Ndege yetu na route za Daladala

Nina uhakika 100% ununuzi wa hii ndege ni upuuzi mtupu. Ni hasara juu ya hasara. Mkuu amekurupuka mnoo. Hakuna tofauti yoyote na mradi wa kile kivuko cha Dar ambacho kilinunuliwa ili kupunguza msongamano na kikazinduliwa na Magu mwenyewe, lakini mwisho wa siku kikayeyuka.
Hata hili la ndege ipo siku wanaobisha hapa watakuja kuelewa na hata mkuu mwenyewe atakuja kulikana hilo dege.

Tujipe muda na tuwe na subiri tu. Ukweli huwa haujifichi, unaweza kucheleweshwa lakini ipo siku utakuwa wazi tu.
Mtapata taabu sana awamu hii...!!!
 
Katika taarifa za kitaalamu ni kwamba chombo chetu tulichokipokea kwa mbwembwe na kila aina ya ushabiki, hakitakiwi kusafiri chini ya 8hrs ikiwa angani kutokana na technical design yake kwamba ni ya masafa marefu for more than 8hrs. Hii ili kuipa engine stability zaidi and proper use of other operating devises.

Kwa ndege kama ile kufanya local routes ni sawa na mabasi ya mkoani kupiga route za daladala tena zile fupi fupi za Tandika-Kkoo au Makumbusho-Mwenge au Ubungo-Tegeta.....
Kwakweli yajayo yanafurahisha
Hata kama nauli itakuwa mia 5 , nimeapa kutopanda ule ujinga wao , sitaki kuunga mkono vitu ambavyo vimenunuliwa kimagumashi .
 
Hivi ile ndege ya Rais alonunua mkapa iko wapi? Awamu ya nne mama salma alikuwa anatanua nalo
 
Punguzeni uzwazwa ndege imekuja juz tu kutwa kuiongelea iyo mengine yote mmesaau,binadamu wa kitanzania ndiye kiumbe pekee ambacho unaweza kukipumbaza kwa lolote na ukafanikiwa.
 
Tumeondolewa kwenye mfumo wa kimataifa wa aviation wa IATA kwa sababu tuna madeni ya Mabilioni ya Shilingi, Hizo International flight tutaziratibu vipi?
-ve attitude.

kama waliweza kununua hilo dege la mabilioni unadhani ni nini kitakachowashinda kulipa hayo mabilioni ya madeni kusudi dege lifanye kazi. After all IATA wanapenda kuwa shirika lilwe na ndege za uhakika; ATCL iliondolewa siyo kwa madeni tu, bali kwa sababau haikuwa na ndege za kuaminika.
 
Hivi nani kawambia ukinunua ndege lazima ianze na safari za ndani, ingenunuliwa na serikali ya Zanzibar au Rwanda au visiwa vya comorro ingetua viwanja vipi vya ndani, acheni kukariri.
ukijibiwa unitag
 
Hata kama nauli itakuwa mia 5 , nimeapa kutopanda ule ujinga wao , sitaki kuunga mkono vitu ambavyo vimenunuliwa kimagumashi .
Hahahahaa, unajua fika hutoruhusiwa kwani huwezi kupanda ndege ukiwa na yeboyebo rangi tofauti, mfuko wa rambo na chupa ya gogo..
 
Kamanda, mpelekee hii taarifa yule mkuu wa genge lenu wa lawasaliti kule ubelgiji ili awaambie mabwana waje waichukue.
 
Wabongo sijui nani katuloga Kipindi cha bombadia, tuliponda ndege gani inazidiwa kasi na bajaji, haya boing imekuja tunaanza uchuro wetu tena

Haya toeni ushauri tufanye nini sasa maana tunakuwa kama tumelogwa na aliyetuloga kafa so tupo kuweweseka tu.
 
Watanzania tumezidi sasa ' Majungu ' hebu tutulie na tuwaachie ATCL watajua nini cha Kufanya. Kuna muda mnakera!
Wahenga walisema, "mtaji wa maskini ni majungu"; chadema wamekuwa maskini wa hoja kwa hiyo lazima waje na aina yoyote ya porojo na majungu ili waonekane bado wamo. Chama kilichojijenga kwa kutumia hoja sasa kinajiendesha kwa kutumia porojo: too bad!
 
Watanzania kila kitu kukosoa tu! Sijui ni wivu! Faida ya ndege sio lazima iende nje au ifanye safari za ndani. Ndege sio mchezo hata kuingia ndani na kutoka tu ni faida. Shilawadu wametuonyesha wameijaribu na watanzania wengi tunapenda shilawadu hiyo sio faida? Hata likipaki tu lisipofanya kaz kabisa bado kwetu ni faida. Wengine hatukuwahi panda denge tukiwa watoto kwanini tusipende ndege tukiwa wakubwa!!
Jambo la msingi hapa ni kuruhusu watanzania wanayoipenda ndege yao hata wamikoani wafike dar waonje utamu was denge yao kwa kuingia na kutoka.
Tuache kulalamia, tuipende ndege yetu.
 
Unaweweseka kweli ww....concept hapo ipo kwenye ndege kubwa kama hyo kuanza kupiga route za ndani usiwe nyumbu kiivo wataalam wesha eleza kuwa engine ikikolea iwe more than 8hrs sasa from dar to mwanza ni masaa mangap? Huon kama tunaiumiza
Mimi hili la masaa manane sijui limetoka wapi maana ghafla wataalamu wa Boeng wameibuka. siandiki kuunga mkono kununua au hapana ila hili la 8 hours halina mshiko, maana hata kwenda Dubai ni kama 5 hours tu halafu kuna ndege kubwa na maanisha kubwa kama airbus 380 inatoka Dubai to Mumbai kama 2 hours tu sasa hii ya dreamline utasema sijui ina ukubwa gani. na nchi nyingi wanatumia Boeng na ndege zingine kubwa kwa domestic routes na safari za 1 mpaka 2 hours. labda hoja ingekuwa je ATCL walikuwa wa business ideas hii ndege itakuwa inapiga route zipi na vizuri wakachagua nchi za east africa halafu shusha bei kidogo watapata sana maana bado kusafiri within EA na ghali sana sijui ni kwanini maana kwenda Dubai ni rahisi kuliko kwenda Kenya nadhani sababu hakuna ushindani na hii ni nafasi ya kuchukuwa business.
 
Muwe mnasoma ilani kama inawafaa kabla ya kuchagua.

Yule mkwere bahati nzuri/mbaya alipata sema ilani haitekelezeki. Sasa tunaye Jiwe Sezonje anaisimamia ipasavyo.

Huyo Jiwe Sezonje ndiye nani???!!! Msiletehumu majina yanayowadhalilisha viongozi wetu ...
 
Moja ya sababu zinazofanya nchi zetu kuwa masikini ni kuamini sana wanasiasa.

Hizi habari za shaka sana, halafu mtu anasema "bila shaka walifanya research".

Iko wapi hiyo research?
Alisema Kagame alimwambia " we nunua tu"
Na akasema anamshukuru sana Kagame.
 
Heeee!!yaani boing 787 iwe na masafa ya dk 50 hadi 60!!!bado unaleta sababu kama hiyo kweli??kwanza hiyo gharama ya kuruka tu itarudi kutoka kwenye hizo nauli za route hizo??
mie taarifa zangu nimezitoa website ya Boeing wewe zako umezitoa wapi? hizo gharama hebu zitaje, sio kuleta porojo za kishamba
 
Mimi hili la masaa manane sijui limetoka wapi maana ghafla wataalamu wa Boeng wameibuka. siandiki kuunga mkono kununua au hapana ila hili la 8 hours halina mshiko, maana hata kwenda Dubai ni kama 5 hours tu halafu kuna ndege kubwa na maanisha kubwa kama airbus 380 inatoka Dubai to Mumbai kama 2 hours tu sasa hii ya dreamline utasema sijui ina ukubwa gani. na nchi nyingi wanatumia Boeng na ndege zingine kubwa kwa domestic routes na safari za 1 mpaka 2 hours. labda hoja ingekuwa je ATCL walikuwa wa business ideas hii ndege itakuwa inapiga route zipi na vizuri wakachagua nchi za east africa halafu shusha bei kidogo watapata sana maana bado kusafiri within EA na ghali sana sijui ni kwanini maana kwenda Dubai ni rahisi kuliko kwenda Kenya nadhani sababu hakuna ushindani na hii ni nafasi ya kuchukuwa business.
Bado tu unaweweseka
 
Back
Top Bottom