Ndoto yangu usiku wa leo: Wale ndege aina ya "njiwa' walitolewa kama zawadi ili kuwaziba midomo waliopewa huko katika Bara fulani la mbali

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
47,013
144,371
Usiku wa kuamkia leo nimeota kuwa kuna mfalme mmoja katika nchi ambayo jina limenitoka, katoa zawadi ya njiwa wazuri kwa watu mashuhuru katika sherehe aliyoiandaa kwa yeye kutimiza miaka kadhaa ya kuzaliwa (Birthday).

Nilijiuliza sana maana ya ile ndoto na baada ya kutafakari kwa kina, nikagundua kuwa ujumbe kwenye ndoto yangu ni kuwa wale waliopewa wale njiwa kama zawadi ni watu ambao hawezi kuwapa kitu kingine zaidi ya vitu kama hivyo ili kuwaweka zaidi karibu yake na pia kuwaziba midomo.

Wadau, hii ndio ilikuwa ndoto yangu usiku wa leo na ambayo nimejaribu kuwashirikisha labda na nyinyi mnaweza kunisaidia katika kuitafsri ndoto hii.
 
Kweli ndoto!!

Kama ndoto unazoota ndo kama hizi bado kuna safari ndefu ya kwenda mbele, bola uoteshe miti au papai utakula, acha kujitesa na ndoto za namna Hiyo.

Pia usiwaongopee watu , hamna cha ndoto hapo, kuwa na haya mbele za Mungu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom