Yesu Anakuja
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 9,374
- 19,032
Sijajua nini Mungu amepanga kwenye maisha yangu, niwe muwazi, nimeokoka, though mimi sio malaika, kwa uwezo wa Mungu napambana na dhambi, na nazidi kujitakasa kila wakati kwasababu najua wakati mwingine namuuzi Mungu na wanadamu kutokana na madhaifu yangu kama mwanadamu, madhaifu ambayo hata hivyo sio justification ya kutenda dhambi. Mungu atusaidie, na pamoja na yooote hayo, pamoja na madhaifu yangu yoote, Mungu bado amenipenda.
Maishani mwangu nilishawahi kuota ndoto nyingi sana za Kimungu, kwani kuna ndoto unaota ukishiba ugali, na zingine unaota unaona Mungu anaongea na wewe kabisa na haitoki moyoni hata miaka nenda rudi. nilishawahi kuota ndoto malaika wamekizunguka kiti cha enzi wa Mungu, wanaimba wimbo, ni miaka kadhaa sasa, huo wimbo hadi leo upo akilini mwangu na niliusikia kwenye ndoto tu. nilishawahi kuonyeshwa mambo mengi ambayo sitayazungumzia hapa kwasababu hiyo sio ndoto niliyotaka kuwashirikisha leo. Ndoto niliyoiota ni hii:-
Niliota nipo kwenye shughuli zangu, tukashambuliwa na maadui hatari mno wameshika mapanga wanadhuru watu, ilikuwa ni ndoto lakini nilikuwa naelewa kila kinachoendelea hivyo ilikuwa kama ni ndoto lakini ni maono kwasababu nilikuwa naona fulani hivi. walikuja wakishambulia watu wengi, walipofika kwangu, yule kiongozi wao akawaambia hao walio chini yake "HUYU MWACHENI KWASABABU HUYU NI MALI YA YESU", ever since that moment, roho yangu ikaanza kuimba wimbo wa kukiri kwamba mimi ni Mali ya Yesu na sitadhurika, huo wimbo hautoki moyoni mwangu hadi sasahivi....unaimbwa "mimi ni mali ya Yesu mmmmhh mmhhh, mali ya Yesu, mhhmm mmhh,Mali ya Yesu......" ni wimbo mzuri sana. sisemi kwamba nataka kuwa mwimbaji, hicho kipaji sina. ila ninachotaka kuwahakikishia ni kwamba, wote waliokabidhi maisha yao kwa Yesu, wanakuwa mali ya Yesu.
nimeshaona maono siku kadhaa mfululizo pia ikionyesha dunia hii ipo mwishoni kabisa, nikaona mvurugano umetokea watu wanakimbia kila mahali hata hawajui waende wapi, lakini wameshachelewa, wametumia muda mwingiii kwa ajili ya mambo ya dunia hii, muda ambao Mungu aliwapatia, they just misused it.
Neno la Mungu linasema, wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio Jina lake. Zaburi 91 inasema, Aketiye mahali pa siri pake Aliye juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi. Nitasema, BWANA ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu nitakayemtumaini.
Mungu amenifundisha kitu kimoja kwamba, tunaweza kuwa tunategemea vitu vingi sana hapa duniani, pesa, connections serikalini, kazi, cheo, wazazi, ndugu, uchawi, etc, lakini ukweli ni kwamba, Jesus Christ is the only trusted refuge that will never let you down. Yesu pekee ndiye kimbilio la uhakika, na alishasema, yeyote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe. wale wanaokaa katika uvuli wake, yeye atakuwa kimbilio lao na ngome yao. Mungu hutoa ulinzi na warning kwa shetani kutowagusa kabisa watu wake, na shetani akikugusa jua Mungu ameruhusu na amekuwekea mlango wa kutokea katika jaribu hilo lakini kwa hali ya kawaida wote walio wa Mungu hulindwa na kupiganiwa na Mungu hata hatuhitaji tegemeo lingine. yeye pekee ndiye uhakika wetu.
walio wa Mungu watanielewa, na watamtafuta zaidi Mungu baada ya kusoma haya, ila wale walio wa shetani watapinga kwasababu baba yao shetani hapendi ukweli huu ujulikane. Mungu akusaidie,Mungu anisaidie, tumwone yeye pekee ndiye kimbilio letu, tukabidhi maisha yetu kwake katika nyakati hizi za mwisho, kabla giza halijaifikia dunia. Amen.
Maishani mwangu nilishawahi kuota ndoto nyingi sana za Kimungu, kwani kuna ndoto unaota ukishiba ugali, na zingine unaota unaona Mungu anaongea na wewe kabisa na haitoki moyoni hata miaka nenda rudi. nilishawahi kuota ndoto malaika wamekizunguka kiti cha enzi wa Mungu, wanaimba wimbo, ni miaka kadhaa sasa, huo wimbo hadi leo upo akilini mwangu na niliusikia kwenye ndoto tu. nilishawahi kuonyeshwa mambo mengi ambayo sitayazungumzia hapa kwasababu hiyo sio ndoto niliyotaka kuwashirikisha leo. Ndoto niliyoiota ni hii:-
Niliota nipo kwenye shughuli zangu, tukashambuliwa na maadui hatari mno wameshika mapanga wanadhuru watu, ilikuwa ni ndoto lakini nilikuwa naelewa kila kinachoendelea hivyo ilikuwa kama ni ndoto lakini ni maono kwasababu nilikuwa naona fulani hivi. walikuja wakishambulia watu wengi, walipofika kwangu, yule kiongozi wao akawaambia hao walio chini yake "HUYU MWACHENI KWASABABU HUYU NI MALI YA YESU", ever since that moment, roho yangu ikaanza kuimba wimbo wa kukiri kwamba mimi ni Mali ya Yesu na sitadhurika, huo wimbo hautoki moyoni mwangu hadi sasahivi....unaimbwa "mimi ni mali ya Yesu mmmmhh mmhhh, mali ya Yesu, mhhmm mmhh,Mali ya Yesu......" ni wimbo mzuri sana. sisemi kwamba nataka kuwa mwimbaji, hicho kipaji sina. ila ninachotaka kuwahakikishia ni kwamba, wote waliokabidhi maisha yao kwa Yesu, wanakuwa mali ya Yesu.
nimeshaona maono siku kadhaa mfululizo pia ikionyesha dunia hii ipo mwishoni kabisa, nikaona mvurugano umetokea watu wanakimbia kila mahali hata hawajui waende wapi, lakini wameshachelewa, wametumia muda mwingiii kwa ajili ya mambo ya dunia hii, muda ambao Mungu aliwapatia, they just misused it.
Neno la Mungu linasema, wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio Jina lake. Zaburi 91 inasema, Aketiye mahali pa siri pake Aliye juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi. Nitasema, BWANA ndiye kimbilio langu na ngome yangu, Mungu wangu nitakayemtumaini.
Mungu amenifundisha kitu kimoja kwamba, tunaweza kuwa tunategemea vitu vingi sana hapa duniani, pesa, connections serikalini, kazi, cheo, wazazi, ndugu, uchawi, etc, lakini ukweli ni kwamba, Jesus Christ is the only trusted refuge that will never let you down. Yesu pekee ndiye kimbilio la uhakika, na alishasema, yeyote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe. wale wanaokaa katika uvuli wake, yeye atakuwa kimbilio lao na ngome yao. Mungu hutoa ulinzi na warning kwa shetani kutowagusa kabisa watu wake, na shetani akikugusa jua Mungu ameruhusu na amekuwekea mlango wa kutokea katika jaribu hilo lakini kwa hali ya kawaida wote walio wa Mungu hulindwa na kupiganiwa na Mungu hata hatuhitaji tegemeo lingine. yeye pekee ndiye uhakika wetu.
walio wa Mungu watanielewa, na watamtafuta zaidi Mungu baada ya kusoma haya, ila wale walio wa shetani watapinga kwasababu baba yao shetani hapendi ukweli huu ujulikane. Mungu akusaidie,Mungu anisaidie, tumwone yeye pekee ndiye kimbilio letu, tukabidhi maisha yetu kwake katika nyakati hizi za mwisho, kabla giza halijaifikia dunia. Amen.