Omutwale
JF-Expert Member
- Feb 4, 2008
- 1,429
- 1,045
Awali ya yote nawaomba Mods wasiuunganishe huu uzi wala kuuhamisha hapa. Lengo la huu uzi ni kudhihirisha ujungu kuu wa JF. Hivyo, hapa nitarejesha nyuzi mbalimbali za miaka kadhaa nyuma iliyotoa mwangwi wa hiki kinachodhihirika kwa wengi hivi leo juu ya vijana wa CHADEMA.
Tuanze na uzi huu wa December, 2011: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...n-saanane-waweza-kuanzisha-chama-kingine.html
Ukweli wake unathibitika kwenye kitubio (Confession) ya Ben Saanane mwaka huu. Soma hapa chini:
Tuanze na uzi huu wa December, 2011: https://www.jamiiforums.com/jukwaa-...n-saanane-waweza-kuanzisha-chama-kingine.html
Ukweli wake unathibitika kwenye kitubio (Confession) ya Ben Saanane mwaka huu. Soma hapa chini:
Tulikubaliana katika kundi hili tuwe na mkakati wa siri na tukusanye fedha nje na ndani ya chama.suala la kukusanya fedha nje ya chama nililipinga sana.Nakumbuka Mchange ndiye aliyeleta wazo la kukusanya fedha nje ya chama.miongoni mwa walengwa walikua
-David Kafulila
-Mwigulu Nchemba
-Deo Filikunjombe
na baadhi ya wafanyabiashara
Draft niliyoandika ilionekana kuwa na ushawishi mkubwa kwa wale ambao walikua potential donors.
Pia Habibu Mchange alileta taarifa kwenye kikao kwamba Zitto amemwambia tuandae bajeti ya kundi hili. Zitto alisafiri siku hiyo bila kutuambia na tulilalmika sana sana. Baada ya hapo alikua akiwasiliana na mtu mmoja mmoja. Hata hivyo kwa kuwa ulikua mpango wa siri nilipendekeza tutumie code names au namba zilizochanganywa na herufi kama mbinu mojawapo ya kijasusi. Mwishowe kila mmoja alikubaliana tutumie tu majina kwa kuwa walihofia kusahau code names.tulibatizana majina na jina langu likawa COBRA, Mchange-Mdude, Shonza-Benazir, Mwampamba-Kony na code name ambayo tuliitumia kwa Zitto ni Prezzo au Dogo
Role yangu mimi ilikua katika fedha baada ya majadiliano kwa kuwa kila mjumbe alisema Ben ndiye tunayemuamini pekee katika usimaizi wa fedha na kubuni vyanzo vya fedha. Nilipewa kazi ya kuandaa bajeti.Lakini nilikataa kwa kuwa nilisema bado siridhishwi na mwenendo wa kukusanya fedha nje ya chama.
Shonza Alikuwa Mwenyekiti wa PM7 strategically ili awe na wajibu mkubwa kwa kuwa alikua kiongozi wa juu wa BAVICHA. Mchange alijichagulia kuwa makamu Mwenyekiti, Mwampamba Katibu, Festo Sanga alipewa kazi ya kuandika kwenye mitandao kwa kutumia ID ya TUNTEMEKE akisaidiana na mchange na Mwampamba. Tulikubaliana iwe taasisi kwa kundi lote la Masalia ili itumike panapolazimika. Sikuwahi kuitumia kwa kuwa niliwaambia nitaendelea kutumia ID yangu kwa kuwa siatamtukana mtu au kuzusha kitu hata kama michango yangu ingeniweka matatani
Hata hivyo baadae nilikubali na niliandaa bajeti ya Sh. 25,000,000 kwa awamu ya kwanza na tukachora ramani ya jinsi tutakavyogawana mikoa.
Lengo lilikua kuingia mikoani hata kwa lazima na kufanya mikutano ya hadhara na kujenga mtandao. PM7 ilikuja kubadilika na malengo yakawa too narrow kwa kuwa yalilenga kuimarisha kundi ndani ya chama. Badala ya Patriotic Movement ilikuja kuwa PINDUA MBOWE-7. Lengo hapa lilikua kumtenganisha mwenyekiti na Katibu mkuu ili kundi liweze kuimarika na kupenya kati kati. Hapa ndipo kazi ambayo ilikua imekwisha anza mwezi wa 4 katika kampeni za Arumeru Mashariki ya kumchafua Mbowe na Katibu mkuu kwa kutumia ID ya TUNTEMEKE iliposhamiri
Actually, niliona hatari ya kukichafua chama hasa tuhuma zilizokuwa ziktumika zilikua tuhuma za uongo na uzushi.Wakati tunafanya maandalizi ya kufungua akaunti benki, nilikutana na Dr. Kitila kwa haraka na kumweleza kama zitto au yeyote amemweleza kuhusu kundi hili. Alinijibu kwamba hana taarifa hizo.Hata hivyo tulikubaliana tukutane haraka na Zitto tuweke mikakati mipya kwa kuwa alishangaa ni kwa nini amewahusisha akina Mchange na Mwampamba huku akijua siyo watu makini katika strateggy na ni waropokaji. Aliniomba nifanye mpango wa kulivuruga kundi hili na Pm-7 ife taratibu. Baadae alinieleza kwamba tutapanga siku tutoke nje ya Dar mimi, yeye na zitto tuweke mikakati upya kwa kuwa hapa dar tulikua tunafuatiliwa sana sana. Nilifanikiwa katika mipango hii ya kuiua Pm-7 taratibu na hata wakati mwingine tuligombana sana na baadae kwenye kiakao karibu na Pacific hotel pale Manzese, Mchange na Mwampamba waliibuka na hoja kwamba kuna haja ya kwenda kula viapo kwa mganga ili tusisalitiane katika kazi hii pm-&. Kwa bahati nzuri shonza, Mimi naMwakajila tulipinga vikali upuuzi huu. Shonza hili unalijua na unajua ni kiasi gani nilikasirika siku hiyo. Uliniandikia Message na kunisihi tuendeleze kundi hili
Baada ya hapo wakati kikao cha bajeti kinaendelea Shonza na Mwampamba walinipigia simu kuhusu kikao cha dgharura na David Kafulila. Ilikuwa Tarehe 4/07/2012. Tulikutana Tamal Hotel. Kafulila alitudokeza juu ya kusajiliwa kwa chama cha CHAUMMA, tulijadili mambo mengi.Nilishirikishwa juu ya kujiunga na CHAUMMA na kuhakikisha kinasajiliwa rasmi kwa usajili wa kudumu. Kafulila alinisihi sana na kuniambia ndani ya CHADEMA yatanikuta yaliyomkuta yeye kwa hiyo tuungane. Nilimwambia nitafikiria. Hussein Bashe alikuja dakika za mwisho kwenye kiako kile. Yeye ni miongoni mwa mashuhuda. Kafulila aliniambia mzee Hashim Rungwe pia atajiunga na anafanya mawasiliano na Zitto. Tulipanga kukutana siku iliyofuata. Mwampamba alipewa kazi ya kuandika kwenye mitandao pamoja na Shonza. Siku hii mchange hakuwepo
Tarehe 7/07/2012 nilikuwa ndani ya Ofisi ya CHAUMMA. Nilitambulishwa kwa viongozi wote tukaweka mikakati. Mingine sitaiandika hapa kwa sasa. Walinipa kazi ya kuandika sera ya Vijana na sera ya mambo ya nje huku Kafulila akisema kwenye uchumi sera ya gesi atashirikiana na Zitto kwa kuwa wote wana utaalamu kutoka holand na Norway. Niliwakubalia kimkakati hasa nilipogundua wanapanga kupunguza kura za CHADEMA mwaka 2015 huku akiniahidi kwamba kundi kubwa litatoka CCM na CHADEMA baada ya chaguzi za ndani mwaka huu na mwaka ujao respectively. Aliniambia hata akina Hashim Rungwe wapo nyuma ya kundi hilo na vigogo wa CCM. Mliniambia CHAUMMA kitakua chama darasa. Kafulila anaweza kuthibitisha hili.
Katibu Mwenezi wa CHAUMMA ndg.Mawazo Athanas kutoka kigoma alinisihi sana nimsaidie na Zitto akiwa nje amemuhakikishia kwamba sisi tutamsaidia yaani masalia group au PM-7. Hapa Dr. Kitila mkumbo hakuhusika.Ikumbukwe Mawazo athanas alikua Mgombea Ubunge kwa tiketi ya NCCR-Mageuzi huko kigoma na baada ya kuhama alitaka kujiunga na CHADEMA. Nilimshawishi sana ajiunge na CHADEMA lakini baadae nilimsikia yupo CHAUMMA. Nilikuwa nikifahamiana naye hapo kabla. Tuliendelea kuwasiliana nae kwa karibu na pia nikamuahidi Kafulila na uongozi wa juu wa CHAUMMA kwamba nitatoa ushirikiano ila waandae vitendea kazi. Nitaweka baadhi ya mawasiliano yetu hapa. Hata ID ya CHAUMMA hapa JF niliifungua mimi nikiwa ndani ya Ofisi za CHAUMMA na tulipeana Password. Kafulila alitaka nimpe paswd yeye, Katibu Mwenezi na katibu mkuu huku akiahidi kwamba atampa zitto itakapobidi. Alinisihi nisiwape akina Mchange na wengine kwa kuwa wanaweza kuharibu na kuonyesha wazi kwamba lengo la CHAUMMA ni kuigawa CHADEMA. Alitaka tuende kimya kimya. Akina Mchange na Mwampamba waliendelea kutumia ID Fake na ID ya TUNTEMEKE. Hii ni sehemu ndogo tu,sitaki kuharibu mambo mengi hapa hasa nyeti kwa kwa chama.
Nitaendelea....Nikihitajika nitakuja tena