Ndege yaanguka sumbawanga

Kidagaa

Member
Nov 17, 2008
9
0
Ndugu zangu naomba niwahabarishe kwamba ndege ndogo iliyokuwa imebeba watu wanne imeanguka mara baada ya kupaa kutoka katika uwanja wa ndege wa Sumbawanga, leo mnamo saa kumi kasoro jioni. Kizuri ni kwamba wote waliokuwemo wamepona. Chanzo cha ajari hakijawekwa wazi. Ndege hiyo yasemekana ilikuja kumchukua mgonjwa mmoja kumpeleka hospitali ya rufaa. Cha kushangaza ni kwamba hawa jamaa wa zimamoto (firefighters) wamefika baada ya nusu saa. Pongezi ziwaendee jamaa wa ambulance ambao wamefika baada ya muda mchache kama dakika 7. Hali ya uwanja mbaya kama nini labda ndo maana mgombea kigoda ameahidi kama kawaida yake kuujenga. Tusubiri tuone.
 
Ndugu zangu naomba niwahabarishe kwamba ndege ndogo iliyokuwa imebeba watu wanne imeanguka mara baada ya kupaa kutoka katika uwanja wa ndege wa Sumbawanga, leo mnamo saa kumi kasoro jioni. Kizuri ni kwamba wote waliokuwemo wamepona. Chanzo cha ajari hakijawekwa wazi. Ndege hiyo yasemekana ilikuja kumchukua mgonjwa mmoja kumpeleka hospitali ya rufaa. Cha kushangaza ni kwamba hawa jamaa wa zimamoto (firefighters) wamefika baada ya nusu saa. Pongezi ziwaendee jamaa wa ambulance ambao wamefika baada ya muda mchache kama dakika 7. Hali ya uwanja mbaya kama nini labda ndo maana mgombea kigoda ameahidi kama kawaida yake kuujenga. Tusubiri tuone.
hawa jamaa mara nyingine tunawalaumu bure tu, hivi wataota kama kuna tukio bila kujulishwa?wamefika baada ya nusu saa walijulishwa baada ya muda gani, inaweza kuiwa response yao ni nzuri, labda dakika moja toka walipotaarifiwa. haijalishi hata kama wangefika baada ya wiki moja so long as ndiyo muda waliopata taarifa. ushauri wa bure kunapokuwa na tukio linalowahitaji wazimamoto tuwe wepesi kutoa taarfifa badala ya kusubiri watafika baada ya muda gani withou notifying them...
 
hawa jamaa mara nyingine tunawalaumu bure tu, hivi wataota kama kuna tukio bila kujulishwa?wamefika baada ya nusu saa walijulishwa baada ya muda gani, inaweza kuiwa response yao ni nzuri, labda dakika moja toka walipotaarifiwa. haijalishi hata kama wangefika baada ya wiki moja so long as ndiyo muda waliopata taarifa. ushauri wa bure kunapokuwa na tukio linalowahitaji wazimamoto tuwe wepesi kutoa taarfifa badala ya kusubiri watafika baada ya muda gani withou notifying them...
Duh zimamoto huyu!!!!!!!!!!!!!
 
Kwanza wamejitahidi kufika mapema!! Ile ajali ya moto jengo la mkuu wa mkoa Dodoma gari ziko karibu lakini zilichukua muda kibao kuonekana tena moja tu kati ya matatu likiwa na maji kiduchu kabisa. Cha kumshukuru Mungu hao abiria wamepona. Kwa ajali ya ndege most of the time ni miracle ukiokoka kufa!!
 
Poleni sana wahanga.
Pia twashauri uwanja uwekwe katika hali nzuri.
 
Ndugu zangu naomba niwahabarishe kwamba ndege ndogo iliyokuwa imebeba watu wanne imeanguka mara baada ya kupaa kutoka katika uwanja wa ndege wa Sumbawanga, leo mnamo saa kumi kasoro jioni. Kizuri ni kwamba wote waliokuwemo wamepona. Chanzo cha ajari hakijawekwa wazi. Ndege hiyo yasemekana ilikuja kumchukua mgonjwa mmoja kumpeleka hospitali ya rufaa. Cha kushangaza ni kwamba hawa jamaa wa zimamoto (firefighters) wamefika baada ya nusu saa. Pongezi ziwaendee jamaa wa ambulance ambao wamefika baada ya muda mchache kama dakika 7. Hali ya uwanja mbaya kama nini labda ndo maana mgombea kigoda ameahidi kama kawaida yake kuujenga. Tusubiri tuone.

Ndugu Kidagaa!

Taarifa yako ni njema sana, lakini inakosa vipengele vya muhimu sana ili kuikamilisha!
-Je ndege hiy ni mali ya nani?...ya serikali...ya kibinafsi... ya mashirika ya Hifadhi za Taifa au Msalaba mwekundu?
-Je namba za usajili(registration No and Marks) ni zipi?
-Ilikuwa ikielekea wapi?
Nadhani ukitufahamisha hayo utakuwa umeboresha sana habari hii, unless kama nia yako ilikuwni kuwang'ong'a zimamoto!

 
Back
Top Bottom