Angalia hizo red halafu zingatia mahojiano yetu kwenye thread ya MS na yako ya Maandamano:
1. Leo unakiri kuwa hili ni suala la IBADA ZENU. Kwa hiyo nafikiri sasa umeshaelewa kuwa lina tofauti na huduma za jamii kwa hiyo ni jambo binafsi na halihitaji ushiriki wa wasio wa ibada hizo kwa hali wala mali. (Asante)
2.Hukumu ya Allah! Ukimaanisha kuwa Allah ametoa mwongozo na naamini ndani ya Quran kitakuwepo kifungu kinachoelezea nini adhabu ya mtu asiyefuata maagizo ya Allah. Kwa hiyo hapa nachoona ni kuwa hakuna haja ya mtu kujifanya kuwa yeye ni zaidi ya Allah, kiasi atoe adhabu kwa watu kwa niaba ya Allah ilhali ukamilifu wa nafsi yake hauna uhakika.
3. Unataka kuniambia kuwa, hata baada ya kuundwa kwa mahakama ya kadhi bado litakuwa ni chaguo la mtu kupeleka mambo yake kwa kadhi au mahakama ya sheria. Sasa juzi ulisema unataka mahakama ya kadhi itambulike kikatiba na ipewe nguvu ya kisheria ya kuenforce hukumu itakazozitoa. What if marehemu alitaka mambo yake yazungumziwe kwa kadhi lkn mjane hataki, mtamwacha mjane aende LC au ndio zitatumika zile nguvu ulizokuwa unazipigia debe kumlazimisha?
4. Unasema unafikiri swala la imani hakuna kulazimishana, Then what is the concept of having a Kadhi court for?
Mimi nachokiona hapa, unam-sweettalk BR kwa kuwa kaja na hoja za msingi. Ni unafiki kuyageuka yote uliyoyasema juzi kwa kuogopa kujibu hoja na hiyo ni daili kuwa hujui unachozungumza. Mrejee aliyekutuma mwambie umeshindwa kazi.
Ukiacha dharau na kijeli tunaweza kufanya mjadala
Lakini bado una hasira na waislamu wamekufanya nini?? au mafundisho yako ndio yamekufanya uwe na hasira hivyo
Calm down sema shida yako tujadili..hunijui sikujui, hunilishi sikulishi ok..