Ramea
JF-Expert Member
- Mar 19, 2015
- 2,146
- 4,051
Mimi kutafsiri ndoto alinifundisha mzee wangu. Kwenye yote hayo umegusa moja tu, ishu ya kupanda mlima. Kupanda kwa shida au kuanguka mlimani, ghorofani, mtini.. hiyo ni ndoto yangu kuu inayonipa mwelekeo wa mafanikio au anguko kimaisha na huwa hivyo kwa 100%.
Ndoto nyingine alonifundisha mzee wangu kuwa ni mbaya na ndiyo inayo determine siku itaishashe ni kuota una sex na mtu ambaye si mwenza wako. Au kuona uchi wa mtu flan ndotoni. Hatariii. Siku nikiota ndoto kama hiyo siku inayofata kuna kamkosi nitaupata 150% bila chenga.
Nyingi hapo ni porojo, umefananisha tu matukio (lugha ya picha). Soma ndoto za kwenye biblia zilizotafsiriwa na kina YUSUF, hazikuwa za kiramli kama hizo zako. Nitaiandaa mada ya tafsiri za ndoto, siyo huo uongo wako.