Kwenye ndoa kuna vibweka sana,ndoa ikiwa haina mtoto utasikia ooh ndoa haijajibu,mara mwanaume hajui shughuli,mara mawifi nao wanakuja juu wakidai wifi yao mgumba,mara mashemeji nao wanakuja juu wakidai shemeji yao hana uwezo wa kumpa ujauzito dada yao mara ndoa pwaaaaa!!!!Upande wa pili nako vituko,ndoa ikipata mtoto,utasikia mume analalama mkewe hamjali anamjali mtoto tu,kesho jamaa analalama mkewe kawa mchafu anuka maziwa ya mtoto masaa 24,mara ndani hapasafishwi minguo ya mtoto imezagaa mpaka bafuni,jamaa anaamua kutafuta kipozeo nje,mama mtoto anagundua mara ndoa pwaaaaa!!!!KIPI NI KIZURI????