Ndejembi: Watumishi wa umma 1,477 wasimamishwa kazi 2015-2022

Lady Whistledown

JF-Expert Member
Aug 2, 2021
1,023
1,609
NDEJEMBI: WATUMISHI WA UMMA 1,477 WASIMAMISHWA KAZI 2015-2022

Naibu Waziri katika Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Deogratius Ndejembi amesema Watumishi wa Umma 1,477 wamesimamishwa kazi kwa kukiuka Sheria, Kanuni, Taratibu na Miongozo inayosimamia nidhamu katika Utumishi wa Umma kuanzia mwaka 2015 hadi 2022

Ameyasema hayo leo Jumatatu Aprili 11, 2022 wakati akijibu Swali la Nyongeza la Mbunge wa Mlimba, Godwin Kunambi aliyehoji sababu za mashauri yanayoendelea kusikilizwa na Tume ya Utumishi wa Umma kuchukua muda mrefu sana

Ndejembi ameongeza kuwa Watumishi 598 wamekata rufaa Tume ya Utumishi wa Umma, ambapo rufaa 411 zina maelezo yaliyokamilika na 187 hazina vielelezo na zimerudishwa kwa Waajiri kwa Mamlaka za Nidhamu ili ziweze kufanyiwa kazi
 
Mashauri yanachukua mpaka miaka mitatu sijui kipi huwa wanafanya hao tume ya utumish! Halafu kuna wale wanaomba vibali vya kurejea utumishi baada ya kuacha kazi wenyewe ama kuchufukuzwa kazi, baso hayo majibu ya kuwa umekubaliwa ama umekataliwa nayo huchukua muda sana ni kuanzia miaka w mpka 3 au zaidi ya hapo. Hapo waziri hajatoa ufafanuzi wa kutosha kuhisu suala hilo.
 
mashauri yanachukua mpaka miaka mitatu sijui kipi huwa wanafanya hao tume ya utumish! Halafu kuna wale wanaomba vibali vya kurejea utumishi baada ya kuacha kazi wenyewe ama kuchufukuzwa kazi, baso hayo majibu ya kuwa umekubaliwa ama umekataliwa nayo huchukua muda sana ni kuanzia miaka w mpka 3 au zaidi ya hapo. Hapo waziri hajatoa ufafanuzi wa kutosha kuhisu suala hilo.
Wanafanya kazi kwa mapozi na kunywa soda wakati huo huo viyoyozi havipo mbali
 
Back
Top Bottom