NDONDI: Deontay WILDER vs Luis ORTIZ kumaliza ubishi kesho..

screpa

JF-Expert Member
Sep 10, 2015
10,776
15,671
Kesho alfajiri tutashuhudia pambano kubwa la uzito wa juu kati ya Deontay Wilder 'The Bronze Bomber' na Luis Ortiz 'KingKong', hili ni pambano la marudiano baada ya lile la awali liliyofanyika mapema mwaka jana, ambapo Wilder alishinda kwa KO (kwa tabu sana). Endapo Wilder atashinda ataungana na magwiji wengine kama Muhammad Ali kwakuwa atakuwa ameutetea mkanda wake wa WCB kwa mara ya 10 mfululizo, rekodi za hawa wawili ni kama zinavyoonekana hapo pichani...
Screenshot_20191123-061448_1574480189440.jpeg
images.jpeg
 
Ortiz alijitaidi sana pambano la kwanza lakini alikalishwa.namkubali sana Wilder na atanikalishia Tena ortiz
 
Huyu Wilder ana mangumi kombora ambayo huwa yanamfikilisha sana Antony Joshua kuingia nae kwenye pambano.
AJ mtu mwingine mzee hayo maneno na vijembe wanavyotupiana ni mapromoter wanataka watengeneze pesa katika pambano lao liwelamvuto na ndio maana wanakwepana kwepana tu.
 
Ortiz anamkalisha aj..huyu Wilder anamuua aj tunabeba maiti tu.ila Ortiz atakalishwa
 

Similar Discussions

2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom