Expensive life
JF-Expert Member
- May 2, 2020
- 1,691
- 5,451
Iko hivi, hili tukio limetokea hapa ninapoishi, jamaa akiwa amekaa zake ndani amepumzika na mihangaiko ya hapa na pale, mkewe na majirani wenzie wapo nje kibarazani wakipiga stori.
Katika stori zao wakaanza kumsema mke wa jamaa kuwa huyu mtoto baba yake ni nani? Mbona hawajafanana hata ukucha na baba yake? Mke wa jamaa akabaki anachekacheka tu.
Jamaa baada ya kusikia hivyo katoka kafura na kuondoka pasipo kuaga siku ya tatu hajatokea nyumbani, baada ya kurudi nyumbani ugomvi mkubwa baina yake na mkewe.
Tumejaribu kumuweka sawa kuwa ule ulikuwa ni utani tu jamaa kaweka ngumu, kesi ni kubwa jamaa anataka DNA.
Nb: Kwa dunia ya sasa uhaminifu ni sifuri hawa viumbe wanatupiga sana, nakumbuka kipindi wife alipojifungua, mama alikuja akamcheki mtoto akasema yes hii ni damu yetu.
Katika stori zao wakaanza kumsema mke wa jamaa kuwa huyu mtoto baba yake ni nani? Mbona hawajafanana hata ukucha na baba yake? Mke wa jamaa akabaki anachekacheka tu.
Jamaa baada ya kusikia hivyo katoka kafura na kuondoka pasipo kuaga siku ya tatu hajatokea nyumbani, baada ya kurudi nyumbani ugomvi mkubwa baina yake na mkewe.
Tumejaribu kumuweka sawa kuwa ule ulikuwa ni utani tu jamaa kaweka ngumu, kesi ni kubwa jamaa anataka DNA.
Nb: Kwa dunia ya sasa uhaminifu ni sifuri hawa viumbe wanatupiga sana, nakumbuka kipindi wife alipojifungua, mama alikuja akamcheki mtoto akasema yes hii ni damu yetu.