Ndugu zangu naomba niwahabarishe kwamba ndege ndogo iliyokuwa imebeba watu wanne imeanguka mara baada ya kupaa kutoka katika uwanja wa ndege wa Sumbawanga, leo mnamo saa kumi kasoro jioni. Kizuri ni kwamba wote waliokuwemo wamepona. Chanzo cha ajari hakijawekwa wazi. Ndege hiyo yasemekana ilikuja kumchukua mgonjwa mmoja kumpeleka hospitali ya rufaa. Cha kushangaza ni kwamba hawa jamaa wa zimamoto (firefighters) wamefika baada ya nusu saa. Pongezi ziwaendee jamaa wa ambulance ambao wamefika baada ya muda mchache kama dakika 7. Hali ya uwanja mbaya kama nini labda ndo maana mgombea kigoda ameahidi kama kawaida yake kuujenga. Tusubiri tuone.