Mary Chuwa
Senior Member
- Feb 24, 2011
- 177
- 40
Habari hii iliyopo katika gazeti la Mtanzania la Jumatatu machi 21,iliyoandaliwa na Shabani Matutu inasema.
Daktari wa dawa asili wa kituo cha Haleluya sanitarium,Issack Ndodi amewaponda wachungaji wanaodai dawa za Mchungaji Mwaisapile ni za Kishirikina.
Akizungumza na Tanzania Daima mwishoni mwa wiki nyumbani kwake maeneo ya Mbezi Juu,alisema tatizo la Askofu Zakaria kakobe na Mtume na Nabii wa kanisa la Efatha,Josephat Mwingira ni wivu wa kumuona mwenzao kapata dawa ya kutibu magonjwa sugu ambayo yalikuwa yameshindikana.
Kakobe na wenzake walitakiwa kusema Amina kwa watu kupona kuliko kuanza kuonesha wivu wao na kumtaka azuiliwe.
kitendo cha Kakobe kutaka kujua majibu ya Serikali kwa dawa hiyo inayotolewa kwa maombi haiwezekani kwa kuwa ina miujiza hivyo haiwezi kugunduliwa na vyombo vya kisayansi'' alisema.
Alisema walichopaswa kusema ni kwamba wale wanaopona ugonjwa huo wawe wanatoa ushuhuda kwa kuonesha kipimo chao cha kwanza kinaonesha wameathirika na baadaye waoneshe baada ya kunywa kikombe na kupona.
Kauli kama hiyo ilitolewa na Mhubiri Antony Lusekelo maarufu kama Mzee wa Upako aliyesema kuwa dawa isiwekewe kipingamizi kwani Mungu ana Nguvu ;na anaweza kufikisha ujumbe kwa mtu asiyetegemewa.
Daktari wa dawa asili wa kituo cha Haleluya sanitarium,Issack Ndodi amewaponda wachungaji wanaodai dawa za Mchungaji Mwaisapile ni za Kishirikina.
Akizungumza na Tanzania Daima mwishoni mwa wiki nyumbani kwake maeneo ya Mbezi Juu,alisema tatizo la Askofu Zakaria kakobe na Mtume na Nabii wa kanisa la Efatha,Josephat Mwingira ni wivu wa kumuona mwenzao kapata dawa ya kutibu magonjwa sugu ambayo yalikuwa yameshindikana.
Kakobe na wenzake walitakiwa kusema Amina kwa watu kupona kuliko kuanza kuonesha wivu wao na kumtaka azuiliwe.
kitendo cha Kakobe kutaka kujua majibu ya Serikali kwa dawa hiyo inayotolewa kwa maombi haiwezekani kwa kuwa ina miujiza hivyo haiwezi kugunduliwa na vyombo vya kisayansi'' alisema.
Alisema walichopaswa kusema ni kwamba wale wanaopona ugonjwa huo wawe wanatoa ushuhuda kwa kuonesha kipimo chao cha kwanza kinaonesha wameathirika na baadaye waoneshe baada ya kunywa kikombe na kupona.
Kauli kama hiyo ilitolewa na Mhubiri Antony Lusekelo maarufu kama Mzee wa Upako aliyesema kuwa dawa isiwekewe kipingamizi kwani Mungu ana Nguvu ;na anaweza kufikisha ujumbe kwa mtu asiyetegemewa.