Kipis
JF-Expert Member
- Jul 23, 2011
- 492
- 61
Pata yai moja la kienyeji,lipasulie ndani ya kisosi cha chai,kisha changanya na vijiko vitatu vidogo vya asali mbichi ya nyuki wa aridhini. Koroga kwa muda usiopungua dk3. Kumbuka dawa hii inatakiwa uitumie kabla ya kunyoa ndevu zako. Ipake hiyo dawa mahala husika, kisha iache kwa muda wa dk3, baada ya hapo waweza kunyoa ndevu zako bila ya kuchanganya na kitu chochote zaidi ya hivyo nilivyo elekeza. Angalizo: ngozi yako yaweza kuwa na mikunjomikunjo. Lakini waweza kutumia mafuta ya ufuta yaliyochanganywa na mafuta ya habat sauda. Jipake uso wote kisha yaache kwa saa24 bila kuosha uso.