Ndoto: Sehemu muhimu kwa afya ya hifadhi ya akili

Mshana Jr

Platinum Member
Aug 19, 2012
269,605
696,697
Wafu pekee ndio hawaoti na hawaoti kwakuwa hawana kumbukumbu tena na hawana kumbukumbu tena kwakuwa hawana uhai tena.

Kila binadamu kamili lazima awe na vivuli vitatu kukosa kuwa na vivuli vyote vitatu ni ulemavu wa kiroho sawa tu na kukosa kuota kabisa.

Ndoto za kawaida ni uchambuzi wa matukio ya siku nzima tuliyowaza kunena na kutenda, jana leo na mbeleni.

Ni katika mchakato wa kuchuja matukio ya kuhifadhi kwenye database ya ubongo ndio watu huota wakati huo mwili ukiwa katika dormance state. Ni vitu vinavyotokea bila ridhaa ya mhusika.

Mchakato mwingine wowote ufuatao wa ndoto za aina nyingine zile za wanga, wachawi, maono na taarifa msingi wake ni hizi ndoto asili ni katika mchakato wa huo wa kuchuja na kuchambua matukio ya kuchukua na kuacha ndio binadamu ama niseme kiumbe hai hupata mtimbwiliko uitwao ndoto.

Ni katika mnyambulisho huo wa matukio kunakuwa na matukio ya uhifadhi wa muda mfupi, muda wa kati na muda wa kudumu.

Matukio ya uhifadhi wa muda mfupi huishia katika mlango wa tano wa fahamu sawa na ndoto zake. Matukio ya muda wa kati huishia katika mlango wa sita sawa na ndoto zake. Angalia kuna ndoto za mwaka jana unaweza kuzikumbuka vizuri sana tofauti na ndoto za wiki iliyopita.

Vile vile na matukio ya kudumu huhifadhiwa kwenye mlango wa nane wa fahamu yakiwa yamechujwa hasa kwenye mlango wa saba na kuchambuliwa kwenye mlango wa sita matukio haya na ndoto zake huwa ni ya kudumu bila kujali umri wake.

Je ni kwanini kuna mchujo mkali kiasi hiki?

Chukulia database ya inavyowekewa ulinzi ili isiathiriwe na kirusi chochote.Basi hivyo ndivyo hali ilivyo kwenye software ya database ya ubongo.

Ubongo wako ndio data center, database ya kumbukumbu zako zote. Ukidisturb hiyo umekwisha.Vichaa na mwendawazimu huchezewa hapa, pakiguswa hapa ama pakiwa over loaded kuchanganyikiwa ni lazima.

Kwa ufahamu usiojua ni kwamba ndoto ndio maabara ya kupima kuchuja, kuchambua kuweka katika makundi husika aina za kumbukumbu za kutunzwa na ubongo. Asiyeota hana kumbukumbu na tafsiri yake ni moja tuu maabara yake haifanyi kazi.
 
Mkuu hata ndoto za kutisha pia?
Ndio hasa kama hazihusiani na mambo ya giza kwa uzoefu wangu ni kwamba watu wanaoshinda bila stress huwa na ndoto njema sana lakini ukishinda full worries, visasi na mambo mabaya hata usiku mandoto yako yatatisha
Kula sana na milalo ya kitandani pia huchangia maabara kushindwa kufanya kazi yake sawa sawa ni sawa na lab ambayo iko congested.. Huku chemicals zikimwagika huku na kule
 
Huwa naota ndoto za kipindi cha nyuma mara nipo kwenye mitihani nafanya wakati sijafanya Maandalizi, mara nipo bwenini chuoni..... Sipendi kweli... Kwann nisiote future yangu naota past tu.

Utakuwa unaambiwa kuwa huna muda mrefu katika mahali ulipo na unatakiwa kupasoma zaidi ili kuelewa.
 
Shukrani sana Mkuu kuna mtu karibu kila siku anaota ndoto za kutisha. Mie nikihadithiwa ndoto husika sina mbavu maana baadhi zinachekesha sana Mkuu.

Ndio hasa kama hazihusiani na mambo ya giza kwa uzoefu wangu ni kwamba watu wanaoshinda bila stress huwa na ndoto njema sana lakini ukishinda full worries, visasi na mambo mabaya hata usiku mandoto yako yatatisha
Kula sana na milalo ya kitandani pia huchangia maabara kushindwa kufanya kazi yake sawa sawa ni sawa na lab ambayo iko congested.. Huku chemicals zikimwagika huku na kule
 
Shukrani sana Mkuu kuna mtu karibu kila siku anaota ndoto za kutisha. Mie nikihadithiwa ndoto husika sina mbavu maana baadhi zinachekesha sana Mkuu.
Mchunguze mdadisi utaona mfanano wa ajabu na maisha yake ya siku
 
Kwa hapa Tanzania ukiota ndoto usitangaze maana pogba akisikia utajikuta upo gereza la kisongo, kuota ndoto hapa Tanzania ni kosa kubwa na unaweza kukaa jela kwa muda mrefu
inategemea unaota ndoto gani... Kama ni ndoto maono ama ndoto taarifa na huna NGUVU baki nayo moyoni usitafute sifa.. Anga limechafuka
tapatalk_1523295127436.jpeg
 
kwahiyo itakua kuna watu walikua wananipinga kiroho sio?
au itakua wananionea wivuu???

Sio watu tuu.. Ulimwengu wa roho ni mpana sana kama kinga zako za kiroho ni dhaifu mapambano hayatakoma.... Kasome hii kinga za kiroho
 
Jee kumuota marehemu aliyekufa... kunakuwa na uhusiano upi maana kuna siku uwa namuota jamaa flani tukiwa katika hali ya bashasha.
 
Jee kumuota marehemu aliyekufa ...kina kuwa na uhisiano upi maana kuna siku uwa namuota jamaa flani tukiwa katika hali ya bashasha.
Ndoto za kawaida retrieval of the past memories... Sometimes ndoto kama hizi jua tu kwamba roho yake haiko mbali nawe
 
Mkuu kwanza shukrani kwa mada hii, nina Mambo napenda unieleweshe.

1. Hili la milango ya fahamu kwangu linanipa utata, nimeona umetaja takribani milango hadi nane ya fahamu. Nisaidie kunichambulia japo kwa ufupi kila mlango na kazi zake.

2. Ndoto maono na ndoto taarifa zina utofauti gani?

Binafsi naota sana ndoto tatizo langu huwa sikumbuki ndoto nayoota na kuna wakati kwa usiku mmoja naweza kuota ndoto hata mbili shida inakuja kwenye kukumbuka.

Naweza kumbuka kipande kifupi kingine sikumbuki, shida ni nini mkuu?
 
Mkuu kwanza shukrani kwa mada hii, nina Mambo napenda unieleweshe.

1. Hili la milango ya fahamu kwangu linanipa utata, nimeona umetaja takribani milango hadi nane ya fahamu. Nisaidie kunichambulia japo kwa ufupi kila mlango na kazi zake.

2. Ndoto maono na ndoto taarifa zina utofauti gani?

Binafsi naota sana ndoto tatizo langu huwa sikumbuki ndoto nayoota na kuna wakati kwa usiku mmoja naweza kuota ndoto hata mbili shida inakuja kwenye kukumbuka.

Naweza kumbuka kipande kifupi kingine sikumbuki, shida ni nini mkuu?

Asante sana
La kwanza jibu lake utalipata hapa mawasiliano ya kiroho katika milango nane ya fahamu

La pili
Ndoto maono hukujia kwa ajili ya watu wengine wengi... Ni ujumbe unatumwa kupitia wewe.. Manabii na watabiri hutumia sana hii nafasi

La tatu
Kumbukumbu ya ndoto ulizoota.. Hizi hupaswi kuhangaika nazo kwakuwa kuota kupo tu kama uko kamili upstairs...
 
32 Reactions
Reply
Back
Top Bottom