Ndoa hizi zina matatizo sana

Sky Eclat

JF-Expert Member
Oct 17, 2012
57,589
215,187
Habari za leo waungwana,

Leo ni kali kuliko, huyu shost wa tangu boarding school, yale mambo ya kushare toothpaste na kuchanganya solution ili ulie mkate. Basi baada ya shule kila mtu aliendelea na ustaarabu wake, tumekutana mjini juzi tu na kubadilishana namba. Leo asubuhi dada yake ananipigia simu shost yuko Central Police Station.

Mkasa wenyewe ni hivi, shost ameolewa na amebahatika kupata watoto watatu, wa kiume wawil na wakike mmoja. Shost alihangaika sana kupata dada wa kumsaidia kazi, mama ofisini kwao akamletea binti kutoka mikoani, binti ni mzuri kaumbika, shost alimpeleka nyumbani na kumfahamisha taratibu za kazi.

Baada ya miezi mitatu kupita binti ameota mapembe ndani ya nyumba, shost akiagizi leo mchana chakula ni wali maharage na mchicha, akirudi anakuta wali njegele na nyama, jamani inakuwaje mtoto anamwambia nimejisikia tu kupika hivyo. Kumbe bwana mtoto ameota mapembe baada ya kuanza mapenzi na bwana shemeji.

Shost amekuja kumstukia mtoto akiamka asubuhi ni lazima akatapike bafuni, khaa wewe mtoto ni vipi tena hivi, kumpeleka hospitali akagundulika mtoto ana ki mimba cha wiki 6. Basi shost alimueleza yule mtoto hii mimba itabidi waitoe, mimba ilitolewa ikiwa na miezi mitatu.

Baada ya mimba kutolewa ndiyo shost anagundua kuwa mimba ilikuwa ya mume wake, kwa hasira alimpiga vibao dada, mume wa shost kusikia yale amekwenda police kuriport kuwa shost amefanya bodily harm crime amempiga mtu na kusababisha mimba kutoka. Hii ndiyo kesi inayomsubiri shost na akipatikana na hatia anafungwa.
 
Habari za leo waungwana,

Leo ni kali kuliko, huyu shost wa tangu boarding school, yale mambo ya kushare toothpaste na kuchanganya solution ili ulie mkate. Basi baada ya shule kila mtu aliendelea na ustaarabu wake, tumekutana mjini juzi tu na kubadilishana namba. Leo asubuhi dada yake ananipigia simu shost yuko Central Police Station.

Mkasa wenyewe ni hivi, shost ameolewa na amebahatika kupata watoto watatu, wa kiume wawil na wakike mmoja. Shost alihangaika sana kupata dada wa kumsaidia kazi, mama ofisini kwao akamletea binti kutoka mikoani, binti ni mzuri kaumbika, shost alimpeleka nyumbani na kumfahamisha taratibu za kazi.

Baada ya miezi mitatu kupita binti ameota mapembe ndani ya nyumba, shost akiagizi leo mchana chakula ni wali maharage na mchicha, akirudi anakuta wali njegele na nyama, jamani inakuwaje mtoto anamwambia nimejisikia tu kupika hivyo. Kumbe bwana mtoto ameota mapembe baada ya kuanza mapenzi na bwana shemeji.

Shost amekuja kumstukia mtoto akiamka asubuhi ni lazima akatapike bafuni, khaa wewe mtoto ni vipi tena hivi, kumpeleka hospitali akagundulika mtoto ana ki mimba cha wiki 6. Basi shost alimueleza yule mtoto hii mimba itabidi waitoe, mimba ilitolewa ikiwa na miezi mitatu.

Baada ya mimba kutolewa ndiyo shost anagundua kuwa mimba ilikuwa ya mume wake, kwa hasira alimpiga vibao dada, mume wa shost kusikia yale amekwenda police kuriport kuwa shost amefanya body harm crime amempiga mtu na kusababisha mimba kutoka. Hii ndiyo kesi inayomsubiri shost na akipatikana na hatia anafungwa.
Wanaume dhaifu, dhaifu and stupid!
 
huyo mwanaume hana akili!
mwambie hivyo!
mwambie na huyo mwanamke hana akilh.utachukuaje mwanamke mzuri kama wewe as your house help?
halafu mwambie akifika mahakamani aseme alikuwa anafanya self defence!
halafu umwambie kesi ikiisha,achukue hamsini huyo mwanaume hafai!
halafu kutoa halikuwa wazo zuri!
 

Similar Discussions

9 Reactions
Reply
Back
Top Bottom