Priceless soul
JF-Expert Member
- Jul 4, 2017
- 1,484
- 1,727
Never give up on your family never.(children). But wife is NOT your blood relative.Habari wana JF wote kwa ujumla, bila ya kupoteza muda naomba kuja kwenye mada husika. Mimi ni kijana wa miaka 35,ndoa yanagu mpaka sasa inamiaka 5 tuu. Katika kipindi chote hichi tumeishi kwa furaha na upendo mkubwa tumebahatika kupata watoto 2.
Mke wangu ni mtumishi chuo kikuu(mwalimu)na mimi ni unga unga mwana pangu pakavu baada ya kampuni fulani ya mawasiliano niliyokua nafanya kazi kufungiwa na serikali kwa madai ya kukwepa kulipa na kuhujumu uchumi hivyo kesi bado iko mahakamani lakini sijawahi kukosa rizik japo kipato changu ni kidogo ila upendo na furaha viliendelea kushamiri.
KUANZA TATIZO
Mambo yalianza kua mabaya ktk ndoa yangu pale tuu mke wang alivyohamishwa kikazi na kuja hapa Dar ktk chuo kikuu fulani mwaka huu mwez 3 hivyo mimi niliendelea kubaki mkoni kwa lengo la kujipanga ili nihamie dar ili niwe karibu na familia yangu.
Ifahamike kua uhamisho wake haukua wa malipo kutokana na yy ndo aliomba kuhamishwa hivyo alipofika hapa Dar alifikia kwao maana yeye ni mzaliwa wa hapa dar.
Baada ya miezi 2 kupita mimi pia nikatoka mkoani na kuja hapa Dar,ila nilifikia nyumban kwetu kwa wazazi wangu (Mkuranga)
Harakaki za kutafuta nyumba zikaanza,kwa bahati mbaya wakati sijalipia nyumba nikafiwa na mzazi wangu(baba) chakushangaza mke wangu hakuweza kufika msibani kwa madai ya kukosa ruhusa kazini.
Sikua na neno maana bado nilikua kwenye majonzi,baada ya msiba kumalizika nilinza kujisikia homa kali na kulazwa hospitali,baada ya vipimo niligundulika ni Covid 19,
Mungu alisaidia nikaruhusiwa na kuendelea na matibabu nyumban. Wakati naendelea na matibabu mawasiliano na mke wangu yalikua ya tabu sana,simu za zilikua hazipaikan kwa madai mtoto wetu mdogo ameharibu simu yake hivyo ilinibidi niwe namtafuta mama mkwe kuongea na mke wangu
Hali ya kimawasiliano ilizidi kua mbaya zaid kadri siku zinavyozidi kusonga mbele,akawa hanitafuti,mpaka mimi nimtafute yeye, upendo wake kwangu ulikua umepungua sana kwangu. Maana hata kunijulia hali imekua vigumu kwake. Kibaya zaid alinza kufuta account namba yake ya wasapu na kuwa online kupitia Facebook nilivyomuuliza mbona nakuona online ushanunua simu nyingine?alinijibu kua ni ya ndugu yake wanaishi karibu pia namjua huyo mtu.
Nilimuomba namba ya simu anayoitumia ya huyo ndugu yake akanipa. Chaajabu sasa nikipiga ile namba anapokea muhusika wa ile simu na ananimbia yy yuko mbali kidogo na mke wangu.
Hii hali ilinishangaza sana kwan mda ambao nachat na mke wangu Facebook ndo mda huo nimepiga simu baada ya yy kunipa hiyo namba na kaniambia ndo anaitumia kwenye hiyo simu,
Niliendelea kuvumilia hii hali kwakua sikua na jinsi maana bado naendelea na matibabu. Hapa juzi kanitumia ujumbe kupitia Facebook anasema tuachane yy amechoka na maisha ya ndoa hivyo anahitaji kua single,haoni faida ya kua kwenye ndoa. Kwa kwel moyo wangu wote ulikua unawaka moto kwa maumivi makari sana
Kwakua bado naumwa halafu nakutana na changamoto kama hii. Ilinibidi nimtafute kwa kumpigia simu kupitia kwa mama ake akampa simu nikaongea nae.
Nilimuuliza kwan kipi kibaya ambacho nimekufanyia mpaka umefikia maamuz hayo ya kutaka tuachane?alinijibua kua yy amechoka na kudharauliwa hapo kwao maana inaonekama kama mimi nimemdamp tuu hapo kwao,
Nilimuuliza kwan hujui hali yangu ya kiafya kwasasa? Akanijibu kua anajua ila hayo ndo maamuzi aliyaamua kwan kichwa chake hakiko sawa,pia kazin kwake pia hajapandishwa mshahara hivyo hayuko sawa. Baada ya kuniambia hiyo alinikatia simu.
Ifahamike kua kipindi hiki chote ninachoumwa kaja kuniona mara moja tuu mpaka sasa ni mwez umekata hajaja kuniona.
Na mda huu yuko likizo haend kazin.
Naombeni ushauri wenu na mawazao nini nifanye kuinusuru ndoa yangu?hali yangu kiafya bado haija kaa sawa.ndoa inazidi kuniumiza msaada wenu tafadhali.
SO,akitaka kumuacha,onana nae (Ila pambania watoto wako wakue vzr),ili ujihakikishie sababu ya kuachana, alaf kubali kuwa mjinga muachane officially ili asijekusababishia matatizo makubwa mbelen ukapata kilema cha maisha.
#kuna baadhi ya mafanikio maishani, Mungu hawezi kuyaruhus mpk awatoe watu watakao kuangusha tena.
#Ndio pale unaona unatafuta na mtu ila kabla hamjaanza kufurahia maisha,anakata tamaa na anakusaliti na unakosa nguvu ya kuendelea kushirikiana nae,ila baada ya kuachana nae officially,Ndio mafanikio makubwa yanajirud,na hapo HUPASWI KUMRUDIA HATA WAKIJA WAZEE WA KANISA AU MSIKITI(Maana Mungu alikutenga nae kwasababu).
#