Black Rose
JF-Expert Member
- Nov 21, 2011
- 243
- 171
Kama ni hivyo basi Waislam watanzisha hiyo Mahakama ya Kadhi na wala hawata tegemea hela za hao wavuja jasho na hao makafiri, katika hii dunia Waislam ni matajiri sana ukiangalia wewe huko Uarabuni kuna nini kama sio Mafuta? na hayo mafuta ndio yanayoendesha hii dunia ya sasa bila Mafuta hakuna
viwanda wala magari wala mashine wala hakuna kitu kitakachokwenda wakianzisha hiyo mahakama ya kadhi waislam wa Tanzania watapata misaada toka kwa wafadhili toka nje IRAN,SAUDIA ARABIA na nchi nyingine nyingi za kiislam upo pamoja na mimi?
Usinchekeshe!
Ina maana waislam watanzania wao hawajiwezi hadi kuchangiwa? Hebu usituangushe.
Mtumai cha ndugu si hufa maskini?Mahakama ya kadhi tunachoionea mashaka ni kama itaweza kumaliza matatizo ya "kifikra' kwa wanaume wa kiislam hasa kwenye Ndoa.Huu umaskini uliokithiri utamalizwa vipi na hii mahakama? Tatizo ni umaskini wa fikra na mapato unaochangia wanawake wa kiislam kunyanyasika.Salma2015 kauliza maswali ya msingi na hakuna hata mmoja kaweza kujibu hizo hoja.Wanawake wa kiislam hawana tatizo na maagizo ya Kuran au ya Mtume.Wasiwasi ni utendaji kuanzia waumin wenyewe hadi watakaosimamia hizo mahakama.Enyi wanaume, mjue mnatuharibia ibada zetu kwa tabia zenu.Mnalazimisha wanawake wawe na tabia zisizoendana na Uislam kwa vile nyie hamtimizi maagizo.Mnabebesha wanawake mizigo mizito ya "hasira, wivu, chuki" ukiacha mingine ya familia . For you the intellectuals I would confidently say that
Ndoa kwenye uislam ni ibada.Allah kamuumba "mwanamke" kwa "mwanaume" waishi kwenye ndoa kwa lengo la kuwepo amani, utulivu, raha na faraja.Hivyo basi ndoa inatakiwa izae AMANI NA RAHA.Hii itawezekana kupatikana kama tu wote wanatimiziana wajibu unaowapasa vinginevyo kutakuwa na magomvi yatakayoharibu amani, utulivuna hatimaye kuharibu ndoa (Rejea Kur.30.21).Wanaume mmepewa onyo mkaambia Muogopeni Allah kwa jinsi mtakavyoshi na wake zenu, kwa sababu mumewaoa kwa trust ya Allah! Sasa kama nyie hata hili Onyo hamlizingatii, mnaweza kuwa na uhalali kudai mahakama ya Kadhi ili ati iwaamulie mambo ya ndoa?
Haya hili la Polygamy nalo ni suala lenye utata.Uislam umeweka msisistizo mkubwa kwa haki za watu - mume –mke, na pia zile za Muumba.Kufuatana na Uislam,mke ni life partner and not a robot or husband's property that can be put out of commission or replaced at any time without any consideration, concern, shame or feelings!Uislam haumpi mwanaume yeyote yule a right to have more than one wife nor considers it is an act of piety.
Mtume mwenyewe alikuwa na mke mmoja tu for about twenty five years kabla ya kuoa wengine,na alimuoa huyu mke akimzidi mtume kwa miaka 15 years.Pigeni mahesabu ndipo mtambue "tamaa" haikuwa sababu ya msingi ya Mtume kuoa zaidi ya Bi Khadija. Hivyo basi kinyume na wanavyodhania wanaume wengi wa kiislam, monogamy is a norm and polygamy a rare exception in Islam. Kuhusisha dini na polygamy ni upotoshaji wa makusudi wa wale wenye kueneza huo utaratibu wa kuoa wake wengi.
Dini ya Kiislam ni dini ya haki kwa wote na siyo a smoke screen to deceive anyone and or hide behind it to protect personal desires or lust. Wanaume wengi wa Kiislam wanajitafutia uhalali wa vitendo vyao kwa kutumia verses za Kuraan conveniently and selectively bila kusoma ayah kamili na kuwa na uelewa wa kutosha. Ayah inayozungumzia kuoa zaidi ya mke mmoja ina context na imeelezwa uzuri kabisa: Marrying more than one wife was revealed after a battle in which many Muslim men were killed leaving behind helpless widows and orphans. The entire ayah (verse) of Surah (chapter) An-Nisa (The women 4:3), where Allaah The Almighty says; "And if you fear that you shall not be able to deal justly with the orphan-girls, then marry other women of your choice, two or three, or four, but if you fear that you shall not be able to deal justly with them, then (marry) only one……."
Sasa nyie wanaume wa Tanzania, miaka hii mna sababu gani zaidi ya tamaa zenu kuoa zaidi ya mke mmoja?