Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,908
- 30,252
NDOTO KUTOKA MTAA WA KIUNGANI GEREZANI 1957
Ali umenirudisha nyuma mbali sana katika maisha ya utoto wangu.
Nilikuwa nakaa Manhattan jirani na Hudson River New York.
Mwenyeji wangu akaniambia kuwa tukitoka hapo nje tu tukavuka mto tutafika nyumbani kwa Harry Belafonte.
Bahati mbaya yeye hafahamianinae kwa hiyo hakuweza kunipeleka.
Bibi yangu Zena bint Farijallah aliiona movie ya Harry Belafonte, "Island in the Sun," katika miaka ya 1950 na kila ikipatikana nafasi atanihadithia senema ile.
Kitu alichokipenda bibi yangu katika senema ile ni msichana wa Kizungu kumpenda Belafonte mtu mweusi.
1957 nina miaka 5 tunaishi Mtaa wa Kiungani, Gerezani nasikia radio ikipiga, "Round the Bay of Mexico," nyimbo ya Harry Belafonte na mimi nikijitahidi kuimba.
Natazama picha katika gazeti la Drum kutoka Johannesburg linachukua fikra zangu kwa zile suti walizovaa watu mle.
Niko katika ndoto.
Sikujua kuwa ipo siku nitakutana na mwenye gazeti hili la Drum Jim Bailey Dar es Salaam mimi nikiwa kijana na tutafanya kazi pamoja ya kuchapa kitabu kutoka Drum mimi nikiwa mhariri wake.
Ally Sykes ndiye aliyenikutanisha na Jim Bailey.
Wala haikunipitikia kuwa iko siku nitafika Johannesburg na nitatembea kwenye mitaa yake na kusikiliza South African Jazz ya kina Sipho na Hugh Masekela.
Hizi zote zilikuwa ndoto zangu utotoni wala haikunipitikia kuwa hizi ndoto siku moja zitakuwa kweli.
Nilikuwa kwenye ndege nakwenda Mbabane Swaziland safari yangu ya kwanza na nikimaliza shughuli zangu baada ya kiasi cha mwezi nitakwenda Johannesburg nikamuone Jim Bailey.
Nimekaa na Mzungu Muafrika Kusini katika mazungumzo nikamfahamisha kuwa nitakwenda Johannesburg akaniuliza kinachonipeleka nikamwambia matembezi na kumuona rafiki yangu Jim Bailey.
Akashangaa sana akataka kujua nimejuana vipi na Jim Bailey.
Akanipa pole akaniambia, "Jim Bailey alikuwa jirani yangu tumemzika mwezi uliopita."
Jim Bailey ndiye aliyenipatia picha za Julius Nyerere na Sheikh Suleiman Takadir na picha ya Julius Nyerere na Mama Sakina, Bi. Titi Mohamed na Tatu bint Mzee wako uwanja wa ndege wanamsindikiza Nyerere safari ya kwanza UNO February, 1955.
Ali Boxer ahsante sana.
Ali Boxer ahsante sana.
Ali umenirudisha nyuma mbali sana katika maisha ya utoto wangu.
Nilikuwa nakaa Manhattan jirani na Hudson River New York.
Mwenyeji wangu akaniambia kuwa tukitoka hapo nje tu tukavuka mto tutafika nyumbani kwa Harry Belafonte.
Bahati mbaya yeye hafahamianinae kwa hiyo hakuweza kunipeleka.
Bibi yangu Zena bint Farijallah aliiona movie ya Harry Belafonte, "Island in the Sun," katika miaka ya 1950 na kila ikipatikana nafasi atanihadithia senema ile.
Kitu alichokipenda bibi yangu katika senema ile ni msichana wa Kizungu kumpenda Belafonte mtu mweusi.
1957 nina miaka 5 tunaishi Mtaa wa Kiungani, Gerezani nasikia radio ikipiga, "Round the Bay of Mexico," nyimbo ya Harry Belafonte na mimi nikijitahidi kuimba.
Natazama picha katika gazeti la Drum kutoka Johannesburg linachukua fikra zangu kwa zile suti walizovaa watu mle.
Niko katika ndoto.
Sikujua kuwa ipo siku nitakutana na mwenye gazeti hili la Drum Jim Bailey Dar es Salaam mimi nikiwa kijana na tutafanya kazi pamoja ya kuchapa kitabu kutoka Drum mimi nikiwa mhariri wake.
Ally Sykes ndiye aliyenikutanisha na Jim Bailey.
Wala haikunipitikia kuwa iko siku nitafika Johannesburg na nitatembea kwenye mitaa yake na kusikiliza South African Jazz ya kina Sipho na Hugh Masekela.
Hizi zote zilikuwa ndoto zangu utotoni wala haikunipitikia kuwa hizi ndoto siku moja zitakuwa kweli.
Nilikuwa kwenye ndege nakwenda Mbabane Swaziland safari yangu ya kwanza na nikimaliza shughuli zangu baada ya kiasi cha mwezi nitakwenda Johannesburg nikamuone Jim Bailey.
Nimekaa na Mzungu Muafrika Kusini katika mazungumzo nikamfahamisha kuwa nitakwenda Johannesburg akaniuliza kinachonipeleka nikamwambia matembezi na kumuona rafiki yangu Jim Bailey.
Akashangaa sana akataka kujua nimejuana vipi na Jim Bailey.
Akanipa pole akaniambia, "Jim Bailey alikuwa jirani yangu tumemzika mwezi uliopita."
Jim Bailey ndiye aliyenipatia picha za Julius Nyerere na Sheikh Suleiman Takadir na picha ya Julius Nyerere na Mama Sakina, Bi. Titi Mohamed na Tatu bint Mzee wako uwanja wa ndege wanamsindikiza Nyerere safari ya kwanza UNO February, 1955.
Ali Boxer ahsante sana.
Ali Boxer ahsante sana.