Ndoa za siku hizi bwana! Wanajamii naomba mnisadie maana ndoa za siku hizi hazidumu kabisa ni mdudu gani kaingilia kati? Ndoa nazifananisha na mua, mbona wanandoa wanaanza kula kutamu na kumalizia kuchungu wakati inatakiwa uanze kula kuchungu umalizie kutamu. nina swali moja kwa kila jinsia tafadhali:
- Mume ungependa kufanyiwa nini haswa kwenye ndoa ili usiende nje?
- Mke nawe pia ungependa kufanyiwa nini, mnataka mpendejwe na vitu gani mnashidwa kuwafanyia waume zenu mpaka waangaike?