Amanikullaya
JF-Expert Member
- Mar 26, 2017
- 1,237
- 1,666
Ukweli nimechoka nahitaji kusafiri mbali na nyumbani kwangu kila mtu aishi maisha yake maana tunakaa muda wote kama mtu na mke mwenza.
Ndoa yangu ina miaka 5 tuna watoto 2. Nilikuwa nafanya Biashara vizuri nikafanikiwa kujenga nyumba ya Familia na kumfungulia wife biashara naye ili asinitegemee kila kitu.
Bahati mbaya biashara yangu ikayumba nikawa nakomaa nayo ila yeye muda wote ni kunikatisha tamaa niachane nayo.
Nikapata dharura ya kusafiri kwanda mkoani kwa wazazi nikamwacha kijana.
Huku nyuma wife akamsonga songa kijana mwisho Biashara yangu ikafugwa nikapigiwa simu na wife kijana anaingiza hasara nimefunga.
Niliporejea home uzi ni ule ule anataka niachane nayo. Kweli nikaamua kuachana nayo kwani kodi ya pango iliisha na pia palifugwa wateja wangekuwa wametuhama zaidi hivyo nikilazimisha naweza tengeneza hasara na madeni
nikahitimisha kufunga Rasmi.
Niko zangu home najipanga kutafuta mishe ya kufanya wife ndiye mwenye kazi ndiye kila kitu kinacho husiana na hela. Manyanyaso yakaanzia hapa,
kelele, kupangiwa anachotaka.
Jumamosi ya ngao jamii kati ya Simba na Yanga niliomba Elfu mbili tu nikakae kwenye kibanda umiza niangalie mechi nilitolewa nje.
Siku hiyo nilishinda home kuna kazi nilikuwa nafanya. Nilichoka kweli,
basi nikajirudia zangu home saa 18:00 kujilalia saa tatu na nusu akawa anaingia. Alipofika akanyosha moja kwa moja kitandani. Nikauliza “wife hupiki?” maana njaa inauma. Akasema sipiki na sijakununulia chochote tutakula kesho. Kila nikimwongelesha kimya basi kuepusha shari nikakaa kimya nikalala japo usingizi wa tabu uchovu + njaa + mawazo
Kuanzia siku hiyo ni kununiwa hakuna kusemeshana. Nimewaza niuze nyumba nipate mtaji naona ugumu biashara zikigoma.
Wazo langu kwa sasa kwa sababu sina thamani kwake niondoke nikatafute maisha mbali ata miaka 10 ili nipate amani na faraja. Nahofia nitakufa bure na mawazo naye abaki na amani yake anilelee tu wanangu.
Ndoa yangu ina miaka 5 tuna watoto 2. Nilikuwa nafanya Biashara vizuri nikafanikiwa kujenga nyumba ya Familia na kumfungulia wife biashara naye ili asinitegemee kila kitu.
Bahati mbaya biashara yangu ikayumba nikawa nakomaa nayo ila yeye muda wote ni kunikatisha tamaa niachane nayo.
Nikapata dharura ya kusafiri kwanda mkoani kwa wazazi nikamwacha kijana.
Huku nyuma wife akamsonga songa kijana mwisho Biashara yangu ikafugwa nikapigiwa simu na wife kijana anaingiza hasara nimefunga.
Niliporejea home uzi ni ule ule anataka niachane nayo. Kweli nikaamua kuachana nayo kwani kodi ya pango iliisha na pia palifugwa wateja wangekuwa wametuhama zaidi hivyo nikilazimisha naweza tengeneza hasara na madeni
nikahitimisha kufunga Rasmi.
Niko zangu home najipanga kutafuta mishe ya kufanya wife ndiye mwenye kazi ndiye kila kitu kinacho husiana na hela. Manyanyaso yakaanzia hapa,
kelele, kupangiwa anachotaka.
Jumamosi ya ngao jamii kati ya Simba na Yanga niliomba Elfu mbili tu nikakae kwenye kibanda umiza niangalie mechi nilitolewa nje.
Siku hiyo nilishinda home kuna kazi nilikuwa nafanya. Nilichoka kweli,
basi nikajirudia zangu home saa 18:00 kujilalia saa tatu na nusu akawa anaingia. Alipofika akanyosha moja kwa moja kitandani. Nikauliza “wife hupiki?” maana njaa inauma. Akasema sipiki na sijakununulia chochote tutakula kesho. Kila nikimwongelesha kimya basi kuepusha shari nikakaa kimya nikalala japo usingizi wa tabu uchovu + njaa + mawazo
Kuanzia siku hiyo ni kununiwa hakuna kusemeshana. Nimewaza niuze nyumba nipate mtaji naona ugumu biashara zikigoma.
Wazo langu kwa sasa kwa sababu sina thamani kwake niondoke nikatafute maisha mbali ata miaka 10 ili nipate amani na faraja. Nahofia nitakufa bure na mawazo naye abaki na amani yake anilelee tu wanangu.