Nyankurungu2020
JF-Expert Member
- Oct 2, 2020
- 4,086
- 6,568
Tunapoenda tunaelekea pabaya sana. Na hii ni dalili mbaya sana ya kuwepo kwa viongozi wanafiki na wasiofaa katika jamii yetu.
Rais wa JMT ni sehemu ya bunge, bunge la JMT lina mamlaka ya kuisimamia Serikali na kuhoji pale serikali inapofanya ndivyo sivyo, hili lipo wazi kabisa kwa mujibu wa katiba ya JMT ibara ya 63.
Leo hii spika Ndugai anaongea mambo na kuwaona watanzania ni wajinga? Kwamba alienda huko China na kuonana na bodi ya kampuni ya China Merchant, na walitoa presentation nzuri yenye kumuhakikishia kuwa wakipewa kazi ya kujenga mradi wa bandari Bagamoyo, utakuwa na faida kw Tanzania
Kwa kumalizia anasema mkuu wa nchi aliyekuwepo alipotoshwa na ndio maana akaupiga chini mradi wa Bagamoyo. Sasa kama alipotoshawa na wewe na Bunge lako mna mamlaka ya kuhoji, na kuisimamia serikali kwa nini hamkueleza ukweli? Leo unasubiri hayupo baaada ya kufariki ndio unatufanya watoto?
Wewe kama mkuu wa bunge, ulishindwa vipi kujadili na wabunge ili kumuambia mkuu wa nchi aliyekuwepo kuwa anapotoshwa? Na je, kama alikuwa hapotoshwi ila kulikuwa na mashariti yasiyo na tija?
Rais wa JMT ni sehemu ya bunge, bunge la JMT lina mamlaka ya kuisimamia Serikali na kuhoji pale serikali inapofanya ndivyo sivyo, hili lipo wazi kabisa kwa mujibu wa katiba ya JMT ibara ya 63.
Leo hii spika Ndugai anaongea mambo na kuwaona watanzania ni wajinga? Kwamba alienda huko China na kuonana na bodi ya kampuni ya China Merchant, na walitoa presentation nzuri yenye kumuhakikishia kuwa wakipewa kazi ya kujenga mradi wa bandari Bagamoyo, utakuwa na faida kw Tanzania
Kwa kumalizia anasema mkuu wa nchi aliyekuwepo alipotoshwa na ndio maana akaupiga chini mradi wa Bagamoyo. Sasa kama alipotoshawa na wewe na Bunge lako mna mamlaka ya kuhoji, na kuisimamia serikali kwa nini hamkueleza ukweli? Leo unasubiri hayupo baaada ya kufariki ndio unatufanya watoto?
Wewe kama mkuu wa bunge, ulishindwa vipi kujadili na wabunge ili kumuambia mkuu wa nchi aliyekuwepo kuwa anapotoshwa? Na je, kama alikuwa hapotoshwi ila kulikuwa na mashariti yasiyo na tija?