Nje ya box
JF-Expert Member
- Apr 11, 2012
- 241
- 251
Duh unashangaa nini, mambo uliyoandika hapa unaonekana kabisa wewe ni mkosaji
Mkubwa kwenye hii ndoq japo umemlaumu mke wako. Mpaka mke wako anasema yeye na mama ni wake wenza basi inaonekana hii ndoa imeshikiliwa na mama yako, tena ingekuwa mimi ningekuambia namuachia kitanda mama yako. Tafuta source nini Lkn kwa jinsi ulivyoandika inaonekana una
Makosa mengi kushinda mke wako.
Na kwanini wao wakae kwa wakwe?bora arudi kwao maana naona kama mwanamme ndoa imekushinda.
Sisi wakristo kuna maandiko kwenye biblia kuwa mume and mke wataacha wazazi/ familia zako na kuungana kama kitu kimoja
Mkubwa kwenye hii ndoq japo umemlaumu mke wako. Mpaka mke wako anasema yeye na mama ni wake wenza basi inaonekana hii ndoa imeshikiliwa na mama yako, tena ingekuwa mimi ningekuambia namuachia kitanda mama yako. Tafuta source nini Lkn kwa jinsi ulivyoandika inaonekana una
Makosa mengi kushinda mke wako.
Na kwanini wao wakae kwa wakwe?bora arudi kwao maana naona kama mwanamme ndoa imekushinda.
Sisi wakristo kuna maandiko kwenye biblia kuwa mume and mke wataacha wazazi/ familia zako na kuungana kama kitu kimoja
DuhHabari za Jumapili wapendwa
Hivi kunapotokea mgogoro baina ya wanandoa ambapo katika hiyo migogoro mke hapigwi wala hajatishiwa maisha,,baba mzaz wa mwanamke anaruhusiwa kwa utaratibu wa sheria ipi kunipeleka mahakaman mimi mume?
Pili baba mkwe anapomuhitaji binti yao lakin hasemi waz lengo wa kumuhitaj bint yao kama anavunja ndoa kabisa ama ana nia ya kwenda kumkanya mtoto wao wakati huo huo tuna watoto wadogo ambapo mimi kama baba wa familia sina iman na mazingira ambayo wataenda kuishi wanangu,naweza kutumia utaratibu gan wa kisheria wa ama wamchukue binti yao bila ya watoto yaani nibaki na watoto ili ataporud awakute watoto huku ninakoishi hapo izingatiwe kuna mtoto wa mwaka mmoja na miezi miwili?
Kutokana na migogoro hiyo ambapo wife amekuwa akinitishia kuwa atanikomoa kwa njia yoyote na ushahidi ninao hivo nililazimika kumuacha nyumbani kwetu na mimi kuishi mbali nae,lakin kila wiki huwa naenda kuwajulia hali na kupeleka mahitaji ,je naweza kushitakiwa kwa kosa gani hapo?
Mke wangu alitoa kauli kwamba mama yangu mzaz na yey ni kama mtu na mke mwenza,je naweza kumshitak kwa matusi hayo?
Baba mkwe amenipigia simu na kunitishia kwamba atakuja kuchukua familia yangu,,je akifanya hivo na mimi nikazuia yey kuondoka na watoto, ntakuwa na kosa lolote kisheria?
Naomba niwatakie siku njema naomba mnishaur kwa upendo,pale nilipokosea au sijaeleweka niko tayar kutoa ufafanuzi pia matus ruksa