Zogwale
JF-Expert Member
- Jul 10, 2008
- 15,287
- 10,842
Nilisimamia ndoa ambayo imedumu kwa miaka 15 kwa sasa. Ni ndoa njema na sikivu. Tatizo kubwa ambalo nimekuwa nikilipata kama msimamizi wa ndoa ile ni kutoridhishana katika tendo la ndoa. Mke huwa yuko down sana kimapenzi, na si kwamba ana bwana nje, bali ni kwamba huwa akiwa katika tendo la ndoa akishamaliza round moja basi anapoa kabisa na hataki tena kabisa kuendelea. Na hapa itamchukua muda mrefu (wiki na kuendelea) ndipo awe tena na hashiki/tamaa ya tendo la ndoa. Kitendo hiki kinamuumiza sana mume na kunakuwa na kutoelewana kwa jambo hilo. Nimesuluhisha, na mke anasikitika sana kwa hali yake hiyo. Wamepata ushauri lakini kila akijaribu bado tatizo liko pale pale.
Nimeona hapa jamvini tunashirikishana matatizo na kupata ushauri. Nakaribisha ushauri mwema na wenye nidhamu ili kumsaidia hawa ndugu waweze kuishi maisha mema, ya upendo kwa ndoa yao na pia kuweza kuwasaidia wengine hapa au ndugu na marafiki zetu ambao wana tatizo hili. Asanteni.
Nimeona hapa jamvini tunashirikishana matatizo na kupata ushauri. Nakaribisha ushauri mwema na wenye nidhamu ili kumsaidia hawa ndugu waweze kuishi maisha mema, ya upendo kwa ndoa yao na pia kuweza kuwasaidia wengine hapa au ndugu na marafiki zetu ambao wana tatizo hili. Asanteni.