Ndio maana tv za bongo zinakufa

lendila

JF-Expert Member
Sep 26, 2012
5,806
4,370
Ndio maana tv za bongo zinakufa,hawajui wateja wao wanapenda nini, wao wanawalisha wateja wao habari ambazo wateja wao hawazipendi. Nitatoa mifano michache...

Vyombo vya habari vya Tanzania viliripoti habari za mkutano mkuu wa CCM, bila kujali wateja wao wanapenda nini lakini mkutano mkuu wa CHADEMA vyombo vya habari vya ndani havikuripoti live hata kimoja bila kujali kama mkutano mkuu wa CHADEMA una watazamaji wengi

Mfano wa pili ni msiba wa mzee Ndesamburo,watanzania wengi sana wanataka kujua nini kinaendelea kwenye msiba wa mzee Ndesamburo na kwa chombo chochote cha habari kilicho makini kingejitahidi kuhabarisha umma ni kinaendelea kwenye msiba wa mzee Ndesamburo mjini Moshi,sasa kama hawaamini nilichokiandika,wasubiri waangalie ni wananchi wangapi watakaofutilia msiba wa mzee Ndesamburo kwenye mitandao ya kijamii.

Vyombo vya habari vikiendelea na tabia hii,vitabaki kama mapambo na pengine vitakuwa vinatazamwa na wamiliki pekee tu,wananchi tunahamia kwenye tv online,na mitandao ya kijamii.
 
Ndio maana tv za bongo zinakufa,hawajui wateja wao wanapenda nn?wao wanawalisha wateja wao habari ambazo wateja wao hawazipendi
Nitatoa mifano michache

Vyombo vya habari vya tanzania viliripoti habari za mkutano mkuu wa ccm,bila kujali wateja wao wanapenda nn?lkn mkutano mkuu wa chadema vyombo vya habari vya ndani havikuripoti live hata kimoja bila kujali kama mkutano mkuu wa chadema unawatazamaji wengi

Mfano wa pili ni msiba wa mzee ndesamburo,watanzania wengi sana wanataka kujua nn kinaendelea kwenye msiba wa mzee ndesamburo,na kwa chombo chochote cha habari kilicho makini kingejitahidi kuhabarisha umma ni kinaendelea kwenye msiba wa mzee ndesamburo mjini moshi,sasa kama hawaamini nilichokiandika,wasubiri waangalie ni wananchi wangapi watakaofutilia msiba wa mzee ndesamburo kwenye mitandao ya kijamii

Vyombo vya habari vikiendelea na tabia hii,vitabaki kama mapambo,na pengine vitakuwa vinatazamwa na wamiliki pekee tu,wananchi tunahamia kwenye tv online,na mitanda ya kijamii

Usemacho ni kweli mfano Clouds na Star TV,achilia mbali TBCCM
 
Ndio maana tv za bongo zinakufa,hawajui wateja wao wanapenda nn?wao wanawalisha wateja wao habari ambazo wateja wao hawazipendi
Nitatoa mifano michache
Tumezoea kulalamika kama vyura! Kwanini wapinzania wasianzishe vyombo vyao vya habari?
 
Kinachofanya na vyombo vyetu vya habari kwa sasa ni sawa na kuwalazimishia wateja bidhaa wamiliki wanazotaka,badala kuwapa wateja wanachotaka,angalia idadi ya watanzamaji wa tv kwa sasa imepungua sana,wananchi siku hizi mtaani hata taarifa ya habari hawaangalii tena
 
Uko sahihi sana .. Star TV imepoteza ma elfu ya watazamaji kipindi cha asubuhi tangu wamrushe BASHITE....

ACHA VITUO VIFE TU.

Itv wakionyesha coverage ya Ndesa leo watajivunia watazamaji wapya wengii. Wacha tusubiri.
 
Vyombo vya habari vinamuogopa mkulu. Alishasema "vyombo vya habari viko huru but not to that extent"
 
kalupieni matangazo mrushwe live, chadema punguzeni ubashite bhana. muda wote mnawaza ujinga tu, wekeni mikakati ya kuingia ikulu 2030 na sio vinginevyo!!

jpm anapiga kazi ya ukweli sana, ingawa tunaona anazingua, mrithi wake atapiga kazi chini ya kiwango chake, ndipo atakumbukwa jpm na huo ndo muda wa kuchagua upinzani.


siasa sio kuja arithmetics kwa kuangalia kura za 2005, 2010 na 2015!!


pambaneni kuongeza wabunge, madiwani na wenyeviti wa vijiji na mitaa.

kama lengo lenu ni kushika dola anzeni kuwalipa wenyeviti wenu wa vijiji, mitaa au vitongoji hata 40,000 kila baada ya miezi mitatu.

ccm wamejipanga vzr sana, wamefanya marejebisho na wana uhakika wa kura 5,000,000 mwk 2020 kbla ya kampeini.

halafu chadema acheni ukanda, Mimi hadi 2011, nilikuwa chadema damudamu. nilipofika Udsm, nikapangiwa hostel ya mabibo na jamaa wa karutu na moshi, wakawa wanatamba sana kuwa wao ndiyo wakombozi wa nchi hii.

nikawa nahudhuria vikao pale landmark yaani pale ujinga uliosema ni kugawana vyeo tu. safu ya rais, mawaziri, marc, madc, maras na maded ilikamilika 2013!!

yaani nusu yao walikuwa chagadema, na misukule wachache.


may 20, 2014 nikachukua rasmi kadi ya ccm, chama dume, na mwaka huohuo serukali za mitaa ccm ikashinda na 2015 ikashinda kwa zali,

kama jk aliagiza vifaa vya PT vipya 2015, kumbe ngosha ataleta vifaa super vya tpdf vipya ili kuweka sawa mambo.

naipenda chadema, cuf, act na ccm.

naipenda zaidi Tanzania na rais wa jmt,

ova
 
Ndio maana tv za bongo zinakufa,hawajui wateja wao wanapenda nini, wao wanawalisha wateja wao habari ambazo wateja wao hawazipendi. Nitatoa mifano michache...

Vyombo vya habari vya Tanzania viliripoti habari za mkutano mkuu wa CCM, bila kujali wateja wao wanapenda nini lakini mkutano mkuu wa CHADEMA vyombo vya habari vya ndani havikuripoti live hata kimoja bila kujali kama mkutano mkuu wa CHADEMA una watazamaji wengi

Mfano wa pili ni msiba wa mzee Ndesamburo,watanzania wengi sana wanataka kujua nini kinaendelea kwenye msiba wa mzee Ndesamburo na kwa chombo chochote cha habari kilicho makini kingejitahidi kuhabarisha umma ni kinaendelea kwenye msiba wa mzee Ndesamburo mjini Moshi,sasa kama hawaamini nilichokiandika,wasubiri waangalie ni wananchi wangapi watakaofutilia msiba wa mzee Ndesamburo kwenye mitandao ya kijamii.

Vyombo vya habari vikiendelea na tabia hii,vitabaki kama mapambo na pengine vitakuwa vinatazamwa na wamiliki pekee tu,wananchi tunahamia kwenye tv online,na mitandao ya kijamii.
Anzisheni vyombo vyenu vya habari a see tusiharibiane program za vipind
 
Siku hizi kutokana na teknolojia ukitama kipindi kinarushwa hewani live,unaona na watanzamaji wangapi wanaangalia kipindi,mfano angalia kipindi cha binge cha maswali na majibu,unakuta bunge watazamaji ni 40 mpaka 50 tu
 
Angalau Clouds wameanza kuwa na akili tangu waachane na BASHITE..

Ile ilisaidia kuwatoa matongotango,maana walikuwa hawaoni wala kusikia.Sawa na Nape,baada ya kupigwa teke sasa amerudisha akili
 
Watu wako kibiashara wewe unataka bure kana kwamba uliwachangia mtaji wa kuanzisha media
 
Back
Top Bottom