flulanga
JF-Expert Member
- Jul 1, 2016
- 4,861
- 6,342
Dah unaweza kulia aiseeUPDATES....
Habari ndugu zangu JF...
Jumapili tulivu nikitokea church hapa misa ya kwanza kabisa...niliwahi na huyu mwanangu mdogo...nikasahau kumchapa pampers mana niliamka na mzuka wa kazi nikamwambia dada wa kazi aniandalie nguo tu na maji
Ntamuogesha mwenyewe nk ...kanikojolea usingizin church mpaka nimeishiwa pozi ase...hahaha ila burudani alipoamka kakaza sura namwambia umejikojolea kakana kwa sauti huku kanuna sijakojoa mimi...
Back to the topic...
Wakuu mimi ni mwanadamu na pia nina mengi kujifunza katika hili na nakiri kwa asilimia kubwa sana kubwa sana ushauri wenu umenisaidia sana tena sana kukubaliana na ukweli maana amini nawaambia tunaweza tukasema yote ila naamini kuna wengi mmenitangulia na ushauri mnaotoa ni from vivid life example...
Kuna mda week hii ninawaZa hivi labda aliteleza sijui (kutokana week hii namuona kakosa amani anajitahid kuniongelesha n.k na hata kutuma mesej za kawaida namjibu short tu mana tangu nimemblock whatsapp ni tabu)..ila nikikumbuka wadau ushauri wenu humu kwamba haya mambo yapo nisijitie kipofu na mawazo basi kidume nasali tu Mungu naomba nimalize salama hili natafuta zangu usingizi sebleni mdo mdo...
Anajua navyopenda mpira na huwa na enjoy sana kucheki boli indoor afu dak ya 80 huwa ndo natoka kuumalizia maeneo na washikaji...sasa safar hii boli kuanzia preview analysis linanikutia nje...jana mchana nilitoka kwenda kuchek la man u...nikarud nikapita saloon kunyoa nivorud nikamkuta nikasalimia nikapitiliza bafuni nikaoga nikajiandaa nikatoka mapema tena nikamwambia naenda mpirani(game la liver)
Nimetoka tu akanipigia mbona mechi bado haijaanza naona hapa ndo kwanza wana discuss..nikajibu tu nataka kubeti nasikiliza watabir !akashangaa!tangu lini nikamjibu badae kidog nikakata(yani inshort sasa hivi tangu nimeanza kukubaliana na hali halisi najihisi moyo unapumua vizur na najitahid kumuepuka sana...
Mlitoa ushauri wa kuwa makini naweza hata tiliwa sumu wadau mimi nimuoga sana wakutangulia kizembe ni waache wanangu...bas sikuiz jion nabeba kitu namwambia dada anipike chap nikirejea au nakaangiza mwenyew...
Maamuzi niliyofikia ni kwamba krismas hii ntamrudisha kwao...nimeshaongea na pande zote mbili la msingi sitotaka familia upande zote mbili sishauri tuvumiliane wakati mwanamke katamka sana tuachane...
Nafanya hivyo kuka na familia kwasababu wakuu nilioa huyu bint kihaki kabisa nilikabidhiwa kabisa ntamtudisha kama hivyo kiungwana.
ILA... Sitaki wanangu awachukue.
Nataka atoke aende zake na kila kitu akitakacho ntampa ila sio watoto(hata nyumba akijiwehua kulopoka mana akili zake anazijua mwenyew kwa sas)...
Mimi ndo last born kwetu nina kaka zangu wawili
Mama alifariki nikiwa na miaka minne tu..mzee wangu alishauriwa sana aor aligoma kwakutuonea huruma bado wadogo esp mimi...na hakuoa mpaka anafariki...aliniambiaga kitu utakapo maliza shule ndo ntaoa(alikua na mpenz wake tunamuita mamdogo kwemye family gathering walikua pamoja nk ila hakuwahi kulala nyumbani nadhan walikuwa wanahook up kwa mamdogo )i was too young to analyse ila kaka zangu ndo niliwasikia wakiwa wana anyicipate scenerio zote...
Nilipoanza kaz mwaka wangu wa kwanza kazini natimiza ndo nikapata mchumba huyu mzee akaandika barua ilatukatoa mahali nk akafariki...
Ila he was very happy mana alisema adi wewe unaoa mie sijaoa ase kweli sasa kazi yangu duniani imeisha nikapumzike na mwenzangu peponi (utani utani kweli )
Nasema haya namini wanangu ntawalea vizuri sana Mungu atanipigania hili na hata marehem baba yangu alipo atafutahi na kuamini i am everything like him as i wished when it comes to being aparent.
back to the topic
Huyu sas hivi naona anajivisha sana ngozi ya kondoo sijui anaona maneno yake yanataka kutimia nk
Ila ndo nimeamua
Kama ananiona sifai kwa sasa aniache tu i will reach for the stars in Gods favor...
Yani nilianA kuzeeka najiona ase
Inabidi niji pimpu maana am very very on point ase...
Guys thanks alooot...
Mmefanya kazi ya Mungu
Na ndugu zangu tuliokutana PM
Mbarikiwe sana laMa tukeep intouch na mbarikiwe sana kwa moyo mmoja
Hamjanuangusha na kuniacha nipotee mlipohis nalegeza kamba.
Nikihisi sielewi taswira au nalegeza kamba ntawakimbilia mnipe muongozo