Boflo
JF-Expert Member
- Jan 20, 2010
- 4,384
- 4,409
Jemeni sasa huu mwaka mmoja na miezi 2 sasa nimo katika ndoa lakini mambo ninayokumbana nayo kwa kweli ni makubwa mno, yamenielemea. Nimeona bora nimwage mtama hapa jamvini ili wenye nia njema wanipe ushauri wa kufanya. Mwaka jana mwanzoni nilimuoa binti wa Kitanga anatoka Pangani.Siwezi kueleza yote lakini huyu mwanamke ana matarahambe sijapata kuona, kila nikijitahidi kumridhisha hatosheki, tukianza kugombana basi anapiga kelele mpaka majirani wote wanasikia, aibu tupu!! Kwa mfano mara nyingi yeye anapenda nimnunulie nyama ya kuku, Juzi nilipita Kisutu nikachukua kuku 4, kufika nao nyumbani, ananiambi eti kachoka kula nyama ya kuku, anatamani kula nyama ya kasuku, nilishtuka sana, nikamuuliza kama yuko serious, akaniambia hivyo ndivyo anavyotaka, nimejaribu kuulizia kasuku anauzwa bei gani, nimeambiwa mmoja ni laki mbili, hivi wadau mnanipa ushauri gani?? Huyu mke si wa kuachana naye!! Au kuna njia yoyote ya kufanya....