Ndoto huwa zinatimia? Tushirikishane na kupeana uzoefu

Hiyo ya Dada yako kuwa mjamzito sio ndoto ni kwamba ulikiwa umisha sikia sema ulikuwa umesahau,so hilo jambo likaibuka usingizini.
Hujanielewa. Sikuwa na taarifa. Niliota ndoto na kumwona mjamzito na pia amejifungua mtoto wa kike.
Na kupatia jinsia nayo nilisikia?
 
Mimi Juzi nimeota kuwa tulikuwa tunakimbizwa simba Mimi na mfanyakazi mwenzangu ambaye ni KE,kulikuwa na gema Fulani ilitakiwa turuke Mimi nikaanza kuruka badaye nikamsaidie yeye kuvuka kwa kumshika mikono na kumvuta Mara paa simba akaanza kumrarua na kumvuta na kuondoka Naye.

Nikaaa pale kwenye gema nikitafakari namna ya kwenda kutoa taarifa kwamba Fulani ameliwa na simba,badaye wazo likaniijia kwamba nifatilie yule simba nikafika nikamkuta simba amelala na amemla yule Dada kimebaki kichwa tu.badaye ndio nikasituka
Kuota wanyama ndotoni mara nyingi huwa ni mizimu ya familia. Mwambie huyo dada aombe Mungu sana
 
Katika jambo ambalo huwa linanisumbua ni hili la ndoto.
Namshukuru Mungu huwa naota sana haipati siku 3 bila kuota jambo lolote, hata lisilonihusu mm laweza linalohusu jirani, ndugu na watu wanaonizunguka.

Katika ndoto nyingi moja hii ilitimia kwa usahihi ni kuhusu dada yangu aliye sumbuka kupata mtoto muda wa miaka takribani 10 akiwa kwenye ndoa na kumwota mjamzito na amejifungua mtoto wa kike..

Nikampigia simu baada ya siku chache na kumuuliza kama mjamzito akasema ndio na muda wa kujifungua ulipofika na kweli alipata mtoto wa kike...

Nyingine bado kutimia maana huwa na kitabu maalumu ambacho huandika ndoto na akitimia naiwekea alama ya tick

Je, wewe unauzoefu gani juu ya ndoto?
Me najuaga ndoto ambazo huwa zinatimia ni ile unaota unakata gogo au unakojoa, hizo ndoto hazichukui muda kutimia yani papo hapo ndoto yako inakua kweli, hizo ndoto zingine huwa naona kama changa tu.
 
Daah, mwaka Jana Mwezi wa 7 niliota nipo shule ya msingi na nimevaa mpaka sare kabisa, Muda huo nilikuwa nimepata sehemu ya kupiga deiwaka baada ya kukaa benchi na Corona. Asubuhi baada ya kuamka kwenda sehemu ya kazi, nikaambiwa baharia hapa kuhusu mkataba haiwezekani.

Wataalamu wa mambo wanasema ukiota upo shule jua mambo yako yatarudi nyuma.
 
Zinatimia ila lazima ujue ndoto inayotokana na kuvimbiwa na ubwabwa maharage na ndoto yenye kaukweli....

Ndoto za ukweli Ina taste yake mara nyingi unazijua kbs km wewe ni muotaji wa ndoto za kweli
Aisee basi mimi nadhani huwa naota hizo za baada ya kuvimbiwa maana hazitimiagi kabisa 🤔😄
 
Katika jambo ambalo huwa linanisumbua ni hili la ndoto.
Namshukuru Mungu huwa naota sana haipati siku 3 bila kuota jambo lolote, hata lisilonihusu mimi laweza linalohusu jirani, ndugu na watu wanaonizunguka.

Katika ndoto nyingi moja hii ilitimia kwa usahihi ni kuhusu dada yangu aliyesumbuka kupata mtoto muda wa miaka takribani 10 akiwa kwenye ndoa na kumuota mjamzito na amejifungua mtoto wa kike..

Nikampigia simu baada ya siku chache na kumuuliza kama mjamzito akasema ndio na muda wa kujifungua ulipofika na kweli alipata mtoto wa kike...

Nyingine bado kutimia maana huwa na kitabu maalumu ambacho huandika ndoto na akitimia naiwekea alama ya tick

Je, wewe una uzoefu gani juu ya ndoto?
Jifunze na tafsiri ya ndoto unazoota.kuna nyingine ni za kukuathiri bila kujua. Naamini kabisa Kuna ndoto unaota unaziona salama kumbe sio salama Kama unavyofikiri. Refer ndoto aliyoota Yusuph.....ilimheshimisha baadae Ingawaje ilimsotesha Sana.
 
Jifunze na tafsiri ya ndoto unazoota.kuna nyingine ni za kukuathiri bila kujua. Naamini kabisa Kuna ndoto unaota unaziona salama kumbe sio salama Kama unavyofikiri. Refer ndoto aliyoota Yusuph.....ilimheshimisha baadae Ingawaje ilimsotesha Sana.
Kujua tafsiri ya ndoto ni neema ya Mungu
 
Katika jambo ambalo huwa linanisumbua ni hili la ndoto.
Namshukuru Mungu huwa naota sana haipati siku 3 bila kuota jambo lolote, hata lisilonihusu mimi laweza linalohusu jirani, ndugu na watu wanaonizunguka.

Katika ndoto nyingi moja hii ilitimia kwa usahihi ni kuhusu dada yangu aliyesumbuka kupata mtoto muda wa miaka takribani 10 akiwa kwenye ndoa na kumuota mjamzito na amejifungua mtoto wa kike..

Nikampigia simu baada ya siku chache na kumuuliza kama mjamzito akasema ndio na muda wa kujifungua ulipofika na kweli alipata mtoto wa kike...

Nyingine bado kutimia maana huwa na kitabu maalumu ambacho huandika ndoto na akitimia naiwekea alama ya tick

Je, wewe una uzoefu gani juu ya ndoto?
kawaida huwezi kuota bila kulala ,vile vile huwezi kuzifanikisha hizo ndoto kwa kulala. kwa vile pia ukilala sana utakula ulichokiota ni wewe uamke uzitimize hizo ndoto. kwenye ndoto pia kuna jinamizi na kuna njozi. njozi amka fanikisha na jinamizi simulia na kufuru.
 
Daah, mwaka Jana Mwezi wa 7 niliota nipo shule ya msingi na nimevaa mpaka sare kabisa, Muda huo nilikuwa nimepata sehemu ya kupiga deiwaka baada ya kukaa benchi na Corona. Asubuhi baada ya kuamka kwenda sehemu ya kazi, nikaambiwa baharia hapa kuhusu mkataba haiwezekani.

Wataalamu wa mambo wanasema ukiota upo shule jua mambo yako yatarudi nyuma.
Umeibiwa nyota Mzee au imefifishwa hautafanya cha maana had usolve help tatzo
 
Back
Top Bottom