Ndege ya Fastjet yaharibika,yashindwa kuruka kwenda Mbeya,bi harusi aangua kilio kuchelewa send-off

Ngaliba Dume

JF-Expert Member
Oct 6, 2010
1,710
3,669
Wakuu jioni hii nilikuwa nasafiri na Fastjet ya kwenda Mbeya,nilifika mapema sana uwanjani kwa ajili ya kuwahi safari yangu

Kufika pale uwanjani,nikafanya kuchekiwa na mpaka kupewa "boarding Pass" kuelekea Mbeya.Muda ukafika tukaingia mpaka katika ndege na kukaa tayari kwa kuondoka.Baada kama ya dakika 20 tukatangaziwa kuwa ndege ni mbovu hivyo haiwezi kwenda Mbeya.

Abiria wote tukaambiwa tushuke,watu wakawa wabishi pale na kelele za hapa na pale.Tumeuliza tatizo ni nini?Wanasema tu ni "Technical Faults"...Mle ndani ikawa joto sana mpaka wakalazimika kufungua mlango wa mbele na ule wa nyuma wa kushoto na kulia.

Baada kama ya saa moja hivi,ikaamuliwa wote tushuke na tukutane pale nje ili tupewe utaratibu.Lakini ukweli ni kuwa safari ya Mbeya leo hakuna,na nasikia hata kesho pia hakuna.Ukiwauliza wanasema ndege ni mbovu.

Nilikuwa nimekaa seat moja na bibi harusi mtarajiwa,ambaye jana alishindwa pia kwenda Mbeya sababu ndege ilijaa(overbooking) na leo pia ndege ni mbovu.Huyu bibi harusi mtarajiwa ana "send off" yake kesho.Nimemuacha hapo analia kama mtoto...Hata kesho akichukua "Super Feo" lazima atafika Mbeya wakati watu washaingia ukumbini.Fastjet wanasema kwa sasa ndege ya kwenda Mbeya ipo moja tu mchana saa 1430hrs,ile ya asubuhi wameifuta.

Lakini ajabu tukiwa palepale uwanjani,tumesikia ndege ya Fastjet inaondoka kwenda Mwanza,na wanatangaza abiria wa Mwanza kwa kutumia Fastjet wapitee geti namba fulani tayari kwa safari.

Sasa huu ubovu wa ndege ni kwa safari ya Mbeya tu??Wengine tulikuwa na safari za haraka za kibiashara na kesho asubuhi tulihitajika,sasa hata kesho tena uhakika hakuna?Kumbe sio ATCL tu,hata Fastjet nao wamepaki "bombadia" yao!!Usafiri wa anga ni kiboko
 
wanamuonea bure chenge. Yeye alikuwa anatekeleza ilani ya ccm ya kuliibia taifa...
Ccm akiwemo magufuli ni wapumbavu sana kwa sababu haya yote ni sababu yao wote kwa umoja wao dhidi ya rasilimali za watz. Alafu wanaunda mitume kwa kuwapa ulaji wa bure watu wkt walipitisha haya yote kwa mbwembwe huku wakiwatukana watz matusi ya nguoni.
Shame on them ccm + their corrupt leaders
 
wanamuonea bure chenge. Yeye alikuwa anatekeleza ilani ya ccm ya kuliibia taifa...
Ccm akiwemo magufuli ni wapumbavu sana kwa sababu haya yote ni sababu yao wote kwa umoja wao dhidi ya rasilimali za watz. Alafu wanaunda mitume kwa kuwapa ulaji wa bure watu wkt walipitisha haya yote kwa mbwembwe huku wakiwatukana watz matusi ya nguoni.
Shame on them ccm + their corrupt leaders
Mkuu una hasira sana na chama dola,mpaka unachanganya madesa...Pole sana
 
Wakuu jioni hii nilikuwa nasafiri na Fastjet ya kwenda Mbeya,nilifika mapema sana uwanjani kwa ajili ya kuwahi safari yangu

Kufika pale uwanjani,nikafanya kuchekiwa na mpaka kupewa "boarding Pass" kuelekea Mbeya.Muda ukafika tukaingia mpaka katika ndege na kukaa tayari kwa kuondoka.Baada kama ya dakika 20 tukatangaziwa kuwa ndege ni mbovu hivyo haiwezi kwenda Mbeya.

Abiria wote tukaambiwa tushuke,watu wakawa wabishi pale na kelele za hapa na pale.Tumeuliza tatizo ni nini?Wanasema tu ni "Technical Faults"...Mle ndani ikawa joto sana mpaka wakalazimika kufungua mlango wa mbele na ule wa nyuma wa kushoto na kulia.

Baada kama ya saa moja hivi,ikaamuliwa wote tushuke na tukutane pale nje ili tupewe utaratibu.Lakini ukweli ni kuwa safari ya Mbeya leo hakuna,na nasikia hata kesho pia hakuna.Ukiwauliza wanasema ndege ni mbovu.

Nilikuwa nimekaa seat moja na bibi harusi mtarajiwa,ambaye jana alishindwa pia kwenda Mbeya sababu ndege ilijaa(overbooking) na leo pia ndege ni mbovu.Huyu bibi harusi mtarajiwa ana "send off" yake kesho.Nimemuacha hapo analia kama mtoto...Hata kesho akichukua "Super Feo" lazima atafika Mbeya wakati watu washaingia ukumbini.Fastjet wanasema kwa sasa ndege ya kwenda Mbeya ipo moja tu mchana saa 1430hrs,ile ya asubuhi wameifuta.

Lakini ajabu tukiwa palepale uwanjani,tumesikia ndege ya Fastjet inaondoka kwenda Mwanza,na wanatangaza abiria wa Mwanza kwa kutumia Fastjet wapitee geti namba fulani tayari kwa safari.

Sasa huu ubovu wa ndege ni kwa safari ya Mbeya tu??Wengine tulikuwa na safari za haraka za kibiashara na kesho asubuhi tulihitajika,sasa hata kesho tena uhakika hakuna?Kumbe sio ATCL tu,hata Fastjet nao wamepaki "bombadia" yao!!Usafiri wa anga ni kiboko
Hii ni ya leo tarehe 12/06/2017 au ni wiki mbili zilizopita?
 
Hapa ndio ingekuwa ATCL,basi watu wangetukana sana na huko insta kusingekalika kabisa leo
Yaani my dear ATCL anaandamwa sana...Nipo mbali na nyumbani,ngoja nitafute vyanzo vyangu,wanambie nini kimeikumba fastjet?Kwamba wanaenda Mwanza lakini si Mbeya?

Ila kama ilifika saa 1625hrs bado mpo Dsm,isingewezekana kwenda Mbeya,maana uwanja wa Mbeya hauna taa,unategemea muda wa Sunset na Sunrise.

Sasa leo jua Mbeya limezama saa 1723 bila shaka,Fastjet isingeruhusiwa kuruka kuja Dsm wakati wa machweo,hata kama kwa macho ya kinyakyusa ungekuwa unauona mwanga.

Nasubiri vyanzo vyangu,nitarudi hapa....
 
wanamuonea bure chenge. Yeye alikuwa anatekeleza ilani ya ccm ya kuliibia taifa...
Ccm akiwemo magufuli ni wapumbavu sana kwa sababu haya yote ni sababu yao wote kwa umoja wao dhidi ya rasilimali za watz. Alafu wanaunda mitume kwa kuwapa ulaji wa bure watu wkt walipitisha haya yote kwa mbwembwe huku wakiwatukana watz matusi ya nguoni.
Shame on them ccm + their corrupt leaders
Japo umeenda nje ya mada lakini imebidi nikupe ka bonus kidogo
 

Attachments

  • VID-20170612-WA0043.mp4
    4.9 MB · Views: 26
Ndo tatizo la kuwa na ndege moja, ndege ilichelewa kutoka kilimanjaro, sasa ukichanganya na hiyo snag, kulekebisha muda ushaenda , songwe airport hauna taa,wangekuwa waungwana wangeenda kesho asubuhi, lakini ndiyo hivyo tena, si mara ya kwanza Fast jest kufanya huu ujinga..pole kwa bi harusi..
 
Hawa watu hawajafungiwa bado last year pale Nairobi kidogo nipige MTU yaani siku mbili tumesubiri ndege mwisho ilibidi nikate ticket niondoke na Kenya airways
 
Fastjet is dying.kibaya zaidi hata sisi ni full maujinga.Tuna ground ndege kisa PMU na FInance wamechelewesha malipo.Ndege nyingine inazingua na sababu kubwa zinalalia kwenye sabotage
 
wanamuonea bure chenge. Yeye alikuwa anatekeleza ilani ya ccm ya kuliibia taifa...
Ccm akiwemo magufuli ni wapumbavu sana kwa sababu haya yote ni sababu yao wote kwa umoja wao dhidi ya rasilimali za watz. Alafu wanaunda mitume kwa kuwapa ulaji wa bure watu wkt walipitisha haya yote kwa mbwembwe huku wakiwatukana watz matusi ya nguoni.
Shame on them ccm + their corrupt leaders
Povu
 
Hapa ndio ingekuwa ATCL,basi watu wangetukana sana na huko insta kusingekalika kabisa leo
Yaani my dear ATCL anaandamwa sana...Nipo mbali na nyumbani,ngoja nitafute vyanzo vyangu,wanambie nini kimeikumba fastjet?Kwamba wanaenda Mwanza lakini si Mbeya?

Ila kama ilifika saa 1625hrs bado mpo Dsm,isingewezekana kwenda Mbeya,maana uwanja wa Mbeya hauna taa,unategemea muda wa Sunset na Sunrise.

Sasa leo jua Mbeya limezama saa 1723 bila shaka,Fastjet isingeruhusiwa kuruka kuja Dsm wakati wa machweo,hata kama kwa macho ya kinyakyusa ungekuwa unauona mwanga.

Nasubiri vyanzo vyangu,nitarudi hapa....
Kaka barafu we ni rubani wa ATCL? :D
 
Back
Top Bottom