Ndomba kumrithi Hosea very soon

Status
Not open for further replies.
Swali la msingi la kujiuliza ni kama Hosea ndo kikwazo cha ufisadi, mimi namchukia kwa kuwa na yeye ameiibia nchi hii sana lakini sina uhakika kama yeye ndo kiwazo cha kupambana na ufisadi.

Tusishangilie kwa kitu ambacho akitaleta mabadiliko hapo baadae tunatakiwa kudai PCCB iliyo huru zaidi na sio kiongozi wa PCCB mwadilifu kwani bila yeye kuwa huru hakuna chochote cha maana kitakachotokea.

Naungana na wewe kwa kiasi kikubwa. Lakini nadhani Hosea (in his own right) ni fisadi. Kwa hiyo aondolewe. Lakini tusishangilie sana kwa sababu ulizotoa. Pia nadhani wakiweka mtu mkali/msafi kidogo (mwingine ameshauri akina warioba na ulimwengu) nadhani tunaweza kuona mabadiliko kidogo. Unajua wakiweka mtu serious ambaye hata wakubwa zake wakimlazimisha kukubali jambo akaamua kuwakatalia/kujiuzulu tutakuwa tumepiga hatua. Hili la kudai PCCB huru, ni muhimu lakini maadam kwa sasa halionekani kuwa linawezekana (in the short run) basi tuweke mtu atakayeonyesha angalau tofauti (kama wanavyofanya akina Sita, Mwakyembe nk). Suala la PCCB kuwa na mandate linaweza kuwa gumu kama la kudai katiba mpya! Maana hawa jamaa wote wanaweza kupelekwa Keko!
 
heshima mbele wakuu

taarifa zilizotoka hivi punde kutoka kwenye mitambo na nzi wetu wamekamata kwenye antena zao zinasema muda si mrefu mkulu atampiga chini bw.hosea wa takukuru na kumweka mjeshi ndomba aliyewahi kuwa mkuu wa mkoa wa arusha na baadae mkulu kumrudisha jeshini ili kuweka nidhamu ya jeshi juu. Hapa tutaambiwa hosea anastaafu lakini umri bado mhh!!!!. Pia wale tunaowapigia kelele sana hapa jf kama mwanyika na mwenzie mgonjwa watapigwa chini tukipata dodoso tutaziwasilisha

nzito

natamani kama hili lingetokea leo leo. Mungu ibariki tz
 
Mwinyi akiwa rais, siku moja alimuaigiza malecela kuwa anataka kuona viongozi wapya wenye asili ya kiisilamu wakipewa nafasi za uongozi, muungwana wakati huu alikuwa Tunduru, ambako alikuwa amepewa adhabu ya kwenda huko na bosi wake CCM Dododma, Mwakawago aliyekuwa akimchukia sana,

katika uho mkumbo malecela aliwapromote, Dr. Mtulia, Makamba, na muungwana kuja kuwa waziri mdogo.

FMES...Mkuu siku hizi umekuwa unachangia very low....ktk Uongo uliokuja nao huu sasa too much....

TO assume kauli yako ni kweli....Hicho ni kisa kilichomfanya Malecela kusimama Bungeni Kama Muangalikana na si Wazir Mkuu wakati akitoa shutuma za Mihadhara ya Kiislam?
 
cheo pekee kikubwa kikwete alichopata kuwa promoted hapo nyuma ni cha huo ukuu wa usalama ccm,cheo hicho pia kimepata kukaliwa na watu kama clonel muhando,augustne mrema..ets ....lakini kitendo cha kikwete kuwa promoted kuwa na hicho cheo ..mwaka 1980..alafu in a year akashushwa tena cheo kuwa katibu wa chama wilaya ..newala..et al ..kinatia chaka ..mwalimu alikuwa na mapenzi sana na vijana ...angentoa hapo angempa responsibility kubwa zaidi...hatujapata kujiuliza madudu aliyofanya..its seems ALIKUWA NA FAILI CHAFU...

HUKU ZANZIBAR ALIKUWA MSAIDIZI WA OFISI YA KATIBU MKUU WA CCM ,KISIWANDUI.....HUO NI UTUMISHI WA KAWAIDA KABISA...!

IN SHORT HISTORIA YA NYUMA YA JK HAIKUWA NA LA KUJIVUNIA...NI BAHATI MBAYA WATANZANIA HAKAKUMCHAMBUA VEMA NA WALIMJUA KIPINDI KIFUPI.......

NA ILIKUWA NGUMU KUPATA INFORMATION ZAKE ZA NYUMA HUKO WILAYANI ..KWA WALIOFANYA NAYER KAZI???????

Philimone...Mwalim sio "barometer" ya kuwapima viongozi...mwalim kuna viongozi wengi tu hakuwataka...lkn hio sio sababu ya kuwa walikuwa wachafu...hakumtaka Malecela..was he right...mifano ipo mingi tu!!!
 
mwinyi akiwa rais, siku moja alimuaigiza malecela kuwa anataka kuona viongozi wapya wenye asili ya kiisilamu wakipewa nafasi za uongozi, muungwana wakati huu alikuwa tunduru, ambako alikuwa amepewa adhabu ya kwenda huko na bosi wake ccm dododma, mwakawago aliyekuwa akimchukia sana,

katika uho mkumbo malecela aliwapromote, dr. Mtulia, makamba, na muungwana kuja kuwa waziri mdogo.

hapa data hazijakaa vizuri mkuu wa medani, malecela hakuwepo ktk baraza la kwanza la mawaziri la ally hassan mwinyi, mzee mwinyi alimpatia ukuu wa mkoa wa iringa mzee malecela baada ya kuukosa ubunge 1985, early 1988 mwinyi alimpatia ubalozi malecela kule uingereza na iringa tulipatiwa colonel tarimo kama area commissioner na mama chips akiwa katibu wa ccm mkoa na mkamba akiwa katibu wa ccm wa wilaya iringa vijini by then niko shuleni kama form one ktk shule mojawapo iringa.

Jk aliteuliwa kuwa mbunge na kufanywa naibu waziri maji,nishati madini (waziri alikuwa alnoor kassum nadhani sina hkika sana)na aliyekuwa rais wa awamu ii mzee mwinyi akisaidiwa na makamu wa kwanza wa rais na waziri mkuu wa jmt ndg joseph sinde warioba.

Ni masahihisho tu
 
Hosea amefanya kile alichoweza kufanya na tumshukuru kwa hilo na atakumbukwa kwa mchango wake huo, sipendi niingie ktk dhambi ya kumhukumu maana uteuzi wake pale ulitegemea imani ya mkuu wa nchi kwake na kama atatengua ni yeye pia.

Ni mchapa kazi hodari, mtu wa watu na zaidi ni mtanzania aliyeelimika vizuri, mungu atampatia fursa ingine ya kututumikia kwa ufanisi zaidi.

Nafasi za kiteule na zenye masikio ya umma si za kushindania wala kushabikiwa,

kumbukeni maneno ya mahita wakuluu........

Mzamivu hosea, songa mbele utafanikiwa tu, chapa kazi mpaka dakika ya mwisho..........

Daima mungu ni mwema mkurugenzi hosea
 
WADAU HIZI TAHARIFA NI ZA KWELI !Brig.Gen.Ndomba ALIFASHA PROVE FAIL ARUSHA TAKUKURU ATAIWEZA?
 
hapa lililopo ni siasa tu ujue huyu ndomba nae kapita kwenye ccm tayari nae ni fisadi,mtazamo wangu sawa apewe but pccb iwe taasisi huru kama bunge kwani ipo chini ya mzalamo jk au rafiki wa mafisadi .kumbukeni kuna kipindi jk alisema anawajua wala rushwa but akufanya chochote hapa ha2na rahis tuna msanii !!!!!!!! kama kweli yeye ni rais hamna lolote epa kawapa muda n richmond chai tupu kikwete rais wangu muige kagame tusonge mbele fuata ushauri wa sitta alipotoa vote of thanks . big up samwel sitta wewe ndio kiongozi natamani ungekuwa rais.
 
Sidhani kama tunahitajhi kung'olewa wka mtu mmoja, tunataka mapinduzi ya kimfumo ili kuhakikisha kuwa taratibu, kanuni na sheria ndizo zitakazoongoza vita dhidi ya ufisadi. Morals za watendaji zinaweza kuwa compromised kirahisi iwapo taratibu, kanuni na sheria hazijakaa sawasawa.
Kama inavyoonekana, hawa wanaobadilishana madaraka wote ni kizazi kimoja, tunahitaji zaidi ya mtu kudhibiti hali ya mambo
 
Philimone...Mwalim sio "barometer" ya kuwapima viongozi...mwalim kuna viongozi wengi tu hakuwataka...lkn hio sio sababu ya kuwa walikuwa wachafu...hakumtaka Malecela..was he right...mifano ipo mingi tu!!!

........you are deadly wrong........!
 
hapa data hazijakaa vizuri mkuu wa medani, malecela hakuwepo ktk baraza la kwanza la mawaziri la ally hassan mwinyi, mzee mwinyi alimpatia ukuu wa mkoa wa iringa mzee malecela baada ya kuukosa ubunge 1985, early 1988 mwinyi alimpatia ubalozi malecela kule uingereza na iringa tulipatiwa colonel tarimo kama area commissioner na mama chips akiwa katibu wa ccm mkoa na mkamba akiwa katibu wa ccm wa wilaya iringa vijini by then niko shuleni kama form one ktk shule mojawapo iringa.

Jk aliteuliwa kuwa mbunge na kufanywa naibu waziri maji,nishati madini (waziri alikuwa alnoor kassum nadhani sina hkika sana)na aliyekuwa rais wa awamu ii mzee mwinyi akisaidiwa na makamu wa kwanza wa rais na waziri mkuu wa jmt ndg joseph sinde warioba.

Ni masahihisho tu

.......Malecela kutokuwemo ktk baraza wakati huo hakumaanishi kuwa Mwinyi alikuwa na imani ndogo naye katika uongozi/ushauri..........halafu inaelekea humjui vizuri huyu Mzee.......

.....sorry guys kwa kwenda nje ya mada kidogo.......

.....Back to Dk. Hosea...Unajua habari zikishavuja namna hii mnakuwa mnawapa shida sana watu kuamua...........
 
apumzika na kelele juu yake ziishe, Kwanini post kama ile isiwe open na watu waapply ili lisiwe chaguo la rais kwani kila anapochagua masuala ya uswahiba yanapata uzito kuliko utendaji kazi wa mtu.
 
Ili kuitengenezea mazingira mazuri na bila kuhusisha makada wa chama, kwa miaka miwili post hiyo ikaliwe na TX kutoka nje - ikiwezekana apendekezwe na vyombo kama Transparency International. Huyu aweke misingi mizuri, afanye capacity building etc.
 
Mwinyi akiwa rais, siku moja alimuaigiza malecela kuwa anataka kuona viongozi wapya wenye asili ya kiisilamu wakipewa nafasi za uongozi, muungwana wakati huu alikuwa Tunduru, ambako alikuwa amepewa adhabu ya kwenda huko na bosi wake CCM Dododma, Mwakawago aliyekuwa akimchukia sana,

katika uho mkumbo malecela aliwapromote, Dr. Mtulia, Makamba, na muungwana kuja kuwa waziri mdogo.

Toka lini Rais anaagiza Waziri Mkuu ateua mawaziri? Na kama imeanza wakati mimi sijui, kwa nini Mwinyi asingewateua yeye mwenyewe bila ya kumwambia Malecela kwamba "anataka kuona viongozi wapya wenye asili ya kiisilamu..."?

Na huyo Mwinyi hata kama angekuwa mdini vipi, hakuogopa kumwambia waziwazi Waziri Mkuu ambaye ni Mkristo kwamba "anataka kuona viongozi wapya wenye asili ya kiisilamu..."?

Halafu huyo Dr. Idrisa Mtulia asingestahili kupewa uongozi pasipo dini yake? Unamdhalilisha huyu Mheshimiwa bure, ndugu.

Huoni, FMES, kwamba hivyo ulivyovisema havileti mantiki ?
 
Hosea amefanya kile alichoweza kufanya na tumshukuru kwa hilo na atakumbukwa kwa mchango wake huo, sipendi niingie ktk dhambi ya kumhukumu maana uteuzi wake pale ulitegemea imani ya mkuu wa nchi kwake na kama atatengua ni yeye pia.

Ni mchapa kazi hodari, mtu wa watu na zaidi ni mtanzania aliyeelimika vizuri, mungu atampatia fursa ingine ya kututumikia kwa ufanisi zaidi.

Nafasi za kiteule na zenye masikio ya umma si za kushindania wala kushabikiwa,

kumbukeni maneno ya mahita wakuluu........

Mzamivu hosea, songa mbele utafanikiwa tu, chapa kazi mpaka dakika ya mwisho..........

Daima mungu ni mwema mkurugenzi hosea

Kwakweli ndugu yangu hata kama ni uhuru wa maoni, wewe mwenzetu mbona unatupotosha???sina neno zuri sana la kuyapima maoni yako zaidi ya kusema kuwa kwa hili mwenzetu umekuwa ''low''.

1.Tumshukuru dr.hosea kwa lipi?na tutamkumbuka kwa lipi jema alilotutendea watanzania?Hivi kama alishindwa kubaini ukiukwaji wa sheria ya manunuzi yaani bado tu wewe unataka tumshukuru?taarifa yake ilisema wazi wazi kuwa hakukuwa na ukiukwaji wowote wa sheria, taratibu na kanuni!kitu ambacho kilibainika kuwa sio kweli.Kwa kweli tutamkumbuka kwa mabaya yake hususani kwa kuupamba ufisadi na mafisadi.Kama alikuwa ameshinikizwa na mafisadi kwanini asijiuzulu kuliko kujiaibisha,na kwakweli hosea amejiaibisha aibu mbaya ambayo itaendelea kumuandama hata akistaafu au kustaafishwa.Hawezi kuaminiwa tena huyo!

2.Hosea si mchapakazi na wala si mtu wa watu kama unavyodai,labda utuambie kuwa ni mtu wako!hata yeye mwenyewe analijua hilo kwamba sasahivi kwamba status yake mbele ya watanzania imeshuka mno!Eti nini kuelimika!hiyo elimu aliyoipata imewasaidiaje watanzania?ndio kusema kuwa yeye ndio mtanzania pekee aliyepea katika elimu?mbona unapenda dhihaka wewe.

3.Nani asiyemjua mahita kuwa alikuwa ni kibaraka wa ccm na alishindwa kutekeleza majukumu yake kikamilifu kama alivyotakiwa?hivi mara hii umesahau matukio ya ujambazi majumbani mwa watu na katika taasisi za fedha?watu tulikuwa tunaishi kwa mashaka ndani ya nchi yetu as if hakuna serikali!
kwahili mwenzetu nadhani umetumwa umsafishe hosea ambaye hasafishiki, vinginevyo utakuwa unajituma ili akuone.Maana fedha ya RICHMOND inatembea sana sasahivi inaweza kukufikia.
 
Mimi nashauri Mheshimiwa Presidaa afanye kama vile kakosea na kumteua Mwanakijiji...Kama ni record ya Ujeshi sii alikwenda JKT au haitoshi!
Nadhani ni wakati wa kuwakabidhi JF kama alivyofanya kwa Zitto na kamati ya madini!
MMM mwanakijiji na rushwa. namashaka kwa sababu ukiona mtu wa bongo akipingapinga ujue kwa sababu amekosa akipata mchungu huyo.Tuthibitishie mwana kijiji nikupendekeze throgh mjomba makamba
 
Philimone...Mwalim sio "barometer" ya kuwapima viongozi...mwalim kuna viongozi wengi tu hakuwataka...lkn hio sio sababu ya kuwa walikuwa wachafu...hakumtaka Malecela..was he right...mifano ipo mingi tu!!!


..hatuongelei barometer hapa...lakini huwezi kusema rais ambaye katawala miaka 23 ...alishindwa kumpa jk hata ukuu wa wilaya..yet unataka kumfananisha kikwete na malecela ...YOU ARE A JOKE!!!..malecela anayo historia nchi hii...hakukaa kwenye cheo cha ukatibu wa chama wilaya miaka 15!!.....malecela alipanda vyeo haraka haraka kwa kuwa alikuwa na uwezo...mwalimu alimuamini na kumpa foreign ministry ..wa kwanza ...[kabla wizara hii ilikuwa state house]...akiwa kijana mdogo..kama alikuja kutofautiana naye ilikuwa badaye....wakati huo kikwete alikuwa akiadhibiwa ovyo kupelekwa mikoani kwa ajili ya ufuska......wenzake alioajiriwa nao kina ditopile ,lowassa na wengine walishapandishwa vyeo na kupewa kazi za kueleweka.....

kubalini tu kuwa kikwete amepanda hapa karibuni tu....hakuwa amepikwa akapikika.....nadhani angekuwa ameingia kwenye active posts kwa muda wa kutosha ....ingetosha kumjua vema...tabia zake zilizojificha za uzembe.....

thats why kuna haja ya kumuangalia na kumchambua KIKWETE HALISI WA MIAKA YA 1976 HADI 1988.....kutakuwa na mambo ya ajabu hapo!!!
 
Mimo nashangaa hiyo CV imeishia 1988. Kumbukumbu zangu zinaionyesha kuwa jamaa alikuwa katibu wa chama atleast 1990. Huo ni wakati mafuriko yalipotokea masasi na Mwinyi alitembelea huko mpaka mwandishi wake Halahala (RIP) alipata ajali ya kukatwa na panga la helikopita ya rais. Kama kupata uwaziri then inawezekana kabisa jamaa aliupata wakati wa Malecela na siyo Warioba kwa sababu Warioba hakuwa waziri mkuu baada ya uchaguzi wa 1990. Vilevile inawezekana kabisa Mwinyi alikutana naye that time alipotemebelea kule. Pamoja na hayo mwinyi lazima alimfahamu kwa vile alikuwa ni member wa NEC, may be hakujua uwezo wake.

Lakini wa kumlaumu ni Mkapa kwa kumuweka pale ili amlinde.

Kuhusu DG wa PCCB kumbukeni vilevile zaidi ya Lilia Mashaka kuna D. Kihiyo palepale ambaye ni mtu wa usalama miaaka kibao.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom