Ndoa ya Kanye West na Kim Kardashian inakimbilia kwenye talaka

Numbisa

JF-Expert Member
Dec 12, 2016
268,184
1,095,278
135830611_1016422382185135_1466802099593661078_n.jpg


Ndoa ya Kanye West na Kim Kardashian yapumulia mashine na kutaka kutalakiana. Kwa mujibu wa media za Marekani kwa muda Sasa ndoa yao Haina afya nzuri na ilidhoofu kwa kiasi kikubwa mwaka 2020 ambapo mastaa hao wamekuwa wakiishi Kila mtu kwake huku Kim akiwa na watoto

Kwa mujibu wa taarifa Kim hasa ndie anataka waachane baada ya mambo kumshinda ila anataka waachane kwa amani sio migogoro kwani wameshajaribu kwenda mapumzikoni pamoja na hata kwenda kupata ushauri maalum kuipa afya ndoa yao lakini mambo ndio yameonekana kutibuka zaidi Kim tayari ameripotiwa kumchukua mwanamama Laura ambaye Ni mwanasheria maarufu wa migogoro ya mastaa ili aweze kumsaidia suala hilo kuimaliza ndoa kwa amani
 
Back
Top Bottom