Air Tanzania iliokuwa inaondoka leo Kigoma nusura kuanguka wakati ikiruka na imejipiga chini ndani ya bwawa ila hakuna abiria aliyepoteza maisha.
========
Habari zaidi..
Ndege pekee ya Shirika la Ndege la Tanzania "Air Tanzania" imepata ajali wakati ilipokuwa inajiandaa kuanza safari ya kutoka Kigoma kuelekea Dar es Salaam, kupitia Tabora.
Ajali hiyo ilitokea jana Jumatatu milango ya saa 4 na robo asubuhi kwa saa za eneo hilo, ikiwa na abiria 35 na wafanyakazi wanne.
Ndege hiyo iliteleza wakati ilipokuwa inajitayarisha kuruka. Wanawake wawili wazee wamekimbizwa hospitalini kutokana na mshituko waliopata.
Kuna taarifa mbalimbali zimetolewa kuhusu sababu ya ajali hiyo huku baadhi wakisema kuwa barabara ya kurukia ndege ilikuwa inateleza sana huku wengine wakisema kuwa kufeli kwa injini ya ndege ndiko kulikosababisha ndege hiyo ilale upande wa kulia na kuharibika sehemu ya mbele, bawa na injini ya pangaboi.
========
Habari zaidi..
Ndege pekee ya Shirika la Ndege la Tanzania "Air Tanzania" imepata ajali wakati ilipokuwa inajiandaa kuanza safari ya kutoka Kigoma kuelekea Dar es Salaam, kupitia Tabora.
Ajali hiyo ilitokea jana Jumatatu milango ya saa 4 na robo asubuhi kwa saa za eneo hilo, ikiwa na abiria 35 na wafanyakazi wanne.
Ndege hiyo iliteleza wakati ilipokuwa inajitayarisha kuruka. Wanawake wawili wazee wamekimbizwa hospitalini kutokana na mshituko waliopata.
Kuna taarifa mbalimbali zimetolewa kuhusu sababu ya ajali hiyo huku baadhi wakisema kuwa barabara ya kurukia ndege ilikuwa inateleza sana huku wengine wakisema kuwa kufeli kwa injini ya ndege ndiko kulikosababisha ndege hiyo ilale upande wa kulia na kuharibika sehemu ya mbele, bawa na injini ya pangaboi.