Ndoa ikifika hali hii mnakaribisha zinaa kama bado haijaingia

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,597
215,272
1605496728190.jpeg

Sababu mojawapo ni kumkosoa mwenza mbele za watu. Mkisha funga ndoa nyinyi ni mwili mmoja. Mume wako akichemka hadharani unaimeza aibu mpaka mfike chumbani ndiyo mnaongea. Mfano unajua mume wako Kimalkia hakipandi, akivunja mbele za watu meza.

Kumkumbatia mume wako asubuhi akiwa anakuaga ni muhimu. Kwa mila za Afrika ni ngumu kufanya haya kama mpo na wazazi au wakwe. Mkumbatie chumbani na busu hata akirudi kutoka kazini.

Jiepushe na marafiki wasio mkubali mke/mume wako. Maneno yao yatakua sumu katika penzi lenu.

Jifunze kuomba msamaha kwa mke/mume wako. Kiburi ni sumu ya mapenzi.

Kuwa muwazi kwa mwenza wako. Mfano Haya mambo ya kuja kufahamu ulizaa kabla ya ndoa mkiwa tayari kwenye ndoa yana leta hatari sana.

Wengine neno niache au tuachane limekaa mdomoni kila mkikwaruzana kidogo tu.

Kila ukipata nafasi weka manjonjo kwenye ndoa yenu. Hata kutumia weekend hotelini kubadilisha mazingira na kuwa na nafasi yenu.
 
Hayo hayawezekeni katika zama hizi ambapo mwanaume anaamini kitu pekee cha thamani kwa mwenza wake ni kumspoil kwa pesa,na mwanamke haoni uthamani wa mwanaume zaidi ya kuwa na pesa hasa penzi linapoanza.Sasa pale ulimbukeni huo unapoisha ndio utamu wa ndoa huanza.
 
Hayo hayawezekeni katika zama hizi ambapo mwanaume anaamini kitu pekee cha thamani kwa mwenza wake ni kumspoil kwa pesa,na mwanamke haoni uthamani wa mwanaume zaidi ya kuwa na pesa hasa penzi linapoanza.Sasa pale ulimbukeni huo unapoisha ndio utamu wa ndoa huanza.

Hii kweli kabisa, pesa ikiisha hapo ndio nafasi ya mambo kuanza kwenda mrama kwa wengi.
 
Na akitokea aliyetoka nje akakutana na mtu akamridhisha kuliko inavyokuwa katika ndoa!

Hatataka tena suluhu itakuwa ngumu sana kuirudisha hiyo ndoa pazuri.

Mwingine anataka suluhu, mwingine hataki!! Ushaona hiyo??
Tunasahau wa nje hufurahisha kwa sababu mnaonana kwa wizi

Cha wizi kitamu, nae mkioana mtakinai tu hatakuwa na aliyokuwa anakufanyia mlipokua wezi
 
Hasa uoe au uolewe na mtu ambaye ametoka kwenye familia ya kimasikini (ambao tuko wengi). Anawaza Mali mlizochuma tu.
Sio tu mlizochuma..hata zile ambazo alizikuta na hajui ulizipatapataje nazo atazitaka....na mshahara ako wote na nguvu zako zote na akili zako zote na muda ako wote...

Kazi yake kuu itakuwa kuteka na kuficha..inaweza kuwa unatumia muda mwingi na nguvu nyingi na akili nyingi kutafuta lakin hakionekani....mbaya kabisa hatajali Kama unavaa mtumba au la...

Acha kabisa wahindi waendelee na castle system yao...oa wa level ya kwenu au zaidi
 
Back
Top Bottom