Ndg Kinana, hili la MNEC wako tulichukulie kama TAKRIMA ama RUSHWA?

Meitinyiku L. Robinson

JF-Expert Member
Aug 29, 2011
412
90
Ndugu wanabodi kuna taarifa zimeanza kuzagaa mitaani kuwa Ndugu Bernad Membe yuko katika mikakati ya kuandaa barua za kutosha na hatimaye kugawa katika ngazi zote za Wilaya na hatimaye Mikoani.

Habari hizi zimeshtua na kushangaza wengi katika tasnia hii ya Siasa hasa baada ya jambo hili kuonekana kutaka kufanyika baada ya Chaguzi za Chama kumalizika hivi majuzi Mkoani Dodoma. Japo bado haijafahamika hasa lengo, na madhumuni ya barua hizo makada hasa viongozi wa Chama katika baadhi ya Mikoa wamekuwa na hamu ya kuzipata na hatimaye kujiridhisha nazo.

Na hili limekuwa na utata hasa ikidhaniwa kuwa kama kweli ni barua za kushukuru ni kwa nini atumie mtindo huo?? Manake 80% ya wajumbe walioshinda wamekuwa wakiwashukuru wapiga kura kwa njia ya ujumbe mfupi kwa simu. Sasa hili la Mhe Membe linaonekana kuwa na walakini na la mashaka sana.

Imani ya watu walio wengi ni kuwa baada ya Mhe. Raisi na Mwenyekiti wa Chama kuonekana kuwa mkali katika swala zima la matumizi ya rushwa katika chaguzi, wagombea wengi hawakupata nafasi ya kutoa mlungula katika uchaguzi wa juzi hivyo inaaminika kuwa Membe anataka kutumia fursa hiyo kuua ndege wawili kwa jiwe moja. Kwamba zaidi ya barua ya shukurani basi zile za Gadaffi nazo zitanyunyizwa humo kwa kila mjumbe ikiwa ni kuendelea na harakati zake za kujaribu kutafuta geti la Magogoni.

Baadhi ya Mawaziri na Manaibu wak vile vile wameshangazwa na hili wengi wao nao pia wakitamani sana kuona mwisho wa mkakati wa hayo mwenzao atakayo kuyafanya na matunda yake yatakayozaliwa ni yepi??

Niseme tu wahusika jiandaeni kupokea bahasha zenu na mfurahie mtakayokutana nayo manake kwa kweli hata mimi binafsi siwezi amini kuwa ni barua za shukrani tu. kwa nini iwe hivyo?? Wapo kina January, Wasira, Shigela, Mathayo, Mbarawa, Shaka, Nchemba, Mukandara to mention some wao walituma sms sasa hili la jamaa........
 
Ndugu wanabodi kuna taarifa zimeanza kuzagaa mitaani kuwa Ndugu Bernad Membe yuko katika mikakati ya kuandaa barua za kutosha na hatimaye kugawa katika ngazi zote za Wilaya na hatimaye Mikoani.

Habari hizi zimeshtua na kushangaza wengi katika tasnia hii ya Siasa hasa baada ya jambo hili kuonekana kutaka kufanyika baada ya Chaguzi za Chama kumalizika hivi majuzi Mkoani Dodoma. Japo bado haijafahamika hasa lengo, na madhumuni ya barua hizo makada hasa viongozi wa Chama katika baadhi ya Mikoa wamekuwa na hamu ya kuzipata na hatimaye kujiridhisha nazo.

Na hili limekuwa na utata hasa ikidhaniwa kuwa kama kweli ni barua za kushukuru ni kwa nini atumie mtindo huo?? Manake 80% ya wajumbe walioshinda wamekuwa wakiwashukuru wapiga kura kwa njia ya ujumbe mfupi kwa simu. Sasa hili la Mhe Membe linaonekana kuwa na walakini na la mashaka sana.

Imani ya watu walio wengi ni kuwa baada ya Mhe. Raisi na Mwenyekiti wa Chama kuonekana kuwa mkali katika swala zima la matumizi ya rushwa katika chaguzi, wagombea wengi hawakupata nafasi ya kutoa mlungula katika uchaguzi wa juzi hivyo inaaminika kuwa Membe anataka kutumia fursa hiyo kuua ndege wawili kwa jiwe moja. Kwamba zaidi ya
barua ya shukurani basi zile za Gadaffi nazo zitanyunyizwa humo kwa kila mjumbe ikiwa ni kuendelea na harakati zake za kujaribu kutafuta geti la Magogoni.

Baadhi ya Mawaziri na Manaibu wak vile vile wameshangazwa na hili wengi wao nao pia wakitamani sana kuona mwisho wa mkakati wa hayo mwenzao atakayo kuyafanya na matunda yake yatakayozaliwa ni yepi??

Niseme tu wahusika jiandaeni kupokea bahasha zenu na mfurahie mtakayokutana nayo manake kwa kweli hata mimi binafsi siwezi amini kuwa ni barua za shukrani tu. kwa nini iwe hivyo?? Wapo kina January, Wasira, Shigela, Mathayo, Mbarawa, Shaka, Nchemba, Mukandara to mention some wao walituma sms sasa hili la jamaa........

Kikwetu 'shondola' maana yake ni 'wivu'. Utabaki hivyo hivyo.
 
Membe kachota pesa uarabuni ili aingie GOGONI ila hana nafasi iyo.KWANZA KINANA AJIBU KWANZA TUHUMA ZA UJANGILI ZILIZOMUELEMEA.
 
Kikwetu 'shondola' maana yake ni 'wivu'. Utabaki hivyo hivyo.

Kumbe ni kikwenu Comrade sasa wajameni nami ningekuambia maana ya Kanyorota kikwetu ungekuwa wapi leo??? Nchi hii ina Kikwao zaidi ya 120 sasa hiyo yako ni sawa na chembe ya haradani!! Ila kimsingi hali halisi ndo hiyo jibu hoja kwa hoja. Na kama huna cha kujibu na unapenda hilo jina la Kanyorota lisomeka basi ungesema wapita tu kuliko kuandika kwa kuogelea....... Pole sana.
 
Shukrani kwa njia ya barua ni jambo la kawaida tu katika mazingira kama haya, unachotakiwa kuwa nacho ni mchakato ulio wazi, usio na alama za rushwa, uwe na muda na pia uwe na resources (bahasha 3,000 na rim nne za A4 Papers); Haitazidi shillingi milioni mbili na nusu;

Ni ubunifu mzuri na utamsaidia kuzidi kuwa karibu na wahusika, na kwa hili, kawapiga bao wenzake; Otherwise hawezi kutoa rushwa ndani ya barua hizo, hilo ni jambo lisilowezekana;
 
wewe kweli umbeya umesomea!!! umepoteza muda wote huo kuandika jambo usilo kuwa na uhakika nalo! kuna ubaya gani kuwashukuru watu walio mchagua kwa barua?? je angetaka kutoa rushwa kwa kutumia simu hawezi? hakika wewe una jambo lako.umeiaibisha jamii ya GREAT THINKERS.YOU ARE NOT ONE OF THEM.
 
Nimeani JF kuna pro-Memba, lowasa, JK, Slaa, Lipumba, Mbowe, Zito nk! sasa nadhani tungeanza mchakato wa kampeni!
 
Shukrani kwa njia ya barua ni jambo la kawaida tu katika mazingira kama haya, unachotakiwa kuwa nacho ni mchakato ulio wazi, usio na alama za rushwa, uwe na muda na pia uwe na resources (bahasha 3,000 na rim nne za A4 Papers); Haitazidi shillingi milioni mbili na nusu;

Ni ubunifu mzuri na utamsaidia kuzidi kuwa karibu na wahusika, na kwa hili, kawapiga bao wenzake; Otherwise hawezi kutoa rushwa ndani ya barua hizo, hilo ni jambo lisilowezekana;

mkuu Mchambuzi naona bado unaendelea na ndoto zako za kuwa membe na january wanaweza kuchukua nchi, mimi bado na subiri nione utabiri wako mkuu.
 
mkuu Mchambuzi naona bado unaendelea na ndoto zako za kuwa membe na january wanaweza kuchukua nchi, mimi bado na subiri nione utabiri wako mkuu.

Kwanza nirudie tena kwamba kuandikia wajumbe barua haina tatizo, na hata ukiweza kuandikia barua ya shukrani wapiga kura wa jimbo zima (ubunge) au kata nzima (udiwani), ni sawa tu, ni juu yako na uwezo wako, kikubwa pasiwe na shaka yoyote juu ya rushwa au matumizi ya hela nyingi ambazo zinaweza kutoa ishara kwamba una fedha haramu; Sasa kama hoja yangu hii imekusumbua kiasi cha kukejeli mjadala wangu juu ya membe au january kuwa wagombea wa CCM, sioni msingi wake;

Pili, suala la membe na january, ule haukuwa utabiri bali uchambuzi kwa HOJA, based on utamaduni wa CCM pamoja na jinsi gani mchakato wa uchaguzi wa ndani wa CCM ulivyomalizika hivi karibuni; Wapo walioelewa hoja yangu ya msingi lakini pia wapo ambao aidha kwa makusudi au kwa bahati mbaya, hawakunielewa, wewe ukiwa ni mmoja wao; vinginevyo mgongano wa mawazo ni jambo la kawaida, ili mradi uwe ni wa hoja dhidi ya hoja;

Yote haya ni kunapo majaliwa, usiseme unasubiria 2015, weka condition yote hiyo mikononi mwa muumba;
 
Back
Top Bottom