda amka mama ! wewe ngoja tuu wajifanye kumsaidia mu Iran na hao west europe na USA watazidi kuwalipua na ma aakounti yao yaliyo uswiss! hao sita ilikuwa na kuwatia jamba jamba kuwa kama mkiendelea tuuu kumbeba muiran basi sisi tuna list za wote waliiibia nchi yenu na tutatoa hadharani!!. usicheze ma myahudi hapa duniani!
 
Back
Top Bottom