Meitinyiku L. Robinson
JF-Expert Member
- Aug 29, 2011
- 412
- 90
Ndugu wanabodi kuna taarifa zimeanza kuzagaa mitaani kuwa Ndugu Bernad Membe yuko katika mikakati ya kuandaa barua za kutosha na hatimaye kugawa katika ngazi zote za Wilaya na hatimaye Mikoani.
Habari hizi zimeshtua na kushangaza wengi katika tasnia hii ya Siasa hasa baada ya jambo hili kuonekana kutaka kufanyika baada ya Chaguzi za Chama kumalizika hivi majuzi Mkoani Dodoma. Japo bado haijafahamika hasa lengo, na madhumuni ya barua hizo makada hasa viongozi wa Chama katika baadhi ya Mikoa wamekuwa na hamu ya kuzipata na hatimaye kujiridhisha nazo.
Na hili limekuwa na utata hasa ikidhaniwa kuwa kama kweli ni barua za kushukuru ni kwa nini atumie mtindo huo?? Manake 80% ya wajumbe walioshinda wamekuwa wakiwashukuru wapiga kura kwa njia ya ujumbe mfupi kwa simu. Sasa hili la Mhe Membe linaonekana kuwa na walakini na la mashaka sana.
Imani ya watu walio wengi ni kuwa baada ya Mhe. Raisi na Mwenyekiti wa Chama kuonekana kuwa mkali katika swala zima la matumizi ya rushwa katika chaguzi, wagombea wengi hawakupata nafasi ya kutoa mlungula katika uchaguzi wa juzi hivyo inaaminika kuwa Membe anataka kutumia fursa hiyo kuua ndege wawili kwa jiwe moja. Kwamba zaidi ya barua ya shukurani basi zile za Gadaffi nazo zitanyunyizwa humo kwa kila mjumbe ikiwa ni kuendelea na harakati zake za kujaribu kutafuta geti la Magogoni.
Baadhi ya Mawaziri na Manaibu wak vile vile wameshangazwa na hili wengi wao nao pia wakitamani sana kuona mwisho wa mkakati wa hayo mwenzao atakayo kuyafanya na matunda yake yatakayozaliwa ni yepi??
Niseme tu wahusika jiandaeni kupokea bahasha zenu na mfurahie mtakayokutana nayo manake kwa kweli hata mimi binafsi siwezi amini kuwa ni barua za shukrani tu. kwa nini iwe hivyo?? Wapo kina January, Wasira, Shigela, Mathayo, Mbarawa, Shaka, Nchemba, Mukandara to mention some wao walituma sms sasa hili la jamaa........
Habari hizi zimeshtua na kushangaza wengi katika tasnia hii ya Siasa hasa baada ya jambo hili kuonekana kutaka kufanyika baada ya Chaguzi za Chama kumalizika hivi majuzi Mkoani Dodoma. Japo bado haijafahamika hasa lengo, na madhumuni ya barua hizo makada hasa viongozi wa Chama katika baadhi ya Mikoa wamekuwa na hamu ya kuzipata na hatimaye kujiridhisha nazo.
Na hili limekuwa na utata hasa ikidhaniwa kuwa kama kweli ni barua za kushukuru ni kwa nini atumie mtindo huo?? Manake 80% ya wajumbe walioshinda wamekuwa wakiwashukuru wapiga kura kwa njia ya ujumbe mfupi kwa simu. Sasa hili la Mhe Membe linaonekana kuwa na walakini na la mashaka sana.
Imani ya watu walio wengi ni kuwa baada ya Mhe. Raisi na Mwenyekiti wa Chama kuonekana kuwa mkali katika swala zima la matumizi ya rushwa katika chaguzi, wagombea wengi hawakupata nafasi ya kutoa mlungula katika uchaguzi wa juzi hivyo inaaminika kuwa Membe anataka kutumia fursa hiyo kuua ndege wawili kwa jiwe moja. Kwamba zaidi ya barua ya shukurani basi zile za Gadaffi nazo zitanyunyizwa humo kwa kila mjumbe ikiwa ni kuendelea na harakati zake za kujaribu kutafuta geti la Magogoni.
Baadhi ya Mawaziri na Manaibu wak vile vile wameshangazwa na hili wengi wao nao pia wakitamani sana kuona mwisho wa mkakati wa hayo mwenzao atakayo kuyafanya na matunda yake yatakayozaliwa ni yepi??
Niseme tu wahusika jiandaeni kupokea bahasha zenu na mfurahie mtakayokutana nayo manake kwa kweli hata mimi binafsi siwezi amini kuwa ni barua za shukrani tu. kwa nini iwe hivyo?? Wapo kina January, Wasira, Shigela, Mathayo, Mbarawa, Shaka, Nchemba, Mukandara to mention some wao walituma sms sasa hili la jamaa........