Ndoto yangu - Wabunge CCM wataiondoa serikali yao

Candid Scope

JF-Expert Member
Nov 8, 2010
11,885
6,885
Nimeota ndoto kama ni ya kweli au la lakini nimeamua kuianika hapa.

Wabunge wa CCM ni kama timu ya mpira daraja la kwanza. Timu isipofanya vizuri huteremka daraja, haina maana mchezaji ameteremka daraja.

Zitto Kabwe nyuma yake wako wengi tu na anawajua. Lakini hawako kimbelembele katika kuweka sahihi, na sahihi zinawekwa kwa mahesabu zikamilike. Lakini kazi maalum ipo inasubiriwa.

Wabunge vijana wa CCM wengi wameshachoshwa na Mfumo dume, ingawa hawako tayari baadhi yao kuinyooshea serikali yao kidole kama Filikunjombe alivyofanya.

Busara serikali ya Kikwete isipotumika, nafasi hii wasijekujutia orodha ile ya wabunge waliotia sahhihi ikageuka kupigia kura kutokuwa na imani si na waziri mkuu ila Serikali nzima, maana yake kuitisha uchaguzi mpya tena. Na hii wengi tutabaki kushangaa idadi kubwa ya wabunge wa CCM watakavyoikataa serikali yao na kuhamia upinzani baada ya kuisulubu serikali yao. Cha msingi serikali ikiteleza tu hapo ni sawa na kanyaga boya baharini. Wabunge wengi ni wazuri tu ila tatizo ni mfumo wa uongozi ni mbovu kabisa isivyotokea katika historia ya nchi hii.
Nyerere aliona yote haya na alishasema lakini tulimpuuzi na leo tunajuta.
 
Mkuu mbona hali halisi ni zaidi ya ndoto?
Wabunge wa ccm watasaidia sana kuizika serikali yao kwa mioyo yao migumu kufanya maamuzi.
 
Back
Top Bottom