Najiuliza sana.......maana ya ndoa ni kupata watoto?,kuna tatizo kubwa sana sasa ivi hapa kwetu , wanandoa wengi huwa wanachanganyikiwa sana wakichelewa kupata watoto.....imepelekea mpaka baadhi ya kina dada wanatokanje ya ndoa kubeba mimba na mwanaume mwingine kwa siri ili?....... ,eti kuokoa ndoa. ...Ni kweli ndoa inapendeza zaidi mkijaliwa watoto na hata mimi ningechanganyikiwa zaidi kama nisingepata watoto kwenye ndoa........ni swali najiuliza sana kwa nini tunachanganyikiwa sana kama tunachelewa au hatupati watoto baada ya kufunga ndoa. Na pia swali lingine gumu sana najiuliza je, kama ndoa ingekua ni watoto, kungekua na ulazima wa kuoa kweli? si tungezaliana tu kama mbuzi na ngo'mbe?....Najiuliza sana.