BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,825
- 287,847
Ndesamburo amshangaa JK
na Grace Macha, Moshi
Tanzania Daima
MBUNGE wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo (CHADEMA), amesema inashangaza kuona nchi iko katika mgogoro, lakini Rais (Jakaya Kikwete) anaikimbia anakwenda kwenye ziara nje ya nchi.
Ndesamburo aliyewahi kufanya kazi serikalini wakati wa Awamu ya Kwanza ya utawala wa Mwalimu Julius Nyerere aliyasema hayo jana nyumbani kwake mjini Moshi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.
Alisema, Rais alipaswa kutulia nchini na kushughulikia tatizo lililopo alilodai ni kubwa, kwani kelele za tuhuma za ufisadi zinazopigwa sasa nchini si jambo la kupuuzwa, bali linapaswa kupatiwa ufumbuzi.
Nchi iko katika mgogoro, nashangaa rais wetu anakimbia nchi wakati huu anapaswa kulivunja baraza la mawaziri ikibidi afanye kazi kwa muda na makatibu wakuu wa wizara siyo alivunje leo aliunde kesho, atakuwa hajapata muda wa kutosha kutafakari, alisema mbunge huyo.
Hata hivyo, alisema rais anapaswa kutumia muda kutafakari kabla ya kuteua mawaziri wengine ambapo alishauri aunde baraza la mawaziri litakalokuwa dogo, atakaloweza kulimudu.
Kwa kauli hiyo, Ndesamburo anaingia kwenye mwelekeo unaofanana na kundi la wazee nchini wakiwemo Joseph Butiku (Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere), Joseph Warioba, John Malecela (Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara) na Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi waliojitokeza kutoa tamko juu ya tatizo la ufisadi na ukiukwaji wa maadili ya uongozi nchini.
Septemba 15 mwaka huu, viongozi wa vyama vinne vya upinzani vya CHADEMA, NCCR, TLP na CUF vilitoa tamko jijini Dar es Salaam ambapo Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa alitaja majina 11 ya viongozi waandamizi serikalini aliowatuhumu kuwa mafisadi.
Tangu kutolewa kwa tamko hilo, baadhi ya waliotuhumiwa wamejitokeza hadharani na kukanusha shutuma hizo na kuahidi kulifikisha suala hilo mahakamani, lakini mpaka sasa hakuna aliyekwenda kufungua mashitaka.
Hivi karibuni Rais Jakaya Kikwete akizungumza kwenye hafla ya harambee iliyoandaliwa jijini Arusha na Kanisa la KKKT, alisema serikali itawachunguza wote waliotuhumiwa kwa rushwa na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria iwapo watabainika kuhusika.
Katika hatua nyingine, Ndesamburo alishauri serikali kuacha kutoa fedha za ruzuku kwa vyama vya siasa, badala yake fedha hizo zipelekwe kwenye majimbo kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.
Alisema vyama vya siasa ni mali ya wanachama, hivyo vinapaswa kujiendesha kwa kile alichosema fedha zinazoingizwa kwenye vyama hivyo hutumiwa kwa masilahi yao wenyewe na si ya taifa.
na Grace Macha, Moshi
Tanzania Daima
MBUNGE wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo (CHADEMA), amesema inashangaza kuona nchi iko katika mgogoro, lakini Rais (Jakaya Kikwete) anaikimbia anakwenda kwenye ziara nje ya nchi.
Ndesamburo aliyewahi kufanya kazi serikalini wakati wa Awamu ya Kwanza ya utawala wa Mwalimu Julius Nyerere aliyasema hayo jana nyumbani kwake mjini Moshi alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari.
Alisema, Rais alipaswa kutulia nchini na kushughulikia tatizo lililopo alilodai ni kubwa, kwani kelele za tuhuma za ufisadi zinazopigwa sasa nchini si jambo la kupuuzwa, bali linapaswa kupatiwa ufumbuzi.
Nchi iko katika mgogoro, nashangaa rais wetu anakimbia nchi wakati huu anapaswa kulivunja baraza la mawaziri ikibidi afanye kazi kwa muda na makatibu wakuu wa wizara siyo alivunje leo aliunde kesho, atakuwa hajapata muda wa kutosha kutafakari, alisema mbunge huyo.
Hata hivyo, alisema rais anapaswa kutumia muda kutafakari kabla ya kuteua mawaziri wengine ambapo alishauri aunde baraza la mawaziri litakalokuwa dogo, atakaloweza kulimudu.
Kwa kauli hiyo, Ndesamburo anaingia kwenye mwelekeo unaofanana na kundi la wazee nchini wakiwemo Joseph Butiku (Mkurugenzi wa Taasisi ya Mwalimu Nyerere), Joseph Warioba, John Malecela (Makamu Mwenyekiti wa CCM Tanzania Bara) na Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi waliojitokeza kutoa tamko juu ya tatizo la ufisadi na ukiukwaji wa maadili ya uongozi nchini.
Septemba 15 mwaka huu, viongozi wa vyama vinne vya upinzani vya CHADEMA, NCCR, TLP na CUF vilitoa tamko jijini Dar es Salaam ambapo Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willibrod Slaa alitaja majina 11 ya viongozi waandamizi serikalini aliowatuhumu kuwa mafisadi.
Tangu kutolewa kwa tamko hilo, baadhi ya waliotuhumiwa wamejitokeza hadharani na kukanusha shutuma hizo na kuahidi kulifikisha suala hilo mahakamani, lakini mpaka sasa hakuna aliyekwenda kufungua mashitaka.
Hivi karibuni Rais Jakaya Kikwete akizungumza kwenye hafla ya harambee iliyoandaliwa jijini Arusha na Kanisa la KKKT, alisema serikali itawachunguza wote waliotuhumiwa kwa rushwa na kuwafikisha kwenye vyombo vya sheria iwapo watabainika kuhusika.
Katika hatua nyingine, Ndesamburo alishauri serikali kuacha kutoa fedha za ruzuku kwa vyama vya siasa, badala yake fedha hizo zipelekwe kwenye majimbo kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.
Alisema vyama vya siasa ni mali ya wanachama, hivyo vinapaswa kujiendesha kwa kile alichosema fedha zinazoingizwa kwenye vyama hivyo hutumiwa kwa masilahi yao wenyewe na si ya taifa.